Mgagaa na Upwa
JF-Expert Member
- Sep 30, 2013
- 13,481
- 28,116
Wapewa dozi watakua wamenuna hili jambo la kuomba msamaha japo watajifanya wanamdhihaki haji lakini mioyoni wameumiaBinafsi kama shabiki wa Yanga SC ninashikuru kuwa ameomba msamaha ili aendelee kuwapo kwa lengo la KUKINUKISHA ZAIDI.
Na hili litawapa shida sana Yanga, kwasababu hawawezi kujitenga na Kauli zake..!Wanaomchukia kama nani?
Halafu msamaha wenyewe umeombwa kwa shinikizo, inaonekana uongozi wa Yanga ndio umemshauri aje aombe radhi
So busara yake hapo iko wapi?
Huyu mtu bado anasimamia msimamo wake, huo msamaha ni takwa la club kulinda maslahi yake lakini mimi na wewe wote tunajua Manara asingeweza kuthubutu kwa willing yake kuomba radhi
Hakuna cha msamaha wala nini.Msemaji wa Yanga Haji Manara ameufya kwa kuamua kujishusha baada ya kumuomba radhi Rais wa TFF Wallace Karia kuhusu jambo ambalo lilitokea Jijini Arusha wakati wa fainali la Kombe la Shirikisho la Azam Sports Federation Cup ASFC, baina ya Yanga SC na Coastal Union.
"Jana mimi na rafiki yangu Heris Said alinisindikiza kwenda kumuona Rais wa Shirikisho la Soka Nchini Tanzania Wallace Karia, na tuliongea kwa furaha sana na kuzungumza mambo ya msingi zaidi nyumbani kwake.
"Kiukweli jambo la Arusha tukio zima halikua na matusi, hilo nataka iwe Very Clear, ambalo watu wengi wananishtumu nalo na waling'ang'ania hapo hapo.
"Ndo maana nilisema pale Airport, kuwa atakayepata tukio lile likiwa na matusi nitajiuzulu kwa kuwa nitakuwa kinyume na hata maadili ya kitanzania na wala si football peke yake.
"Naomba msamaha kwa namna yoyote ile nilikosea kujibizana na Rais Wallace Karia naomba radhi, haimaanishi mini nisichukuliwe hatua.
Kama itaonekana nastahili kuchukuliwa hatua nipo tayari kupokea adhabu hiyo, lakini lazima niombe msamaha bila kujali kamati itaamua nini.
Kingine sina matatizo na Karia, ni Mzee wangu na namheshimu, na nimekuwa mstari wa mbele mara kadhaa kutetea hoja zake.
Naomba radhi, mimi ni mwanadamu na binadamu yoyote yule hukosea, ila kwa kuwa Rais amenizidi kwa vitu vingi sana, sina budi kuheshimu na kuomba radhi kubwa kwake, amenizidi umri na mambo mengi ambayo itakuwa si uungwana kuliacha jambo hili."
Amezungumza Haji Manara kwenye mkutano wake na waandishi wa vyombo vya habari, kufuatia kadhia yake na Rais wa TFF Wallace Karia.
Wangelitaka hilo Safari yenu ya kutwaa ubingwa ingewashinda mapema.
Mkuu, umesahau sifa za watu wa kule? Kwa sasa, baada ya wale WAWILI, wamemuongeza na HAJI!Labda kama unatafsiri yako kuhusu mtu mwenye akili sana.
Umesahau mlivyojiliza miaka 4 eti mnaonewa na Simba inabebwa.Ingewezekana. Nakubali.
Wangeanzisha kanuni mpya ambayo itaruhusu timu yeyote kuwa na zaidi ya wachezaji 13 ndani ya uwanja.
Hapo wangetuweza.
Ila tofauti na hapo, hakuna chochote wangeweza kufanikiwa
Siku akikutukania mama yako ndio utajua ana akili au amekosa maleziHaji Manara ana akili sana yaani.
Mpira bongo umehamia kwenye mipasho sahviHana lolote huu msukule
Msamaha hauondoi sheria na kanuni kutofanya kazi..! Vipo kwa ajili ya kufanya kaziViongozi wa Yanga SC wana akili sana.
Wameshaufahamu uongozi wa Msomali Karie unachotaka. Si kingine bali ninkuidhoofisha Yanga SC wakidhani wanaikomoa.
Wakamshauri akaombe msamaha wakijua wazi msamaha utaondoa adhani ya kufungiwa na kubakisha adhabu ya faini.
Ambayo hata iyo faini inaweza kusamehewa pia.
Si alisema anataka kugombanishwa na viongozi wa TFF, ?Msemaji wa Yanga Haji Manara ameufya kwa kuamua kujishusha baada ya kumuomba radhi Rais wa TFF Wallace Karia kuhusu jambo ambalo lilitokea Jijini Arusha wakati wa fainali la Kombe la Shirikisho la Azam Sports Federation Cup ASFC, baina ya Yanga SC na Coastal Union.
"Jana mimi na rafiki yangu Heris Said alinisindikiza kwenda kumuona Rais wa Shirikisho la Soka Nchini Tanzania Wallace Karia, na tuliongea kwa furaha sana na kuzungumza mambo ya msingi zaidi nyumbani kwake.
"Kiukweli jambo la Arusha tukio zima halikua na matusi, hilo nataka iwe Very Clear, ambalo watu wengi wananishtumu nalo na waling'ang'ania hapo hapo.
"Ndo maana nilisema pale Airport, kuwa atakayepata tukio lile likiwa na matusi nitajiuzulu kwa kuwa nitakuwa kinyume na hata maadili ya kitanzania na wala si football peke yake.
"Kwa namna yoyote ile naomba msamaha, nilikosea kujibizana na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Tanzania Wallace Karia, naomba radhi, na haimaanishi mimi nisichukuliwe hatua.
Kama itaonekana nastahili kuchukuliwa hatua nipo tayari kupokea adhabu hiyo, lakini lazima niombe msamaha bila kujali kamati itaamua nini.
Kingine sina matatizo na Karia, ni Mzee wangu na namheshimu, na nimekuwa mstari wa mbele mara kadhaa kutetea hoja zake.
Naomba radhi, mimi ni mwanadamu na binadamu yoyote yule hukosea, ila kwa kuwa Rais amenizidi kwa vitu vingi sana, sina budi kuheshimu na kuomba radhi kubwa kwake, amenizidi umri na mambo mengi ambayo itakuwa si uungwana kuliacha jambo hili."
Amezungumza Haji Manara kwenye mkutano wake na waandishi wa vyombo vya habari, kufuatia kadhia yake na Rais wa TFF Wallace Karia.
Umesahau mlivyojiliza miaka 4 eti mnaonewa na Simba inabebwa.
Na hili litawapa shida sana Yanga, kwasababu hawawezi kujitenga na Kauli zake..!
Msamaha hauondoi sheria na kanuni kutofanya kazi..! Vipo kwa ajili ya kufanya kazi