Msameheni bure Job Ndugai, amechanganyikiwa baada ya kuomba msamaha batilifu uliokataliwa! Barua yake ya Kujiuzulu nayo pia ni batilifu!

Msameheni bure Job Ndugai, amechanganyikiwa baada ya kuomba msamaha batilifu uliokataliwa! Barua yake ya Kujiuzulu nayo pia ni batilifu!

Paskali,
Mtu yeyote anayejiamini kupita kiasi kwa vile ana fedha, nguvu au madaraka hufanya maamuzi ya ovyo mara zote.

CCM ni chama kinachoamini katika hayo yote hapo juu. Kwa imani yangu naamini Job hajaandika ile barua bali amepelekewa tu asaini na yeye kwa vile yuko depressed akasaini content bila hata kujiridhisha addressee ni nani. Sidhani kama Job ni mbumbumbu wa kanuni kiasi cha kutoelewa alitakiwa kwanza amwambie nani kwamba anajiuzulu.

Kuthibitisha kauli yangu, ni kitendo cha Chongolo (KM CCM) kuthibitisha kupokea barua na yeye kukiuka Katiba zaidi na kumwandikia Katibu wa Bunge barua ya kumjulisha kujiuzulu kwa Spika. Huu utaratibu kausoma kwenye Katiba ipi? Kautoa kanuni gani?
ccm ni mambumbumbuuu, mwenyechair mbumbumbu, chief secretary mbumbumbu, mwenezi mbumbumbu, wanachama ndio basi tena
 
Ni cheo cha bunge alichokipata kwa njia ipi?!

Na ataanzaje kupeleka kwa mamlaka ya kibunge kabla hajawajuza waliomtuma?!

Na ingawaje Ibara ya 149 (1)(c) inamtaka Spika kuwasilisha TAARIFA bungeni pale anapojiuzulu, hizo ni protocol za kiofisi tu lakini hawezi kujiuzulu bila kuiarifu mamlaka iliyomtaka akagombee uspika!! Ni kama Rais tu, nae akijiuzulu, Ibara ya 149 (1)(b) inamtaka awasilishe TAARIFA kwa Spika, nazo ni protokali za kiofisi tu lakini hawezi kufanya hivyo bila kumwandikia kwanza Katibu wa Chama Chake!!

Neno taarifa nimeliweka kwa msisitizo kwa sababu tulichokiona sisi sio Barua ya Kujiuzulu bali taarifa ya kujiuzulu! Barua ya kujiuzulu ilienda kwa waliomtuma agombee uspika, nao wakapeleka nakala kwa Katibu wa Bunge ambae nae akatoa TAARIFA kwa umma!
Hivi ni nini hakieleweki mkuu ?

Utaratibu:
Angeandika barua kwenda kwa BUNGE (katibu), akatoa taarifa (nakala) kwa katibu wa CHAMA.

Alichofanya yeye Ndugai:
Ameandika barua kwenda kwa chama, nakala kwa Bunge. (Kwa kiingereza hii inaitwa Vice-versa)

Unachotueleza wewe:
1. Ndugai alipata uspika kwa dhamana ya chama chake.
2. Mlichokiona sio barua.

Basi acha nijadili hoja zako mbilj hapo juu japokua hazina uhusiano wowote na mada husika.

1. Ndugai kuwa spika kwa tiketi ya chama chake haimpi uhalali wa kujiuzulu uspika kwa utaratibu wowote ambao yeye anaona unafaa. Anatakiwa kufuata muongozo wa katiba maana kujiuzulu ni jambo la kikatiba lililowekewa utaratibu wake. Katiba ingeleekeza ajiuzulu kupitia kwenye chama, tusingekua na tatizo nae. Tunasikitika kusema kwamba katiba (ya sasa) haisemi hivyo mkuu.

2. Tulichokiona sio barua ila ni taarifa kwa umma juu ya kilichofanyika. Kwa mujibu wa taarifa hiyo inatueleza kwamba barua (ambayo ni kweli hatujaiona) imekwenda kwa katibu wa chama, nakala ikaenda kwa katibu wa bunge.
Unataka uione barua wewe mwenyewe ili ujiridhishe kwa kilichofanyika ? Haumwamini Ndugai, Chongolo na Katibu wa bunge ambao wote kwa nyakati tofauti wamesema barua imeenda kwa katibu wa chama na nakala yake kupelekwa kwa katibu wa bunge ?

Screenshot_20220107-073422_Instagram.jpg


Tazama hii
 
Hiyo sio barua ya kujiuzulu ni barua ya kutoa taarifa kuwa ameandika barua ya kujiuzulu, tunasubiri barua yenyewe ya kujiuzulu ameandikaje maana hiyo bado haijawekwa hadharani.
Aliyepelekewa barua ana hili la kusema:
Screenshot_20220107-073422_Instagram.jpg
 
Hivi ni nini hakieleweki mkuu ?

Utaratibu:
Angeandika barua kwenda kwa BUNGE (katibu), akatoa taarifa (nakala) kwa katibu wa CHAMA.

Alichofanya yeye Ndugai:
Ameandika barua kwenda kwa chama, nakala kwa Bunge. (Kwa kiingereza hii inaitwa Vice-versa)

Unachotueleza wewe:
1. Ndugai alipata uspika kwa dhamana ya chama chake.
2. Mlichokiona sio barua.

Basi acha nijadili hoja zako mbilj hapo juu japokua hazina uhusiano wowote na mada husika.

1. Ndugai kuwa spika kwa tiketi ya chama chake haimpi uhalali wa kujiuzulu uspika kwa utaratibu wowote ambao yeye anaona unafaa. Anatakiwa kufuata muongozo wa katiba maana kujiuzulu ni jambo la kikatiba lililowekewa utaratibu wake. Katiba ingeleekeza ajiuzulu kupitia kwenye chama, tusingekua na tatizo nae. Tunasikitika kusema kwamba katiba (ya sasa) haisemi hivyo mkuu.

2. Tulichokiona sio barua ila ni taarifa kwa umma juu ya kilichofanyika. Kwa mujibu wa taarifa hiyo inatueleza kwamba barua (ambayo ni kweli hatujaiona) imekwenda kwa katibu wa chama, nakala ikaenda kwa katibu wa bunge.
Unataka uione barua wewe mwenyewe ili ujiridhishe kwa kilichofanyika ? Haumwamini Ndugai, Chongolo na Katibu wa bunge ambao wote kwa nyakati tofauti wamesema barua imeenda kwa katibu wa chama na nakala yake kupelekwa kwa katibu wa bunge ?

View attachment 2072186

Tazama hii
Man,

Kasome vizuri hiyo katiba (Ibara ya 149.1.c) halafu uone kama inasema ataandika barua kwenda kwa bunge au atawasilisha taarifa kwa bunge!

Ukishaelewa ikiwa ibara husika inazungumzia barua au taarifa, kisha rudi kwenye tukio zima uone Bunge limesema limepokea nini kutoka kwa Katibu Mkuu wa CCM!!
 
udini udi ni udini udini udini udini bi shost
Kama kwa "udini" unamaanisha Uislam, basi upo sahihi 100% Uislam wangu inakukera nini? I am so proud to be a Muslim.

Kama huna dini ni tatizo lako sio langu. Mimi na dini yangu inakuuma nini?
 
Ni spika wa hovyo kuwahi kutokea Tanzania nchi imeendelea kuwa na sheria mbovu za kodi na Tozo kwa sababu kiongozi wao alikua aishauri vizuri serikali na pia kitengo cha kumkataa CAG mtiifu kwa wananchi ndio kimempoteza wengi tulisikitika kwa alichokifanya ukiendelea kutetea uovu karma ipo Pascal na huyo kahukumiwa na karma kutokana na matendo yake mabovu...
 
Man,

Kasome vizuri hiyo katiba (Ibara ya 149.1.c) halafu uone kama inasema ataandika barua kwenda kwa bunge au atawasilisha taarifa kwa bunge!

Ukishaelewa ikiwa ibara husika inazungumzia barua au taarifa, kisha rudi kwenye tukio zima uone Bunge limesema limepokea nini kutoka kwa Katibu Mkuu wa CCM!!
Uwe na siku njema mkuu.
 
Paskali,
Mtu yeyote anayejiamini kupita kiasi kwa vile ana fedha, nguvu au madaraka hufanya maamuzi ya ovyo mara zote.

CCM ni chama kinachoamini katika hayo yote hapo juu. Kwa imani yangu naamini Job hajaandika ile barua bali amepelekewa tu asaini na yeye kwa vile yuko depressed akasaini content bila hata kujiridhisha addressee ni nani. Sidhani kama Job ni mbumbumbu wa kanuni kiasi cha kutoelewa alitakiwa kwanza amwambie nani kwamba anajiuzulu.

Kuthibitisha kauli yangu, ni kitendo cha Chongolo (KM CCM) kuthibitisha kupokea barua na yeye kukiuka Katiba zaidi na kumwandikia Katibu wa Bunge barua ya kumjulisha kujiuzulu kwa Spika. Huu utaratibu kausoma kwenye Katiba ipi? Kautoa kanuni gani?
Sahihi kabisa Barua ameandikiwa. Toka lini barua genuine yote ikaandikwa kwa herufi kubwa halafu anayepelekewa siyo mhusika.
 
Waliomshinikiza kujiuzulu ni CCM na siyo bunge. Si muliwaona kwenye kikao kile pale ikulu, wenyeviti wa mikoa yote wa ccm pamoja na katibu mkuu wao wakitoa cheche bila huruma ikizingatiwa kuwa Ndugai ni mgonjwa na afya yake si nzuri kwa muda mrefu. Hata hayo maudhi aliyoyatamka kwenye hicho kikao cha wagogo wenzake baada kupona mafua makali ya labda omicron, bila shaka ni kutokana na maradhi hayo. Hivyo it was proper kui address barua hiyo ya kujiuzulu kwa hao waliomshinikiza kujiuzulu kwani watu hao (CCM) ndiyo wangalimung'oa huo usipika kama hangalijiuzulu. Kwa hasira walizokuwa nazo watu hawa wangaliweza hata kuufuta uanachama wake wa ccm na hivyo kuukosa hata huo ubunge wake.
 
Kwanini Chongolo aliipokea ile barua na eti kuifanyia kazi? Kwanini Katibu wa bunge kakubali copy na eti anaendelea na mchakato wa kumpata speaker? Kwanini AG yupo kimya?

Tunatengeneza taifa la mazuzu
 
Wanabodi,

Naomba kuanza kwa declaration of Interest
Kwa vile mimi ni mmoja wa waandishi wachache waliowahi kuitwa kuhojiwa na Kamati ya Bunge kwa maandiko yangu, ya kulituhumu Bunge kujipendekeza kwa serikali, hivyo inaweza kuonekana nafurahia kinachompata Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai!. No!. Huyu ni Mkuu wa Mhimili wa Bunge wenye jukumu la kuisimamia serikali, haitakiwa Spika kujipendekeza kwa Executive, inambidi Mkuu wa Executive amuogope na kumheshimu Mkuu wa Bunge na Mahakama, siungi mkono jinsi Job Ndugai alivyodhalilishwa vile pale juzi.

Hili ni bandiko la kupinga ubatili unaendelea katika hili sakata la Spika. Baada ya Spika wetu Job Ndugai kutoa yale matamshi ya ukweli ya kizalendo kwa taifa letu kuhusu mikopo na deni la taifa, halafu akaja kuikana kauli yake na kuomba msamaha batilifu, kwanza niliuliza, Viongozi wetu wanapofanya makosa ya wazi waishie tu kuomba msamaha kisha 'life as usual', au tujenge utamaduni wa kuwajibika kama enzi za Nyerere? kisha nikauzungumzia msamaha batilifu, Ndoa halali, ndoa batili na ndoa batilifu. Je, wajua pia kuna msamaha halali wa kweli, msamaha batili na msamaha batilifu? Msamaha ule ni batilifu! ambao ulikataliwa, na mara baada ya msamaha huo kukataliwa nikauliza tena Baada ya maneno haya ya Rais Samia, kama ni timamu, je, tumshauri to do "The needful?" au akomae nao, till they do him away?

Jana barua hii ya taarifa kwa umma toka kwa Spika kuwa ameandika barua ya kujiuzulu uspika
View attachment 2071447
imesambaa kote. Kama ni kweli hii ndio barua ya Spika Job Ndugai kuuarifu umma kuwa ameandika barua ya kujiuzulu uspika, na kuipeleka kwa Katibu Mkuu wa CCM, kiukweli this looks fake!, ila kama sio fake, then tumsamehe bure Mhe. Job Ndugai, huku kutakuwa ni kutokana na kuchanganyikiwa tuu, barua hii nayo ni barua batilifu!, kwasababu kujiuzulu kwake kumekuwa addressed to a wrong person and to a wrong Institution. Bunge ni mhimili, Mkuu wa mhimili wa Bunge hawezi kujiuzulu kwa barua batilifu na tukaacha tuu hivi hivi, what precedence tunaweka for records?.

Nashauri barua hii ikataliwe, Spika aandike a proper letter ya kujiuzulu kwenye a proper Bunge letterhead kama hii View attachment 2071452

Nakiri nimekuwa inspired kupandisha bandiko hili baada ya kumsoma mwana je huyu

Mkuu Yohane Mbatizaji, johnthebaptist
it's true Job kachemsha!, barua ya kujiuzulu uspika ilipaswa kupelekwa kwa katibu wa Bunge, CCM ndio wanapewa copy. Spika wa Bunge ni Spika wa Bunge la JMT na sio Spika wa Bunge la CCM. Usika wake ni kwa mujibu wa katiba, na kujiuzulu pia kumeelekezwa na katiba anaandika barua kwa nani, na sio kwa CCM!.

CCM ilimpendekeza tuu, baada ya kuchaguliwa, anakuwa ni Spika wa Bunge la JMT na sio Spika wa CCM!, hivyo hata kujiuzulu, anajiuzulu kwa kumuandikia Katibu wa Bunge na sio Katibu wa CCM!. Kama Spika wa Bunge anayepaswa kuijua katiba na kuifuata, anaweza kujiuzulu kwa barua ya kienyeji namna hii, then this is a disgrace kwa nafasi ya Spika!.

Huu sio utaratibu wa kufuata wakati wa kujiuzulu kwa Spika wa Bunge. Ingekuwa anajiuzulu kwa kujivua uanachama wa CCM hivyo kupoteza uSpika hapo ndipo anapeleka barua ya kujiuzulu kwenye chama chake, hata angekuwa amejiuzulu ubunge, barua ya kujiuzulu inakuwa addressed kwa Spika wa Bunge. Japo chama ndicho kimemdhamini kugombea ubunge, na uspika lakini baada ya kuchaguliwa mbunge au Spika, umechaguliwa na Watanzania/Bunge la JMT, unawajibika kwa Bunge na sio kwa chama chako.

Kikatiba, Spika wa Bunge akijiuzulu anatakiwa kufanya kutumia Ibara ya 149(1)(c) ya Katiba ya JMT inayosema iwapo Spika wa Bunge atajiuzulu, basi taarifa ya kujiuzulu aliyoiandika na kuitia sahihi yake ataiwasilisha kwenye Bunge.

Inakuwaje anaipeleka kwenye chama na Bunge lipokee nakala kutoka kwenye chama? . Msameheni bure tuu, Spika atakuwa amechanganyikiwa, maada kwa jinsi alivyokuwa anauringia na kuutambia, "mimi ni mhimili" halafu ghafla unatakiwa kuutema uspika, hata ningekuwa mimi, lazima mtu uchanganyikiwe!

Naendelea kusisitiza Shurti la kudhaminiwa na chama kugombea uchaguzi, ni shurti batili kwa mujibu wa Katiba, linatutia hasara, tulifute!.

Bunge ni mhimili, Spika anapatikana kwa mujibu wa katiba, na akijiuzulu pia anajiuzulu kwa mujibu wa katiba, hawezi kujiuzulu tuu hivi kienyeji enyeji kwa ubatili na kukubaliwa, hata kama ni kujiuzulu, then ajiuzulu kwa mujibu wa katiba, kama kifungu hiki kilivyoeleza

Mkuu Ukwaju thanks kwa kifungu hicho.

Hii tabia ya kuacha na kupuuzia mambo madogo madogo haya ya ubatili, it is now unbecoming, kuna siku tutajikuta tunatengeneza taifa la ubatili. Kama Katiba ndio sheria mama, na imeelekeza jinsi ya kufanyika kwa jambo fulani, there is no options and no negotiations katiba ifuatwe ajiuzulu properly kwa mujibu wa katiba na kujulia mafao yake manene ya 80% ya mshahara na marupurupu ya Spika.

Nakutakia Kustaafu Kwema, ndugu yangu na rafiki yangu, Job Ndugai.
Paskali

Mkuu Mayalla, hiyo sio barua; ni press release kama inavyojieleza!
 
Kuna wanaosema Ndugai katumia njia sahihi sababu Bunge bado halijaanza...

Kuna wewe unayesena kakosea kui address chamani, angei address bungeni...

Au angesubiri mpaka Bunge lianze ndiyo ajiuzuru....

Which is which?
karibu
P
 
Wanabodi,

Naomba kuanza kwa declaration of Interest
Kwa vile mimi ni mmoja wa waandishi wachache waliowahi kuitwa kuhojiwa na Kamati ya Bunge kwa maandiko yangu, ya kulituhumu Bunge kujipendekeza kwa serikali, hivyo inaweza kuonekana nafurahia kinachompata Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai!. No!. Huyu ni Mkuu wa Mhimili wa Bunge wenye jukumu la kuisimamia serikali, haitakiwa Spika kujipendekeza kwa Executive, inambidi Mkuu wa Executive amuogope na kumheshimu Mkuu wa Bunge na Mahakama, siungi mkono jinsi Job Ndugai alivyodhalilishwa vile pale juzi.

Hili ni bandiko la kupinga ubatili unaendelea katika hili sakata la Spika. Baada ya Spika wetu Job Ndugai kutoa yale matamshi ya ukweli ya kizalendo kwa taifa letu kuhusu mikopo na deni la taifa, halafu akaja kuikana kauli yake na kuomba msamaha batilifu, kwanza niliuliza, Viongozi wetu wanapofanya makosa ya wazi waishie tu kuomba msamaha kisha 'life as usual', au tujenge utamaduni wa kuwajibika kama enzi za Nyerere? kisha nikauzungumzia msamaha batilifu, Ndoa halali, ndoa batili na ndoa batilifu. Je, wajua pia kuna msamaha halali wa kweli, msamaha batili na msamaha batilifu? Msamaha ule ni batilifu! ambao ulikataliwa, na mara baada ya msamaha huo kukataliwa nikauliza tena Baada ya maneno haya ya Rais Samia, kama ni timamu, je, tumshauri to do "The needful?" au akomae nao, till they do him away?

Jana barua hii ya taarifa kwa umma toka kwa Spika kuwa ameandika barua ya kujiuzulu uspika
View attachment 2071447
imesambaa kote. Kama ni kweli hii ndio barua ya Spika Job Ndugai kuuarifu umma kuwa ameandika barua ya kujiuzulu uspika, na kuipeleka kwa Katibu Mkuu wa CCM, kiukweli this looks fake!, ila kama sio fake, then tumsamehe bure Mhe. Job Ndugai, huku kutakuwa ni kutokana na kuchanganyikiwa tuu, barua hii nayo ni barua batilifu!, kwasababu kujiuzulu kwake kumekuwa addressed to a wrong person and to a wrong Institution. Bunge ni mhimili, Mkuu wa mhimili wa Bunge hawezi kujiuzulu kwa barua batilifu na tukaacha tuu hivi hivi, what precedence tunaweka for records?.

Nashauri barua hii ikataliwe, Spika aandike a proper letter ya kujiuzulu kwenye a proper Bunge letterhead kama hii View attachment 2071452

Nakiri nimekuwa inspired kupandisha bandiko hili baada ya kumsoma mwana je huyu

Mkuu Yohane Mbatizaji, johnthebaptist
it's true Job kachemsha!, barua ya kujiuzulu uspika ilipaswa kupelekwa kwa katibu wa Bunge, CCM ndio wanapewa copy. Spika wa Bunge ni Spika wa Bunge la JMT na sio Spika wa Bunge la CCM. Usika wake ni kwa mujibu wa katiba, na kujiuzulu pia kumeelekezwa na katiba anaandika barua kwa nani, na sio kwa CCM!.

CCM ilimpendekeza tuu, baada ya kuchaguliwa, anakuwa ni Spika wa Bunge la JMT na sio Spika wa CCM!, hivyo hata kujiuzulu, anajiuzulu kwa kumuandikia Katibu wa Bunge na sio Katibu wa CCM!. Kama Spika wa Bunge anayepaswa kuijua katiba na kuifuata, anaweza kujiuzulu kwa barua ya kienyeji namna hii, then this is a disgrace kwa nafasi ya Spika!.

Huu sio utaratibu wa kufuata wakati wa kujiuzulu kwa Spika wa Bunge. Ingekuwa anajiuzulu kwa kujivua uanachama wa CCM hivyo kupoteza uSpika hapo ndipo anapeleka barua ya kujiuzulu kwenye chama chake, hata angekuwa amejiuzulu ubunge, barua ya kujiuzulu inakuwa addressed kwa Spika wa Bunge. Japo chama ndicho kimemdhamini kugombea ubunge, na uspika lakini baada ya kuchaguliwa mbunge au Spika, umechaguliwa na Watanzania/Bunge la JMT, unawajibika kwa Bunge na sio kwa chama chako.

Kikatiba, Spika wa Bunge akijiuzulu anatakiwa kufanya kutumia Ibara ya 149(1)(c) ya Katiba ya JMT inayosema iwapo Spika wa Bunge atajiuzulu, basi taarifa ya kujiuzulu aliyoiandika na kuitia sahihi yake ataiwasilisha kwenye Bunge.

Inakuwaje anaipeleka kwenye chama na Bunge lipokee nakala kutoka kwenye chama? . Msameheni bure tuu, Spika atakuwa amechanganyikiwa, maada kwa jinsi alivyokuwa anauringia na kuutambia, "mimi ni mhimili" halafu ghafla unatakiwa kuutema uspika, hata ningekuwa mimi, lazima mtu uchanganyikiwe!

Naendelea kusisitiza Shurti la kudhaminiwa na chama kugombea uchaguzi, ni shurti batili kwa mujibu wa Katiba, linatutia hasara, tulifute!.

Bunge ni mhimili, Spika anapatikana kwa mujibu wa katiba, na akijiuzulu pia anajiuzulu kwa mujibu wa katiba, hawezi kujiuzulu tuu hivi kienyeji enyeji kwa ubatili na kukubaliwa, hata kama ni kujiuzulu, then ajiuzulu kwa mujibu wa katiba, kama kifungu hiki kilivyoeleza

Mkuu Ukwaju thanks kwa kifungu hicho.

Hii tabia ya kuacha na kupuuzia mambo madogo madogo haya ya ubatili, it is now unbecoming, kuna siku tutajikuta tunatengeneza taifa la ubatili. Kama Katiba ndio sheria mama, na imeelekeza jinsi ya kufanyika kwa jambo fulani, there is no options and no negotiations katiba ifuatwe ajiuzulu properly kwa mujibu wa katiba na kujulia mafao yake manene ya 80% ya mshahara na marupurupu ya Spika.

Nakutakia Kustaafu Kwema, ndugu yangu na rafiki yangu, Job Ndugai.
Paskali
Paskali,Paskali,PaskaliiiWewe kama Learned Brother wakati mwingine ukitulia huwa unawashauri wana CCM wenzio vema.Ndugai hajakosea wala kuchanganyikiwa kwa lolote.Naamini hata wewe unaufahamu ukweli halisi.
He contradicted his resignation letter deliberetly just to comfuse Tanzanians who are straggling for The Better new Constitution.
It's just the same old Devide and Rule tactic from an old dying politicians.
 
Ukiona mapungufu madogo kama haya imagine sasa ndiyo alikua kiongozi wetu wa bunge akiratibu shughuli za bunge... Kavunja kanuni ngapi za bunge tumeona namna alivyo wapelekesha wapinzani
Kalifikisha pabaya sana Bunge la JMT.Maamuzi yake mengi kama Spika yameliumiza mno Taifa letu.He has set a very bad precedence.
Ndugai hakustahi kuwa hata mbunge kwa hulka zake hizo tulizoziona.
Ulazima wa Katiba upo dhahiri na hakuna tena dawa ya kuitibu Tanzania yetu zaidi ya hiyo.Tuanze upya,The damage is beyond repair.
 
Kalifikisha pabaya sana Bunge la JMT.Maamuzi yake mengi kama Spika yameliumiza mno Taifa letu.He has set a very bad precedence.
Ndugai hakustahi kuwa hata mbunge kwa hulka zake hizo tulizoziona.
Ulazima wa Katiba upo dhahiri na hakuna tena dawa ya kuitibu Tanzania yetu zaidi ya hiyo.Tuanze upya,The damage is beyond repair.
Umeongea vyema mkuu, nchi inachezewa chezewa sana hii
 
Back
Top Bottom