Msiba kwa wafugaji wa kuku wa mayai -- Mayai yamefurika bei chini toka Mombasa!

Nakuunga mkono 62%! Ubunifu unatushinda waTZ. Wangeweza ku- proccess mayai yao kuwa ya unga na kisha kuyauza kwenye vipaketi kwa bei nafuu!
 

Kwanza poleni sana wafugaji wote kwa kukabiliana na hali hii.
Lakini si busara kutegemea hao wanasiasa ukidhani watakusadia/watawasaidia. Kwanza ukiwaendea watakuambia ndio initiative zinazochukuliwa ili kupunguza mfumuko wa bei. Ha ha haa

Sasa kwa kuwa mmeamua kuwa wapambanaji/wajasiriamali ni vyema mkavunja bongo zenu ili muweze kukabiliana na ushindani. Huu ndio wakati wakupunguza gharama zenu za uzalishaji ili end products yenu ziwe nafuu kulingaisha na hao wenzenu wa mombasa. Hebu jiulize wao wanafanya nini ambacho nyie mnashindwa/hamfanyi?

Tusifanye biashara kwa mazoea jamani. Mnaweza mkajiunga wafugaji wachache mkaanza kuzalisha chakula chenu wenyewe, kwani gharama kubwa za kufuga zipo kwenye chakula.
 
FUSO: Mimi nadhani ni muhimu kwa wafugaji wetu kwenda Kenya na kujifunza ni njia gani wanatumia hadi gharama zao za uzalishaji zinakuwa chini kiasi hicho. kama serikali yao ina wasaidia kwa kiasi fulani basi tuomba na sisi serikali yetu itusaidie. Lakini tunapokuwa kwenye soko huria tusikimbilie kuzuia tu vitu kutoka nje visije ila tujivuze kwanza je kwanini wenzetu wameweza kuzalisha kwa gharama nafuu.

Kwa sisi walaji hii ni neema.
 
ndiyo maana tunajadili, je serikali yetu inajitoa kabisa katika suala la kutusaidia kutafuta mbinu mbadala za kibiashara? huoni kuwaacha wazalishaji wadogo wadogo wafanye kila kitu kivyao ni sawa na mtoto yatima hajui wapi aanzie na wapi asonge?

Kaka ni rahisi sana kusema sentensi hiyo lakini kama ungekuwa ni wewe ndiyo umekivaa hiki kiatu cha wazalishaji wadogo wadogo ungeelewa mimi nina maana gani.
 
Mbona msisiba mingi tu Tanzania, nenda mafinga ukaone wakenya wanavyokaa mbao kama vile ndio wazawa. kila sekta hapa ni uozo mpaka JK atoke labda.

 
mi sioni hatari as long as mayai yao yanafaa kwa afya ya mlaji
 
Mbona msisiba mingi tu Tanzania, nenda mafinga ukaone wakenya wanavyokaa mbao kama vile ndio wazawa. kila sekta hapa ni uozo mpaka JK atoke labda.

Usinikumbushe mkuu,
Sasa hivi ukitaka ubao mzuri kwa bei nzuri inabidi uumie sana/ujikamue kana kwamba mbao nazo zinaagizwa toka nje. Ukifika Mafinga vijijini shule hazina madawati ya kutosha. Sijui ni laana?
 
bomu sasa hivi lipo kwenye mchakato wa kulipuka. Mimi ngoja niendelee na kilimo changu
 
Kwahyo mkuu ulitaka hao wakenya wauze 6500 wazidi kutuhumiza?? Ni kweli mayai yapo kibao mbagala trey moja sh4500
 

Waziri wa Elimu akisoma hii hatakupenda
 
Vita vya Panzi furaha ya Kunguru. As long yasiwe na madhara.
 

Wewe bana ndo umesema neno la maana! Wao wakifanya hivi sisi tufanye vile! Twendeni "digitali" wachaneni na mayai ya kuku wa kisasa, sijui wa kizungu, sijui wa kinini! Tukazane na ufugaji wa kuku wa kienyeji hasa hawa chotara na kutokana na mafunzo ya humu JF naamini ndiyo jibu sahihi na mbadala kwa haya mayai ya Mombasa ya leo. Kesho yatakuja ya China, twafaaaa!
 
Kenya ni Leading country kwa ufugaji wa Kuku East and Centra Africa, wale wako Mbali sana na kushindana nao inahitai nguvu za ziada,
 
Hatuna ujanja kwani tayari nchi yetu ni mwanachama wa WTO na tayari tumesain SPS and TBT agreement. Hapo maana yake ukiwa mwanachama hautakiwi kuzuia chochote kiingiacho nchini mwako kama hautathibitisha kuwa kina madhara kwa binadamu.

Cha kuwashauri Wajasiriamali wetu:

Wayapime hayo mayai na kuku. Wakiona kuna madhara basi waanze mchakato wa kuzuia
 
Update:

Hali ya soko imerudi kama kawaida yake, yale mayai yaliyokuwa yanauzwa kwa mafungu (4000 - 4500) kwa tray yemeisha. Tray kwa sasa ni 6500 hadi 7,000 kwa bei ya Jumla.

Serikali msiruhusu tena wahuni wahuni kuingiza mizigo ya vyakula kwa njia za panya!! lindeni wazalishaji wazawa wa ndani - maana mmeshatuambia kuwekeza kwenye GESI HATUWEZI - sasa huku kwenye mifugo nako mnataka kutukimbiza, swali je tuende wapi?

Hili si la kubeza, ni suala muhimu kabisa - LAZIMA KUWAJALI WAKULIMA NA WAFUGAJI WA NDANI.
 
Tatizo sio serikali, watu waliopewa kushughulikia hayo mambo ndo wana matatizo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…