Msanii Rema anamzidi mbali Diamond Platinumz kifedha

B M F ICONIC

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2019
Posts
824
Reaction score
1,631
Kwa vigezo Hivi. Moja kwa moja twende kwenye Mada.

1. STREAMS KWA UPANDE WA SPOTIFY
Kwa upande wa hizi streaming platform Apple music ndo uongoza kwa kulipa vizuri ikifatiwa na Spotify, Youtube hulipa pesa ndogo zaidi. Kama unavyoona hapo chini
Ikumbukwe Diamond ni kinara upande wa Youtbe lakini kwenye platform nyingine hafanyi vizuri​

Spotify hulipa wasanii pesa kwa idadi ya streaams ya ngoma walizoingiza kwenya platform hio. Na hulipa kama unavyo ona hapo chini

UPande wa spotify Diamond ana streams
280,565,117

Na Rema ana Streams 4,103,463,149


KWa streams hizo.mpaka sasa Diamond kaingiza kiasi cha 1,122,260.468 Dollars sawsawa na Tsh 3,054,914,298

Kwa upande wa Rema, kwa streams hizo ameshaingizz kiasi cha 164,138,525.96 Dollar sawasaw na Tsh 44,680,279,462

(😂 kweli mziki unalipa .Na hapo tu ni Rema sio kina Wizkd, Burnaboy na davido
Wana JF na sisi tuingie kwenye usanii kwenye hizo digital platform pesa ipo)

Ikumbukwe upande wa Streams za spotify msanii anaeongoza ukanda wa Afirka mashariki ni Sofiya nzau kutoka kenya.huyo hapo



Kgezo cha pili
2. SHOW ZA NJE YA NCHI
Upande wa Show hasa za nje ya nchi Diamond u charge 70,000 mpka 100,000 dollar sawa na Tsh 190,547,210 mpka Tsh 272,210,300. Angalia hapo chini


Kwa upande wa Rema u charge 150,000 dollar mpka 299,000. Sawa na Tsh 408,315,450 mpka Tsh 813,908,797
Angalia hapo chini


Rema amekuwa na show nyingi za nje ya nchi mfano marekani, UK n.k Hasa baada ya kutoa Album yake mpya na show alizozipata kwenye kibao vchake cha Calm down baada ya kushirikiana na selena Gomez.ngoma hio ilimpa show nyingi kama kuperfom kwnye BET,grammy na Tuzo za fifa

Kwa upande wa Diamond hana show nyingi za nje ya nchi yaani Marekani, United kingdom n.k show alizozipata ni baada ya kutoa EP yake ya FOA Ikumbukwe diamonf hajatoa tena Album tangu 2018 alipotoa Aboy from tandale. Show anazo zifanya sahivi ni za wasafi festival mikoani ili kuji boost kiuchumi.

( kweli wasanii wetu bila show za mikoani na lounge au club hawana pesa maana hata huko kwenye digital platform hawafanyi vizuri wamekomalia Youtube inayoingiza pesa ndogo zaidi ni vijembe vya Insta. Mfano ulikuwa tu wa Rema hajatumika msanii mkubwa wa Naija kam wizkid, Burnaboya na Davido

UWEKEZAJI WA DIAMOND.
Diamond hupata pesa kupitia ubalozi wa makampuni mfano Airt. Pia kupitia wasafi media.
IKumbukwe Media hutengeneza pesa kupitia matangazo, Youtube post na pesa wanazolipwa kupitia media hiyo kuonyeshwa kpitia king'amuzi.

kwa media inavyoingiza pesa itoshe kusema kua WAsafi media inaingiza pesa ndogo kwani pesa nyingi zinatumika kulipa mishahara ya watangazaji.

Wasafi media imekua ikitumika kama kumtengenezea connection n serkl pia kutangaza kazi za wasanii wa WCB (Ikumbukwe moja ya sababu ya Diamond kuanzisha Media n baada ya media z bongo kuacha kucheza ngoma zake na za wasanii wake kwenye chanel zao)

KWA KUSRMA HAYO ITOSHE KUSEMA PESA WANAZO INGIZA WASANII WA NIGERIA KUPITIA TU MZIKI(ukiachana na ubalozi na uwekezaji mwingine) NI NYINGI ZAIDI UKILINGANISHA NA PESA ZA WASANII WA BONGO WANAZOINGIZA KUPITIA USANII NA UWEKEZAJI WAO PAMOJA NA UBALOZI. Uyo alikua tu REMA JE angetumika Burnaboy, wizkid au Davido.
 

Attachments

  • Screenshot_20241027-172835_Opera Mini.jpg
    161.1 KB · Views: 7
  • Screenshot_20241027-173151_Opera Mini.jpg
    214.3 KB · Views: 8
  • Screenshot_20241027-182138_Spotify.jpg
    173.4 KB · Views: 6
  • Screenshot_20241027-174726_Opera Mini.jpg
    140.7 KB · Views: 6
  • Screenshot_20241027-174726_Opera Mini.jpg
    164.6 KB · Views: 6
  • Screenshot_20241027-174726_Opera Mini.jpg
    164.6 KB · Views: 7
Kweli mziki unalipa lakini mpaka uende kwa Pdidi?
 
Mkuu lengo ni kuonyehsa jinsi hizi digital platform zinavyo lipa pesa. Mimi pia nina Acc huko. Njoo na wewe uwekeze kwnye mziki ni sauti yako tu
Hao Spotify wanapataje pesa mimi ninaye stream kwa Bando la Halotel la chuo?
 
Tupe na takwimu ya Dangote na Mo Dewj kwa maana tushakubaliana kuwashindanisha watanzania na wanaijeria
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…