Msemaji wa Simba SC Ahmed Ally hiyo Barua ya Kumfuta Kazi Kocha Mkuu Pablo unairusha lini? au Hasira zetu tuzianzie Kwako mjue mmetukera?

Msemaji wa Simba SC Ahmed Ally hiyo Barua ya Kumfuta Kazi Kocha Mkuu Pablo unairusha lini? au Hasira zetu tuzianzie Kwako mjue mmetukera?

Ninachoona kocha ndo awe anapendekeza wachezaji anaowataka. Sio unamfukuza kocha unaanza usajili kocha analetwa mwishoni na wachezaji hawajui. Iwapo italazimu kumfukuza kocha basi kabla ya usajili kocha mpya awe ashakuja. Yeye ndo apendekeze wachezaji anaowataka
 
Kinachowa wakumba simba ni syndrome tu

Huwezi kutamba milele.

Lazima utaharibu tu somewhere.

Kuna kipindi mo aliwatosaga halafu kule yanga alikuwa manji mlikuwa manashinda derby tu ila ubingwa alikuwa anabeba yanga kila misimu mfululizo .

Yanga alipoanza migogoro na manji kuondoka ndio mkaanza tamba nyie kipindi ambacho alirudi simba

So both yanga na simba wakiwa stable kiuchumi tegemea ushindani wa timu zote.

Ila mmoja wao akiwa ndivyo sivyo mzani huegemea upande mmoja.

Nyie kuvurunda msimu huu msianze tafuta mchawi jipange msimu ujao hela mnazo acheni makelele
 
Kocha hamna kitu humo, mkabidhini matola amalizie mechi zilizobakia - huyo mspaniola aende zake - hatumtaki.

Uchebe pira tuliliona
Gomes pira tuliliona

Sasa huyu jamaa hamna kitu, timu imemshinda - wachezaji hawajitumi - aende.
Kila siku namkumbuka uchebe, walimuacha kwa majungu bila kosa lolote, kufungwa mechi moja na draw moja ndio wakamuona hafai!

Yule Mo kwa lile kosa alilofanya, na kumfukuza yule kocha wa viungo Zrane, wacha Karma iwatafune tu.
 
View attachment 2244555
9fb2589e55c2489185e38acb740acaf4.jpg
 
Sidhani kuwa Simba ilihujumiwa jumamosi. Hizi lawama za Simba kushindwa zinapaswa kwanza ziwaendee wale wote waliofanya usajili kabla ligi haijaanza na wakati wa dirisha dogo. Kwa kweli hawakuitendea haki Simba kwa aina ya sajili walizofanya. Pili kushindwa kwa Simba jumamosi kuwe changamoto na funzo kubwa kwa bodi nzima ya Simba ili timu ifanye usajili wa maana kwa ajili ya msimu ujao.

Tuwe wakweli jamani Simba ilizidiwa kila idara uwanjani na bahati mbaya kwa Yanga lakini nzuri kwa Simba ni kufungwa tu lile goli moja. Iwapo safu ya ushambuliaji ya Yanga (Makambo na Mayele) ingekuwa makini nilikuwa naziona wazi kabisa goli 5 kwa 1. Sehemu ya kiungo ya Simba ambayo ndio mhimili kwa Simba kwa takribani miaka mitano sasa ilipotezwa kabisa na Yanga. Mbinu za benchi la ufundi la Yanga zilikuwa bora kabisa kuzidi zile za benchi la ufundi la Simba kwa kuanza na viungo wengi bila mawinga asili. Kitendo cha benchi la ufundi kushindwa kuudhibiti mfumo waliokuwa wanautumia Yanga kwa dakika zote 90 za mchezo ndio sababu kubwa ya Simba kushindwa mechi ile. Na kibaya zaidi kwa Simba ni aina ya maumbo ta wachezaji wao. Kwa wastani wachezaji wa Simba waliokuwa uwanjani jumamsosi walikuwa na maumbo madogo kulinganisha na wa Yanga kiasi ikitokea "one vs one" wachezaji wa Simba walikuwa wanapata sana shida.

Na hizi stori za Simba kuwa kama Al Haly, Orlando, n.k. ni vyema viongozi na mwekezaji wa Simba wakaachana nazo kabisa iwapo usajili wa mchezaji kama Adebayo tu unawatoa jasho. Sasa utashindana vipi na Al haly, Orlando, n.k. wakati Berekane tu wanakupelekesha kwenye usajili. Kama mwekezaji ameshindwa kuiboresha timu kwa kushindwa kusajili wachezaji wa maana basi ni vyema akaiuza timu au hisa zake kwa wawekezaji wengine wenye uwezo zaidi yake. Na hili halitakuwa la kwanza kwake kwani miaka michache tu iliyopita alishaiuza Sigara ikawa Singida United.
Nguvu Mmoja, hakika umeyatendea haki maoni yako.

Watu tumeumia na matokeo , Simba siyo ya kufungwa na Yanga kizembe vile.

Tunahitaji wachezaji wa kuipambania timu hata ikiwa nyuma wajitoe wapambane kuhakikisha tunapata ushindi , lakini siyo hii Simba niliyoiona juzi.

Tumetoka Kwenye michuano mikubwa , alafu tunakuja fungwa kizembe namna ile.

Hapana lazima club ifanye jambo, mambo kama haya yasijirudie.
 
[QUOTE="GENTAMYCINE, post: 42775933, member: 156632"



Sijawahi kupandwa na Hasira kama Juzi.[/QUOTE
Mkuu pole kwa kupandwa na hasira hiyo juzi
 
Tangu utoe ushauri humu simba wafanye ulozi kwenye mechi zake na kuacha kufanya sayansi
Nimekuona zwazwa kabisa
Hao aliowataja wote walikataa timu isifanye tena yale matambiko ya kuwasha moto uwanjani.

Ndio maana hata Mzee Kaduguda alisema mapema kuwa Simba itafungwa kwa kuwa walikatazwa wasiloge. Ndio sababu ya haya mapovu toka kwa wana kamati ya ulozi.
 
Kocha hamna kitu humo, mkabidhini matola amalizie mechi zilizobakia - huyo mspaniola aende zake - hatumtaki.

Uchebe pira tuliliona
Gomes pira tuliliona

Sasa huyu jamaa hamna kitu, timu imemshinda - wachezaji hawajitumi - aende.
Kiukweli simba ndo imeipa mafanikio Simba, inawezekana watu husahau tu.
Wachezaji wa simba, kuanzia mayele,huyo mganda,na wengine wa AS VITA, waliletwa na Simba,lakini wakatoroshwa na yanga kutoka katika hotel.
Hata hivyo wapo baadhi waliambiwa kwanza waweze kucheza mechi za kirafiki ili kuangalia kama wanafaa kusajiliwa simba,na hata dau lao lilikuwa dogo tofauti na simba.
Matokeo yake,hao wachezaji wote walichukuliwa na yanga.
Hivyo hata dawati la ufundi simba limeanza kuanza kutangaza au kutaja baadhi ya wachezaji inao wataka katika dirisha linalokuja na kutaja inaowaacha, matokeo yake ni:
1: kwanza inasababisha morali kushuka kwa wachezaji ambao hawatasajiliwa na hata hawajui hatma yao ni ipi matokeo yake kucheza chini ya kiwango.
2: inatangaza baadhi ya wachezaji inaotaka au kuongea nao kuhusu kuwasajili na inachukua muda mrefu kumaliza dili, Sasa je yanga akiingiza gia na kuweka hela tu hapo, maana unawaonyesha wachezaji wazuri na wao wanaweza kuwawinda,huoni kuwa itakuwa sawa na kipindi cha msimu wa mwaka Jana?
Mwisho, muddy aache mambo ya uswahili,aanze kuongea na kuingia kwenye mikataba na wachezaji ambao inawahitaji ili kuwazuia,mfano ni kipa manula,inonga ambae anawindwa Sana na timu zingine, na wengine kabla ya kuendelea na wachezaji wengine wa nje. Pia inatakiwa kutozungumza inaowaacha ili morali ya timu iwe juu
 
Nguvu Mmoja, hakika umeyatendea haki maoni yako.

Watu tumeumia na matokeo , Simba siyo ya kufungwa na Yanga kizembe vile.

Tunahitaji wachezaji wa kuipambania timu hata ikiwa nyuma wajitoe wapambane kuhakikisha tunapata ushindi , lakini siyo hii Simba niliyoiona juzi.

Tumetoka Kwenye michuano mikubwa , alafu tunakuja fungwa kizembe namna ile.

Hapana lazima club ifanye jambo, mambo kama haya yasijirudie.
Simba ipi imefungwa kizembe hii ya Mzamiru?
 
Hasira zangu zinaenda kwa Watu hawa Wafuatao....

1. Mwenyekiti Mangungu
2. CEO Barbara
3. Kocha Msaidizi Matola
4. Meneja Rweymamu
5. Mratibu Abbas
6. Kocha Mkuu Pablo

Kuna Watu Wanne tajwa hapa ni 'Virusi Waandamizi' ndani ya Klabu ya Simba na ndiyo kwa 99% wametumika 'Kuihujumu' Simba SC kwa kutoa 'Siri' za Klabu na Mipango yote kwa Wapinzani wetu huku wakilipwa Mamilioni na Kampuni ya Tapeli iliyo na Ofisi zake Jengo refu kiasi Posta Mpya.

Msemaji wa Simba SC Ahmed Ally tunawapeni hadi Jumatano muwe mmeshatangaza rasmi Kuachana na Kocha Pablo na kumpa Timu Kocha wa muda (mwenye Uchungu na Simba SC) ili azimalizie hizi Mechi za Ligi Kuu ya NBC zilizobakia.

Sijawahi kupandwa na Hasira kama Juzi.
Bwana hamis tuachie timu yetu
 
Yaani kwa wachezaji wa Kigeni wa kubalia pale ni 5 tu tena kwa makubaliano maalum

1 Sakho - aache papara, muda wa kutoa pasi hatoi anakimbia kimbia hovyo tu - tutabaki naye ila akubali kujifunza, no gurantee ya number - ataipigania
2. Bwaya, huyu abakie kaonyesha uhai
3. Peter Banda - huyu abakie kwa umri wake ana room ya kujifunza zaidi - hakuna gurantee ya number aipiganie.
4. Chama tumvumilie kwa msimu mmoja atuonyeshe kitu - akishindwa atasugua benchi.
5. Inonga - hili jembe letu.

WENGINE WOTE MA PRO - FUKUZA - FUKUZA

Tafuta Mido mbili za hatari za kusaidiana na Mkude.
Tafuta Beki 2 za kati - zile za kazi kazi za kusaidiana na Inonga
Tafuta Striker moja matata sana ambaye pasi moja kaukamiza - ili atasaidiana na FAZA boko.

Mchezaji wa kuangalia - Mwanuke - ana kipaji anajituma, Simba wekeni jicho hapo.

Kwisha habari.

Simba oyeeeeeeee
Ukowataja wote waondoke tu hawana faida
 
lawama zote ziende kwenye kamati ya USAJILI wametufanya kitu mbaya mbaya saana.
Kamati ya usajili imetimiza majukumu yake, wachezaji waliokuwa nyota Mugalu, Boko, Kagere bado wapo. Leo wote hao ambao walikuwa vinara wa mabao wamekuwa mizigo, Mugalu ndio hoi zaidi, sasa lawama za usajili zinatoka wapi? Lazima mkubali kocha hakuna pale, kocha ambaye hana first 11 hadi sasa maana yake ameshindwa kitumia raslimali zake vizuri au hajui kazi yake.

Vv
 
Hili ndilo neno la bwana.......tumshukuru Mungu.
 
Back
Top Bottom