Msemaji wa Simba SC Ahmed Ally hiyo Barua ya Kumfuta Kazi Kocha Mkuu Pablo unairusha lini? au Hasira zetu tuzianzie Kwako mjue mmetukera?

Ninachoona kocha ndo awe anapendekeza wachezaji anaowataka. Sio unamfukuza kocha unaanza usajili kocha analetwa mwishoni na wachezaji hawajui. Iwapo italazimu kumfukuza kocha basi kabla ya usajili kocha mpya awe ashakuja. Yeye ndo apendekeze wachezaji anaowataka
 
Kinachowa wakumba simba ni syndrome tu

Huwezi kutamba milele.

Lazima utaharibu tu somewhere.

Kuna kipindi mo aliwatosaga halafu kule yanga alikuwa manji mlikuwa manashinda derby tu ila ubingwa alikuwa anabeba yanga kila misimu mfululizo .

Yanga alipoanza migogoro na manji kuondoka ndio mkaanza tamba nyie kipindi ambacho alirudi simba

So both yanga na simba wakiwa stable kiuchumi tegemea ushindani wa timu zote.

Ila mmoja wao akiwa ndivyo sivyo mzani huegemea upande mmoja.

Nyie kuvurunda msimu huu msianze tafuta mchawi jipange msimu ujao hela mnazo acheni makelele
 
Kocha hamna kitu humo, mkabidhini matola amalizie mechi zilizobakia - huyo mspaniola aende zake - hatumtaki.

Uchebe pira tuliliona
Gomes pira tuliliona

Sasa huyu jamaa hamna kitu, timu imemshinda - wachezaji hawajitumi - aende.
Kila siku namkumbuka uchebe, walimuacha kwa majungu bila kosa lolote, kufungwa mechi moja na draw moja ndio wakamuona hafai!

Yule Mo kwa lile kosa alilofanya, na kumfukuza yule kocha wa viungo Zrane, wacha Karma iwatafune tu.
 
Nguvu Mmoja, hakika umeyatendea haki maoni yako.

Watu tumeumia na matokeo , Simba siyo ya kufungwa na Yanga kizembe vile.

Tunahitaji wachezaji wa kuipambania timu hata ikiwa nyuma wajitoe wapambane kuhakikisha tunapata ushindi , lakini siyo hii Simba niliyoiona juzi.

Tumetoka Kwenye michuano mikubwa , alafu tunakuja fungwa kizembe namna ile.

Hapana lazima club ifanye jambo, mambo kama haya yasijirudie.
 
[QUOTE="GENTAMYCINE, post: 42775933, member: 156632"



Sijawahi kupandwa na Hasira kama Juzi.[/QUOTE
Mkuu pole kwa kupandwa na hasira hiyo juzi
 
Tangu utoe ushauri humu simba wafanye ulozi kwenye mechi zake na kuacha kufanya sayansi
Nimekuona zwazwa kabisa
Hao aliowataja wote walikataa timu isifanye tena yale matambiko ya kuwasha moto uwanjani.

Ndio maana hata Mzee Kaduguda alisema mapema kuwa Simba itafungwa kwa kuwa walikatazwa wasiloge. Ndio sababu ya haya mapovu toka kwa wana kamati ya ulozi.
 
Kocha hamna kitu humo, mkabidhini matola amalizie mechi zilizobakia - huyo mspaniola aende zake - hatumtaki.

Uchebe pira tuliliona
Gomes pira tuliliona

Sasa huyu jamaa hamna kitu, timu imemshinda - wachezaji hawajitumi - aende.
Kiukweli simba ndo imeipa mafanikio Simba, inawezekana watu husahau tu.
Wachezaji wa simba, kuanzia mayele,huyo mganda,na wengine wa AS VITA, waliletwa na Simba,lakini wakatoroshwa na yanga kutoka katika hotel.
Hata hivyo wapo baadhi waliambiwa kwanza waweze kucheza mechi za kirafiki ili kuangalia kama wanafaa kusajiliwa simba,na hata dau lao lilikuwa dogo tofauti na simba.
Matokeo yake,hao wachezaji wote walichukuliwa na yanga.
Hivyo hata dawati la ufundi simba limeanza kuanza kutangaza au kutaja baadhi ya wachezaji inao wataka katika dirisha linalokuja na kutaja inaowaacha, matokeo yake ni:
1: kwanza inasababisha morali kushuka kwa wachezaji ambao hawatasajiliwa na hata hawajui hatma yao ni ipi matokeo yake kucheza chini ya kiwango.
2: inatangaza baadhi ya wachezaji inaotaka au kuongea nao kuhusu kuwasajili na inachukua muda mrefu kumaliza dili, Sasa je yanga akiingiza gia na kuweka hela tu hapo, maana unawaonyesha wachezaji wazuri na wao wanaweza kuwawinda,huoni kuwa itakuwa sawa na kipindi cha msimu wa mwaka Jana?
Mwisho, muddy aache mambo ya uswahili,aanze kuongea na kuingia kwenye mikataba na wachezaji ambao inawahitaji ili kuwazuia,mfano ni kipa manula,inonga ambae anawindwa Sana na timu zingine, na wengine kabla ya kuendelea na wachezaji wengine wa nje. Pia inatakiwa kutozungumza inaowaacha ili morali ya timu iwe juu
 
Simba ipi imefungwa kizembe hii ya Mzamiru?
 
Bwana hamis tuachie timu yetu
 
Ukowataja wote waondoke tu hawana faida
 
lawama zote ziende kwenye kamati ya USAJILI wametufanya kitu mbaya mbaya saana.
Kamati ya usajili imetimiza majukumu yake, wachezaji waliokuwa nyota Mugalu, Boko, Kagere bado wapo. Leo wote hao ambao walikuwa vinara wa mabao wamekuwa mizigo, Mugalu ndio hoi zaidi, sasa lawama za usajili zinatoka wapi? Lazima mkubali kocha hakuna pale, kocha ambaye hana first 11 hadi sasa maana yake ameshindwa kitumia raslimali zake vizuri au hajui kazi yake.

Vv
 
Nadhani Mwamedi Bado anaimani na Kocha wa zamani wa mabingwa wa Ulaya
 
Hili ndilo neno la bwana.......tumshukuru Mungu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…