Msanii Lad JayDee kupelekwa mahakani siku ya Jumatatu...

Ninamini kuwa Jd ana advocate wake! Hawwezi kuitwa mahakamani kama vile ameitwa na baba yake. Kwenye order ya kuitwa mahakamani lazima wa ainishe anaitiwa nini. SO kama ana advocate mzuri anaweza kuweka objections regarding the event scheduled on 15th. Gharama na maandalizi aliyokwisha ingia might be considered otherwise.
Hope wakili wake anaweza ku act fast on this ssoonest. All the best JD
 
Tarehe 15 alikuwa anataka kufunguka zaidi kuhusu ruge na kusaga wala si tarehe ya show yake, show yake ni tarahe 30.
Na hapa RUGE anachotaka ni restrain order kutoka mahakamani ambayo itamfanya jyde asiendelee kufunguka zaidi.
Na kama amefungua case ni kuhusu defamation lakini asisahau na yeye alitumia chombo chake cha habari.

Nia yake ni kumziba komando jyde mdomo lakini sidhani kama ataweza.
Daa Ruge kumbe battle hawezi kabisa.
 
barua ya kuitwa shaurini lazima itaje shauri lenyewe, mshitaki na mshitakiwa. Ebu mwambieni aiweke hapa hiyo barua tuione, huenda huyu dada na yeye anatuchezea tu!

tomaso!
 
Mhaya gani mwenye roho mbaya kama za watu wa kaskazini?
 

Hicho ki jay dee chako nacho hakina akili.

Who telegraphs their next move to their nemesis?

Dumb move.
 
Mhaya gani mwenye roho mbaya kama za watu wa kaskazini?

Kaskazini hauikuhusu jamaa..japo im native wa kaskazin ya tz ila kaskazin ya tz ndo nimekuwa adopted and i am proud of that! So stick kwenye mada husika, naona na wewe ume panic kama hao vigeu geu...
 
Ule mnyukano wa Mbunge Mbilinyi@MrII na Ruge& clouds radio ilikuwa ni juu ya nn?
 
Mhaya gani mwenye roho mbaya kama za watu wa kaskazini?
Roho mbaya haina kabila, dini wala chama cha siasa. Na ubaya hauna kwao wala hauna Kabila! Wajua historia ya Wasamaria? Wengi wakisikia "Msamaria Mwema" hudhani Wasamaria ni watu wa huruma, matendo mema na ya haki. La hasha! Ni yule mmoja tu aliyemwonea huruma mtu aliyemkuta njiani akiwa ameshambuliwa na majambazi; wamemwibia kila kitu alichokuwa nacho, wamempiga wakamwacha karibu ya kufa. Yeye alipomkuta, alimwonea huruma, akamwendea akasafisha majeraha yake kwa divai na mafuta, akayafunga. Kisha akamweka kwenye punda wake akaenda naye mpaka nyumba ya wageni ambapo alimtunza. Kesho yake, yule Msamaria alipokuwa anaondoka, akampa mwenye nyumba ya wageni fedha akamwomba amtunze yule mgonjwa na akaahidi kulipa gharama yo yote ya ziada atakaporudi.

Ikumbukwe kwamba Kuhani mmoja naye alipita njia ile. Alipomwona huyo mtu, akapita upande mwingine wa barabara akamwacha hapo hapo. Vivyo hivyo Mlawi mmoja naye alipopita, alimwona, akapita upande mwingine wa barabara akamwacha hapo hapo.

Ajabu ni kwamba Makuhani na Walawi ni miongoni mwa watu waliokuwa wanahesabiwa haki na jamii ilihali Wasamaria lilikuwa kabila lililohesabika la wakorofi, wadhurumaji, wanyanganyi, wauaji, na kila baya lilihesabika kuwa upande wao. Huyu mmoja tu aliyemfanyia huruma mateka ndiye aliye BRAND upya kabila hili. Leo hii ukisema fulani "Msamaria Mwema", linaloingia vichwani mwa watu moja kwa moja ni kuwa fulani ni "Mtu wa Huruma!"

Muonekano wa mtu yeyote akiwemo Ruge kwenye jamii, haupaswi kuhusishwa na asili yake ya kuzaliwa. Isitoshe Ruge anaweza kuwa anaujua na kuuishi vema utamaduni na mila za Marekani na za Dar zaidi kuliko za Wahaya!
 
Mhaya gani mwenye roho mbaya kama za watu wa kaskazini?

HII NI VITA YA MKURYA NA MUHAYA.......

1.MUHAYA ANAJIFANYA MJUAJI NA ANA DHARAU
2.MKURYA NI MJEURI NA MKOROFI.....na haogopi kufa


ruge lazima asalimu amri....chezea wakurya wewe
 
Lets support Jide in her battle against oppressive and exploitative music cartel.This is double std ya Ruge.Dodoma eti wanapambana dhidi ya unyonyaji wa wasanii huku yeye anapambana kuendeleza unyonyaji huohuo kwa kuendesha kesi dhidi ya anayekataa kunyonywa.
Najua kesi ni private matter but one attract public interest.Hebu da Jide tuwekee nakala ya madai yako tuweze kuchangia mawazo just in case haita-prejudice case yenyewe.
I believe at the end truth will prevail.
 
Mwisho wa siku JD akubali yaishe anatafuta nini?kama ana washabiki wake atulie apambane na maisha yake!kwani lazima agombane na Clouds?wapenzi wake wa zamani?ajipange vema afungue hiyo radio yake,yeye afanye tofauti na Clouds ili iwe radio ya mfano chipukizi woote na wakongwe waache Clouds waende kwake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…