Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
- Thread starter
-
- #101
Jackline,Economist hili tunalolijua,au zamani kulikuwa na lingine tofauti- na hasa hiyo nakala uliyoandika ilikuwa inahusu nini??
Umeandika katika Economist,na hukumbuki umeandika nini?? Ina maana Economist alikuwa na hadhi ya sasa? yaani hiyo nakala hata uku I frame??Jackline,
Ni hili The Economist ambalo ni mashuhuri.
Sikumbuki niliandika kuhusu nini lakini ilikuwa inahusu
siasa za Tanzania.
Jackline1,Umeandika katika Economist,na hukumbuki umeandika nini?? Ina maana Economist alikuwa na hadhi ya sasa? yaani hiyo nakala hata uku I frame??
Mohamed Said , keshaweka habari za Kyaruzi nenda kasome utaona ni paragraph mbili tu ndio zenye Kyaruzi, kwingine kote ni Sykes tu, mi sio mgeni na nyie Dada Faiza
Weka wewe historia ya Kyaruzi au mwengine yeyote umpendae na usiwataje wazee wetu. Kinakushinda nini?
Mbona historia ya kivukoni iliweza kuandika historia ya TANU iliyoanzia na kuishia kwa Nyerere?
Badala ya kuja na porojo, Allah akaonesha njia akampa uwezo aliyetokea mitaa hiyo hiyo alipopokelewa Nyerere, akafunguliwa makabrasha na wale wale waliompokea Nyerere, akapewa na uwezo wa kuyakusanya na mengine mengi huku na kule, akatiririka kwenye kitabu, matokeo?
Historia adhyim na adim ambayo imefichuwa na kuweka wazi mengi sana ambayo waliyoiandika historia ya kivukoni hawakuyajuwa na wala wasingeliyajuwa, simply kwa kuwa source yao ni Nyerere na historia hiyo inaanzia na kuishia kwa Nyerere.
Wewe sasa, ni jukumu lako kutuletea mbadala au kusema "hapa haikuwa hivyo, ilikuwa hivi na hivi na hivi, na sisi wasomaji tutaamua wenyewe ipi tuchukue ipi tuache.
Hivi usongo wa nini?
Ndio maana ya Historia hiyo, huwezi kuweka kila kitu ndani ya Historia
Ndiyo maana ile ya kivukoni ikaanzia kwa Nyerere ikaishia kwa Nyerere, si ndiyo? Na Mohaed Said akaliona hilo akanyanyua kalamu akaandika historia ya wazee wake.
Haya na wewe tuwekee ya wazee wako basi, au ya Kyaruzi tu pekee.
Mohamed Said kaandika historia ya harakati zilipoanzia na kaziainisha vilivyo, nawe unaweza kuelezea kwa namna yako. Kuna aliyekupinga?
Lakini kuja kusema ooh anaandika ya Kyaruzi anatia ya Abdul Waheed Sykes, hivi hukuiona post namba moja ile attachment aliiandika Mohamed Said? Au si kuhusu Kahama ile? Na umeona mwanzo mwisho anatajwa Kahama tu?
Huna jipya unaleta ubishani wa kijinga. Bisha halafu weka unachokikosoa au kukibishia mbadala wake ni huu, wewe unabisha hewa tu.
Ni kama ile Historia ya Zanzibar ya Ghassan inayopigiwa debe kila siku na Mohamed Said , Historia inayoanzia kwa Sultan wa Zanzibar as if Zanzibar kulikuwa hakuna watu kabla ya hao Wavamizi wa Kigunya,
Sitakujibu tena kwenye mjadala huu, labda mwingine
Kituko,Ni kama ile Historia ya Zanzibar ya Ghassan inayopigiwa debe kila siku na Mohamed Said , Historia inayoanzia kwa Sultan wa Zanzibar as if Zanzibar kulikuwa hakuna watu kabla ya hao Wavamizi wa Kigunya,
Sitakujibu tena kwenye mjadala huu, labda mwingine
Aah jamani kwa nini mnamsahau Zuberi Bakampeja na Abdullah Bwojo na Issa Juma na Mariam Kokugonzolwa na Muhidini Keto na Salum Iddi na Hawa Lutama na Athumani Rutatatenekwa na Amani Abedi Karume na Adam Nasibu na Mohamed Rutaihwa na Saidi Iborogero na Juma Ali na Iddi Juma na Abdallah Magunia.Chachu...
Siwezi kushangaa ikiwa hamumtambui Ali Migeyo.
Hakutambuliwa Abdul Sykes mwenye kadi ya TANU No. 3
Hakutambuliwa Ally Sykes mwenye kadi ya TANU No. 2 na
kadi ya TANU No. 1 ya Mwalimu Nyerere ni Ally Sykes
ndiye aliyeiandika.
Hajatambuliwa baba yao Mzee Kleist aliyejenga hiyo ofisi
ilipozaliwa TANU 1954.
Hajatambuliwa Iddi Faizi Mafungo aliyesimamia safari ya
Nyerere UNO 1955.
Kipi mimi leo kitanishangaza ikiwa hamumtambui Suedi
Kagasheki?
Ama kuhusu Uislam naam ulitumika sana katika kupambana
na ukoloni kuanzia Vita ya Maji Maji dhidi ya Wajerumani hadi
kudai uhuru kutoka kwa Waingereza.
Ilikuwa Salum Mpunga na Ali Ibrahim Mnjale ndiyo vijana
waliomleta Mwalimu Nyerere Jimbo wa Kusini kuja kupambana
na Kanisa lililokuwa linawatisha wananchi kujiunga na TANU kudai
uhuru.
Wala katika kuandika historia hii hakuna udini ni historia tu tupu
iliyokuwapo hatuwezi kuifuta hata kama kuna baadhi yetu kwa
sababu zetu binafsi hatuipendi.
Kipi kitanishangaza ikiwa wewe leo hii humjui Sheikh Yusuf Badi,
Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Suleiman Takadir waliokuwa
mstari wa mbele kupigania uhuru wa Tanganyika?
Ikiwa wewe una historia nyingine isiyokuwa hii tuwekee hapa Majlis
tuisome.
Mhariri wa Raia Mwema katika toleo lake la 15 - 21, Machi 2007 katika tahariri yake kwa kumuadhimisha marehemu George Kahama aliyezikwa jana ameeleza masikitiko yake kwa Tanzania kutokuwa na historia ya mashujaa wake. Mhariri kamtaja pamoja na wazalendo wengine Abdul Sykes kama mmoja wa wazalendo ambae historia ya mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika bado haujathaminiwa.
Binafsi nimefarajika kuwa kumbe si mimi peke yangu ninayoona upungufu huu katika taifa letu.
Mara ya kwanza mwaka wa 1988 gazeti la Africa Events lililokuwa likichapwa London lilipochapa makala yangu, ''In Praise of Ancestors,'' na nikamtaja marehemu Abdul Sykes kwa sifa ya kuaisi chama cha TANU 1954, toleo zima lilikusanywa na kutolewa katika mzunguko.
Mambo hayakuishia hapo toleo la gazeti hilo lililofuatia ilichapwa barua kutoka CCM Makao Makuu Dodoma iliyoandikwa na kada mashuhuri wa wakati huo na aliyekuwa na cheo kikubwa katika Sekretariati ya Kuhamasisha Umma iliyokuwa na vitisho na dharau dhidi yangu. Kisa na kosa langu kumtaja Abdul Sykes na wazalendo wengine na kusema kuwa historia ya uhuru wa Tanganyika haiwezi kutenganishwa na mchango wa Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Alipokufa Dossa Aziz katika maziko yake Mlandizi hakuna katika viongozi wa CCM aliyekuwapo pale mazikoni aliyejua Dossa alikuwa nani kwa Mwalimu Nyerere wala kwa TANU yenyewe na kwa bahati mbaya sana Nyerere hakuhudhuria maziko yale. Labda angekuwapo angemueleza Dossa alikuwa nani kwake na kwa TANU.
Alipokufa Paul Bomani mambo hayakuwa tofauti na yale ya maziko ya Dossa Aziz. Hakuna katika viongozi wa CCM aliyejua mchango wa Bomani.
Hawa wazalendo watatu niliowataja hapa kwa uchache wote wanaunganishwa na sifa moja adimu sana. Hawa walitajirika katika ukoloni na TANU ilipoasisiwa walikuwakuwa tayari wana na fedha zao. Hawa hawakutajirikia katika TANU. Wazalendo hawa walitoa fedha nyingi kwa TANU katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Kwa kuhitimisha ningependa kusema kuwa hakika nimefarajika sana kuwa kumbe kuna wenzagu na wao wameona upungufu wa jambo hili.
Kwa kuitika mwito wa Mhariri wa Raia Mwema itapendeza kama katika jengo jipya la CCM pale Patrice Lumumba Avenue CCM ikaanza kutafuta historia ya mashujaa wetu na kuwaenzi angalau kwa kuweka picha zao na maelezo mafupi.
Kizazi hiki cha leo kingependa kuona picha ya Sheikh Suleiman Takadir na maelezo yake ya mchango wake katika kudai uhuru wa nchi yetu, picha ya Saadan Abdul Kandoro, Hamza Mwapachu, Bi. Titi Mohamed na Tatu biti Mzee, Iddi Faiz Mafungo, Mshume Kiyate kwa kuwataja wachache na huko mikoani na wilayani haya yafanyike.
Hapo Makao Makuu ya CCM Dodoma ziwekwe picha za Omar Suleiman, Haruna Taratibu, Edward Mwangosi, Tanga zikwekwe picha za Abdallah Rashid Sembe, Bi. Mwanamwema, Hamisi Heri. Lindi picha za Salum Mpunga, Yusuf Chembera, Sheikh Yusuf Badi. Kilimanjaro waweke picha za Eikaeli Mbowe, Yusuf Olotu, Juma Ngoma, Mama Biti Maalim, Halima Selengia.
Bukoba waweke picha za Ali Migeyo, Suedi Kagasheiki, Abdallah Rutabanzibwa nk. nk.
Tusitishike na majina haya ya Kiislam kwani hii ndiyo historia yenyewe hatutoweza kuibadili.