Mshauri Mkuu wa Rais wa Marekani Donald Trump amtaka Trump amsamehe Derek Chauvin muuaji wa George Floyd

Mshauri Mkuu wa Rais wa Marekani Donald Trump amtaka Trump amsamehe Derek Chauvin muuaji wa George Floyd

Mag3

Platinum Member
Joined
May 31, 2008
Posts
13,413
Reaction score
23,592
Elon Musk, mshauri mwandamizi wa Rais wa Marekani, Rais Trump, amtaka bosi wake huyo kumpa msamaha muuaji, Derek Chauvin, mweupe, aliyekuwa na cheo cha afisa wa polisi nchini humo.

Elon Reeve Musk ni tajiri mkubwa anayemiliki kampuni za Tesla, Inc., SpaceX, na Twitter, na pia ofisa mwandamizi katika serikali ya Marekani kama mshauri mwandamizi wa Rais Donald Trump.

Mnamo Mei 25, 2020, Chauvin, mweupe, alibana shingo la George Floyd kwa goti kwa karibu dakika tisa akiwa amefungwa pingu na kulazwa uso chini mtaani, akilia "Siwezi kupumua"

chauvin.png

Picha za muuaji huyo zilisambaa duniani zikimuonesha mtu mweusi aitwaye George Floyd akikata roho huku muuaji akionekana kutojali hata pale alipopigwa picha na mashuhuda wa tukio hilo!

Mapema mwaka 2021, Chauvin alishtakiwa kwa mauaji ya kiwango cha tatu, na mauaji ya kiwango cha pili ya Floyd mbele ya jopo la majaji mahakamani huko Minnessota, USA.

Mnamo Aprili 20, alihukumiwa kwa mashtaka yote na Juni 25, alihukumiwa kifungo cha miaka 22+1⁄2 gerezani pamoja na uwezekano wa kuachiliwa baada ya miaka 15

Kweli hujafa hujaumbika, huu ushirika wa watu hawa wawili Marekani unaweza kuwekewa LUKU na Wamarekani wenyewe tu na si kelele za dunia hata zikiungana kwa pamoja.
 
Mshauri kiboko sanasss...twende kunazidi kupendezaa na kupambazuka
 
Mshauri kiboko sanasss...twende kunazidi kupendezaa na kupambazuka
Watu kama Elon Musk hawaijui Marekani. Kuna mtu unaweza kuisi Marekani miaka yako yote lakini usiijue Marekani. Wamarekani hawakupata uhuru wao mezani, waliupigania na ole wake Trump pamoja na kutaka kuwa kama rafiki yake Putin atafeli vibaya sana

Leo tu keshapigwa stop na US Supreme Court pamoja na mahakama hiyo kujaa watu wake aliowateua. Kaambiwa hana mamlaka yoyote ya kuzuia yaliyopitishwa na bunge kuu la nchi hiyo, CONGRESS! Siku wamarekani watakaposema imetosha si Musk wala Trump watazuia.

Marekani imejengwa katika misingi imara. Asikudanganye mtu, ukaburu hautafanikiwa Marekani!
 
Ni kawaida; hata Babu Seya na vijana wake walipata msamaha kutoka kifungo cha maisha gerezani kwa kosa la ubakaji.
 
Ni kawaida; hata Babu Seya na vijana wake walipata msamaha kutoka kifungo cha maisha gerezani kwa kosa la ubakaji.
Nakusamehe hilo kwani labda hujui namna weusi wanavyosota magerezani nchini Marekani kwa makosa madogo madogo au ya kubambikiwa wanvyojisikia huyu mjukuu wa makaburu wa Afrika Kusini anapomuombea msamaha muuaji kama huyo.
 
Back
Top Bottom