Ni jana wakitokea kisiwa cha Mbudya kurudi Jangwani Sea Breeze kwa mujibu wa maelezo yake kufika katikati boti ikazima na ikaanza kuingiza maji na taratibu ikaanza kwenda chini bahati nzuri walikuwa wamevaa life jackets ndio boti ilivyowaacha na kuzama wakabaki majini wakielea bila kujua la kufanya kwa muda wa saa mpaka walipopita wavuvi na kuwaokoa.
Anasema anashukuru Mungu kwa kuwaweka hai kwani lilikuwa ni jambo la hatari mno isipokuwa kuna mtu mmoja hajulikani alipo na hata ilipofanyika juhudi kurudi Mbudya kumtafuta hakuwepo huko.
Hayo ndiyo maelezo yake mzee wa Sofia Sofia.
Binafsi natia shaka usalama wa vyombo vile kwenda Mbudya pia suala zima la uokoaji pindi ikitokea janga mfano wa hili,wadau tusipende safari za huko pasipo umuhimu.