Mshtakiwa aliyeiomba Mahakama akutanishwe na mkewe, aruhusiwa

Mshtakiwa aliyeiomba Mahakama akutanishwe na mkewe, aruhusiwa

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemruhusu mshtakiwa Said Matwiko anayekabiliwa na kesi ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya Heroine zenye uzito wa kilo 34.89 kuonana na mke wake Sarah Joseph ili wajadiliane kuhusu malezi ya watoto wao.

Sara na mume wake pamoja na watu wengine watatu akiwemo aliyekuwa kocha wa makipa wa timu ya Simba Sport Club, Muharami Sultan (40) wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kusafirisha dawa za kulevya kinyume cha sheria.

Kuruhusiwa kwa wanandoa hao kuonana mahakamani hapo, kunatoka na ombi lililowasilishwa na Matwiko mahakamani hapo.

Machi 16, 2023, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Mary Mrio wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kutajwa.

Tofauti na siku nyingi ambapo washtakiwa husikilizwa kesi yao kwa njia ya video, leo Machi 30, 2023 , washtakiwa wote wameletwa Mahakama kwa ajili ya kusikiliza kesi yao.

Hata hivyo upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Pia soma:
 
Hata hivyo upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.
Hizi ndio sarakasi za prosecutors wetu, utasemaje upelelezi haujakamilika huku una ushahidi wa kukamata kilo hizo za heroine? Ushahidi gani zaidi unaohitajika? You are keeping people in remand prison when they are supposed to be serving their sentences!!!
 
So mume na mke wote walikuwa wanapush? Kama ni kweli je hawakufikiria malezi ya watoto wa wengine walokuwa wanaharibika?
Kama wanasingiziwa Mungu awasimamie wakalee watoto wao.
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemruhusu mshtakiwa Said Matwiko anayekabiliwa na kesi ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya Heroine zenye uzito wa kilo 34.89 kuonana na mke wake Sarah Joseph ili wajadiliane kuhusu malezi ya watoto wao.

Sara na mume wake pamoja na watu wengine watatu akiwemo aliyekuwa kocha wa makipa wa timu ya Simba Sport Club, Muharami Sultan (40) wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kusafirisha dawa za kulevya kinyume cha sheria.

Kuruhusiwa kwa wanandoa hao kuonana mahakamani hapo, kunatoka na ombi lililowasilishwa na Matwiko mahakamani hapo.

Machi 16, 2023, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Mary Mrio wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kutajwa.

Tofauti na siku nyingi ambapo washtakiwa husikilizwa kesi yao kwa njia ya video, leo Machi 30, 2023 , washtakiwa wote wameletwa Mahakama kwa ajili ya kusikiliza kesi yao.

Hata hivyo upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Wamekutana mbele ya hakimu au wamepewa chumba chao wawili tuu wakakutaniana hapo kuongea
 
Back
Top Bottom