Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,509
- 3,756
Muigizaji wa filamu na msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Faiza Omary maarufu kama Sister Fey yupo chini ya ulinzi kufuatia tabia yake ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.
Taarifa hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Kijamii wa Instagram
Ameandika kukamatwa Faiza kunatokana na malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wadau wa filamu na baadhi ya Wananchi juu uwekaji wake wa picha na video zisizo na maadili katika mitandao ya kijamii
Atafikishwa Mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika ili sheria ikachukue mkondo wake
Mpaka sasa Msanii Maua Sama, Watangazaji Soudy Brown na Shaffih Dauda, Michael Mlingwa(MxCarter), Katibu Mwenezi wa CHADEMA Tumaini Makene, Mshehereshaji Anthony Luvanda na wengine wawili wanashikiliwa na Polisi
Taarifa hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Kijamii wa Instagram
Ameandika kukamatwa Faiza kunatokana na malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wadau wa filamu na baadhi ya Wananchi juu uwekaji wake wa picha na video zisizo na maadili katika mitandao ya kijamii
Atafikishwa Mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika ili sheria ikachukue mkondo wake
Mpaka sasa Msanii Maua Sama, Watangazaji Soudy Brown na Shaffih Dauda, Michael Mlingwa(MxCarter), Katibu Mwenezi wa CHADEMA Tumaini Makene, Mshehereshaji Anthony Luvanda na wengine wawili wanashikiliwa na Polisi