Lord Diplock MR
JF-Expert Member
- Mar 16, 2015
- 1,393
- 3,237
Waungwana habari!
Nimekuwa nikisikia mara nyingi watu wakisema msanii ni kioo cha jamii. Wamekuwa wakisema hivyo kwa maana kwamba watu humtazama msanii na maisha yake na wao huishi vivyo hivyo. Wanaopigia chapuo hoja hii wanaamini kwamba tabia, maadili na matendo ya msanii ni muhimu kwa jamii na ndiyo kioo chenyewe, wanaamini jamii inajitazama kwenye maisha ya msanii na kujirekebisha.
Mimi binafsi napingana vikali na nadharia hii kwani haina uhalisia katika maisha ya leo ya mtanzania. Msanii siyo kioo cha jamii bali ni mwalimu wa jamii. Mwalimu ni mtu anayetoa elimu kwa jamii katika jambo analolielewa vyema. Msanii wa Tanzania siyo kioo cha jamii kwa sababu maisha anayoishi hayana uhalisia na matendo yake yamejaa drama na ya kuigiza. Jamii ya kitanzania haijifunzi tena kwenye maisha na mienendo ya msanii bali inajifunza zaidi kwenye kazi zake za sanaa (fasihi). Fasihi ndiyo kioo cha jamii, kwa maana kwamba jamii inajifunza kwa kile anachoimba msanii zaidi.
Kwa mfano msanii kama Bahati Bukuku aliyeimba wimbo wa "umewazidi wote", anajaribu kuwaasa wanandoa kuheshimiana, kupendana na kuvumiliana halafu yeye binafsi hana ndoa na ndoa yake ilimshinda anakuwaje kioo cha jamii zaidi ya ile kazi yake?. Katika mfano huu Bahati Bukuku hawezi kuwa kioo cha jamii katika swala la ndoa, lakini wimbo wake " umewazidi wote" ndiyo kioo cha jamii kwani jamii na wana ndoa watajipima kupitia alichokiimba na kujirekebisha. Yeye msanii Bahati Bukuku atabakia kama mwalimu wa jamii kupitia kazi zake ambao ndiyo kioo.
Chukulia mfano mwingine wa msanii kama Diamond Platnumz ambaye amekuwa nguli wa kuimba nyimbo za mapenzi akihimiza wapenzi kuwa waaminifu na kutokusalitiana, kupitia nyimbo zake kama "nataka kulewa", " nitarejea", "utanipenda", " marry you", na nyinginezo anahimiza wapenzi kupendana na kuvumiliana, anapinga usaliti katika mapenzi. Lakini maisha halisi ya kimapenzi ya Diamond Platnumz yamejaa kusalitiana na kukosekana kwa mapenzi ya dhati. Kama tukisema msanii ni kioo je jamii inajifunza nini kwenye maisha haya ya Diamond Platnumz? Kama jamii itajiangalia kwenye kioo hili na kujipima mwisho wa siku itajikuta inapotoka kabisa.
Lakini jamii itajifunza zaidi kwenye nyimbo za Diamond Platnumz na kujipima kupitia yale anayoyaimba kuhusu mahusiano na si kupitia maisha yake binafsi.
Nahitimisha kwa kusema kuwa msanii siyo kioo cha jamii bali ni mwalimu wa jamii anayefundisha kupitia kazi zake za sanaa. Lakini kazi zake za kisanaa ndiyo kioo cha jamii, jamii inatakiwa ijitazame na kujipima kwenye nyimbo na maigizo ya wasanii.
Nakaribisha mjadala.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekuwa nikisikia mara nyingi watu wakisema msanii ni kioo cha jamii. Wamekuwa wakisema hivyo kwa maana kwamba watu humtazama msanii na maisha yake na wao huishi vivyo hivyo. Wanaopigia chapuo hoja hii wanaamini kwamba tabia, maadili na matendo ya msanii ni muhimu kwa jamii na ndiyo kioo chenyewe, wanaamini jamii inajitazama kwenye maisha ya msanii na kujirekebisha.
Mimi binafsi napingana vikali na nadharia hii kwani haina uhalisia katika maisha ya leo ya mtanzania. Msanii siyo kioo cha jamii bali ni mwalimu wa jamii. Mwalimu ni mtu anayetoa elimu kwa jamii katika jambo analolielewa vyema. Msanii wa Tanzania siyo kioo cha jamii kwa sababu maisha anayoishi hayana uhalisia na matendo yake yamejaa drama na ya kuigiza. Jamii ya kitanzania haijifunzi tena kwenye maisha na mienendo ya msanii bali inajifunza zaidi kwenye kazi zake za sanaa (fasihi). Fasihi ndiyo kioo cha jamii, kwa maana kwamba jamii inajifunza kwa kile anachoimba msanii zaidi.
Kwa mfano msanii kama Bahati Bukuku aliyeimba wimbo wa "umewazidi wote", anajaribu kuwaasa wanandoa kuheshimiana, kupendana na kuvumiliana halafu yeye binafsi hana ndoa na ndoa yake ilimshinda anakuwaje kioo cha jamii zaidi ya ile kazi yake?. Katika mfano huu Bahati Bukuku hawezi kuwa kioo cha jamii katika swala la ndoa, lakini wimbo wake " umewazidi wote" ndiyo kioo cha jamii kwani jamii na wana ndoa watajipima kupitia alichokiimba na kujirekebisha. Yeye msanii Bahati Bukuku atabakia kama mwalimu wa jamii kupitia kazi zake ambao ndiyo kioo.
Chukulia mfano mwingine wa msanii kama Diamond Platnumz ambaye amekuwa nguli wa kuimba nyimbo za mapenzi akihimiza wapenzi kuwa waaminifu na kutokusalitiana, kupitia nyimbo zake kama "nataka kulewa", " nitarejea", "utanipenda", " marry you", na nyinginezo anahimiza wapenzi kupendana na kuvumiliana, anapinga usaliti katika mapenzi. Lakini maisha halisi ya kimapenzi ya Diamond Platnumz yamejaa kusalitiana na kukosekana kwa mapenzi ya dhati. Kama tukisema msanii ni kioo je jamii inajifunza nini kwenye maisha haya ya Diamond Platnumz? Kama jamii itajiangalia kwenye kioo hili na kujipima mwisho wa siku itajikuta inapotoka kabisa.
Lakini jamii itajifunza zaidi kwenye nyimbo za Diamond Platnumz na kujipima kupitia yale anayoyaimba kuhusu mahusiano na si kupitia maisha yake binafsi.
Nahitimisha kwa kusema kuwa msanii siyo kioo cha jamii bali ni mwalimu wa jamii anayefundisha kupitia kazi zake za sanaa. Lakini kazi zake za kisanaa ndiyo kioo cha jamii, jamii inatakiwa ijitazame na kujipima kwenye nyimbo na maigizo ya wasanii.
Nakaribisha mjadala.
Sent using Jamii Forums mobile app