Msanii huyu anaitia aibu tasnia ya filamu

Msanii huyu anaitia aibu tasnia ya filamu

Sio bure, interest ya kufamfanyia utafiti mtu ambaye hakuhusu wala so ndugu yako siku kadhaa hadi akawa anafunga safari kwenda kufuatilia. Wewe Jesca unaona in kawaida? Kuna kitu nyuma ya pazia

Hivi wee jamaa unajua maana ya celeb?! Yani mtu akisha amua kuishi kistaa unafuatiliwa maisha yako hadi unapo lala! Na mleta thread kamfichua jamaa ni muuzaji mzuri tu wa madawa kwa maelezo ya mleta thread! Sasa wew unataka ayafanye siri! huenda ukawa unajua maovu mengi huko kitaa kwako ila unayafumbia macho mwisho wa siku likitokea balaa unakuja kujutia ningejua!!
 
Mkuu sijui habari yako inaukweli kiasi gani,lakini kwenye hilo la sembe usingelisema hapa,kama kweli ulitaka jamii ifahamu basi tungefahamu tu kwa yeye kuwa chini ya ulinzi wa polisi. Lakini hivo ulivyofanya ni kama umemuambia aanze kukimbia jambo litakalofanya kumpata kuwa kugumu.
Halafu mleta thread hajasimuliwa kaenda mwenyewe kajikita huko kambi hii habari
ina ukweli 75% ni sawa na hisa anazo miliki Manji pale Yanga!

Hivi wee jamaa una ndugu yako alieathirika na madawa kweli?
 
Kuna ujumbe mkubwa sana kwenye hii habari:

Hivi watu wa pwani wana matatizo yanayo fanana!kuuza rasilimali zao na kufanyia starehe! Ni rahisi kukuta wanafamilia wanauza nyumba ya urithi, wanagawana pesa. Na wao kwenda kupanga kwenye nyumba za wengine!!!Angalia maisha ya wasanii wa pwani na wengine wa huko bara, ni tofauti kabisa.Ni hii hii akili ya starehe starehe ndio iliyowatia umaskini watu wengi.Ukweli ni kwamba uongozi hatutatoa kwa watu wa pwani tena.
 
Sasa wewe baada ya kugundua mchizi anauza crack kwanini hukumreport police au umeridhishwa na anavyowapoteza vijana wenzio
 
fuata maisha yako kaka, kwani asipokuwa na kijiko si maisha yake , wewe yanakuhusu nn??

Watanzania jitaidini kufata ya kwenu yasiyo wahusu yapotezeeni
Sasa kama wewe ni mfata yako umeingia jf kutafuta nini kwan kuna mstari hata mmoja wa coding uiouandika katika hii app.....na kwanini usome huu .....tuoneshe mfano kwanza kwa wewe kufataa yako
 
"mtu mbeya huwa anasema kweli ila tu husema sehemu zisizostahili" mwanaume kumsengenya mwanaume mwenzake ni dalili za uoga na UKAOGE
Na haswa pale anaposhindwa kumfuata mwenyewe na kumwambia ukweli na badala yake anamsema kwenye mitandao.

Sijui ni uoga au?
 
Ndugu zangu nayasema haya si kwa chuki au unafki , ila wakati mwingine inabidi tuseme kama funzo kwa jamii yetu inayotuzunguka. Na si vyema kujadili maisha ya mtu lakini huyu ninayemjadili ni msanii tena ana jina kubwa tu, hawa ndio tunawaita kioo cha jamii hivyo wanapokwenda tofauti lazima tuseme.

Wapo wengi tu wenye tabia hii ambao huishi maisha yasiyo yao. Kwa sababu tu wanaitwa wasanii na wanajulikana kwenye jamii. Huyu msanii ni wa Bongo movie anaitwa Jumanne Mshindo. Ni msanii wa muda mrefu wengi mmnafaham wale wapenzi wa filamu za bongo. Ukimuona ni mtanashati kweli na Mungu kamjalia umbo lenye Pesa.
View attachment 388623
Katika tembea tembea yangu siku ya wikiendi, nikafika sehemu moja inaitwa Chamazi kwa rafiki yangu, kanunua huko kakibanda kake safi anakaa na familia yake. Wakati tunaendelea kupiga stori hapo nje maana nyumba yake haina fensi. Gafla nikamuona jamaa mnene anatokea kwenye nyumba ya pili yake nayo haina fensi ila ni ya zamani. Nikawa kama nimemfananisha, ikabidi niulize mwenyeji wangu, vipi huyo jamaa aliyepita hapo anafanana na msanii mmoja maarufu wa filamu. Jamaa akacheka, kisha akasema ni kweli wala ujamfananisha, Anaitwa Jumanne Mshindo na hapo ni kwao.

Nikamtania kumbe unaishi na wazazi wa msanii mkubwa hapa kwako, kilichonishangaza akaniambia sio naishi na wazazi wake pekee ata mwenyewe anaishi hapo, na nilipoaamia hapa toka mwezi 10 mwaka Jana nilimkuta hapa, anaishi maisha ya shida sana. Na hii Nyumba ninayoishi kaka yake ndiye aliyemuuzia aliyeniuzia Mimi baada ya kuikarabati. Baada ya kaka yake kuuza hii nyumba alivutia unga yote nae anaishi hapo kwao. Na ili eneo lote lenye majengo lilikuwa lao waliuza viwanja vyote wamebaki na nyumba hiyo moja ambayo haina hata nafasi ya watoto kucheza.

Sikuridhiki na maneno ya jamaa ikabidi mwenyewe niende Chamazi kwa wakati wangu kufanya utafiti. Kilichonishangaza zaidi baada ya utafiti kumbe ndiye muuza unga, kwa wale mateja wa Chamazi. Anashinda kwenye jumba bovu hapo jirani na mateja humzunguka kwa ajili ya huduma. Na anaishi hapo kwao kwa kipindi kirefu yeye na mke wake chumba kimoja, vyombo vyote kauza kabakiza kitanda tu. Nikaingia ndani kabisa kuhusu historia ya hapo nyuma ya familia yao. Baba yao alikuwa na uwezo mkubwa tu, baada ya kufariki, wakauza Nyumba pale mtoni, mashamba, viwanja n.k ikabaki Nyumba 1 iliyoko Chamazi ambayo mama yao anaishi sasa. Pesa nyingi wakagawana vijana wakala maisha.

Kilichosababisha niandike haya ni baada ya kubaini mama yao anateseka sana licha ya mtoto wake ana jina kubwa kwenye jamii na kwenye mitandao wanatupia vitu na maisha ya maigizo, ukiingia kwenye ukurasa wake Facebook unakuta kapiga picha suti kali, gari na funguo mkononi . Kumbe maigizo matupu. Walipouza Nyumba na viwanja vya uridhi yeye alikimbia kuwekeza kwenye movie, alinunua gari Kali, alipanga Nyumba nzima na furniture za kila aina, nguo za bei Kali, akawa anakesha bar kwamba aonekane ni staa mwenye Pesa. Bila kukumbuka kujenga, Pesa zilipoisha karudi kwao kumuangaisha mama yao na soko la movie halilipi kabisa. Hapo kwao ni familia kubwa sana, Nyumba ya vyumba 4, yeye anaishi chumba kimoja na mke, kaka yake nae mvuta unga chumba kimoja, kuna mdogo wake wa kike, bado wajukuu wa kike na wakiume na mama yao humohumo. Jamani hata Pesa ya kupanga chumba kimoja inakosekana unabaki kupishana na mama yako kwenye bafu moja? Kweli haya ndio maisha ya mtu mzima.
View attachment 388649

Wasanii badilikeni jaribuni kuishi maisha yenu halisi, kama huna sema sina, sio kudanganya watu kwenye mitandao mna maisha bora kumbe hakuna chochote, mnashindia mihogo. Fanyeni kazi zingine kama bongo movie haiwalipi, kuna mashamba kibao mkalime.
hii ni zaidi ya ubongo muvi wake,kuna kitu kati yako na yeye nyuma ya pazia hatukijui.....!!
 
Hapana huyu jamaa kasema wazi wazi bila kuficha, kuna ukweli hapa tena 90℅.
Sina shaka na habari yake, linalonipa shaka in muda wa kwenda kumfatilia huyo mtu maisha yake A-Z. Hajaniconvice kuwa hakuna kitu kati yake na mhusika. Ndio maana nasema wewe unamwamini? Kwasababu kama predictions zangu ziko sahihi katika moja ya habari alizoleta lazima chumvi iwepo, ukitaka kujua ni jamaa anavyokuwa mkali kwenye comment za wale wanaohoji,.
 
Back
Top Bottom