Msichana wa watu anataka kutoa mimba.

Ni kosa moja kubwa sana kwani hiyo hiyo 20 ndo ataichanga changa akatoe nayo

lakini me nilimpa ka pesa ya kujikimu baada ya kuniambia hana pesa,ukizngatia ni mtu tunae toka nae sehemu moja,nkaona co mzuka kumuacha hvi hvi!
 
Better Be safe than sorry
Halafu kuna watu wanapinga ile thread ..
Ni vema kila mtu akipata elimu ya kuzuia ..

Anyway yameshatokea , si ya kuzuia tena.
Kwanza kabisa umefanya vizuri kumsikiliza ila usingemchana
kwani hapo alipo kachanganyikiwa.

Mtu akiwa kwenye situation hiyo kweli anahitaji msaada
Kwa sababu wengi hujaribu , kutoa wenyewe, na wengi wengineo
wanafikiri hata kujiua. ndo maana nikasema kumchana haisaiidi kitu.

Alikimbilia kwako sababu anakuamini wewe.
Tatizo hapo chooni usikute hakuna caunceler wala hata nesi ..
We ungemsaidia kutafuta mtu wa kuongea naye "Professional"
 

Nah, actually ilikua vizuri kumweleza jinsi anavyolichukulia hilo swala, huko kuchanganyikiwa kukimtoka labda atafikiria mara mbili mbili kama atoe au la. Sema hata mimi naunga mkono swala la kumpatia mtu wa kuongea nae amwaleze ni kwa namna gani anaweza akaishia kupata kovu la maisha badala ya kupata unafuu anaotegemea.
 

Hivi mtu akiwa amechanganyikiwa huwa ana think straight kweli?
au ndo kwanza anaishia kwenye conclusion. Mtu akichanganyikiwa
anarukie kile ambacho anaona ndo solution kwa muda huo.

Ni sawa kumweleza wazi alichofikiria , lakini hapo aliposema
"Nimemchana Live" yaonekana ni kama vile alikuwa anamropokea..
Na ukimropokea mtu kuna chance kubwa sana
hakusikilizi na hatilii maanani unacho mwambia..
 

We bana, nimesema "KUCHANGANYIKIWA KUKIMTOKA" hata kama itakua ni baada ya kutenda hicho anachotaka.Kesho na kesho kutwa atajifunza kuwa mwangalifu, kama anataka sex awe responsible.
 
utoaji mimba wangehalalisha tu.
 
We bana, nimesema "KUCHANGANYIKIWA KUKIMTOKA" hata kama itakua ni baada ya kutenda hicho anachotaka.Kesho na kesho kutwa atajifunza kuwa mwangalifu, kama anataka sex awe responsible.

Kumtokee mara ngapi??
yaelekea tangu aongee na huyo jamaaa
aliemtia tayari alisha changanyikiwa. na jamaa
alivyo muwekea ngumu ya kwamba kwamba hataki
kumuona tena ndo kuchanganyikiwa kukazidi..
Kuchanganyikiwa kumesha mtokea .. sana sana anazidi
kuchanganyikiwa zaidi na atakachofanya sasa ni atafanya
sababu hafikirii..

Ya baadaye yatakuja baadaye lakini yeye anahitaji
msaada sasa. anahitaji mtu wa kuongea nae tu basi.
maana sasa atakuwa anaogopa..
 

dah! Aisee kaka ulifanya uamuzi wa busara sana. Sijui ungejibu nini mbele ya mwenyezi mungu kwa kuua kiumbe chake tema kisichojuwa na hatia. Yani mimi kama ningemuona huyo dada ningemtandika viboko 6 vya nguvu.
 
...ni utapeli tu wa hao mabinti. Hakuna cha mimba wala nini. Maisha ni magumu tu. Wajinga waliwao, mtaliwa siku zote!! Vijana muamke usingizini.
 
Unashangaa chuo?
Watu wanazitoa huku wako makazini
hadi unashangaa wanataka nini
pole zao wakaka wanaoa wakidhani mwali
kumbe wameshazitoa kama nini
afu unafika kwenye ndoa unashindwa pata watoto bure
kama ulitolea uchochoroni

Yuko chuo atoe mimba ya nini tena?
 

cna maana kwamba nimemropokea mkuu,nimemwambia kiustaarabu tu.
 
Duh!mimba atatoa na ukimwi je?
Mtu anapokuamini na kukwambi lake la moyon usiwe unapenda kumchana km ulivyosema,
Kwa kauli hiyo ni km ulimsuta au kutumia lugha ya kejeli wakati unamweleza msimamo wako,
Nakusifu kwa kumwonyesha msimamo wako ila naungana na A.D na Lizzy ungemwelekeza kwa watu proffessional ambao angeongea nao na kupata msaada kulingana na hali yake na maamuzi anayotaka kuyafanya.
 
"mimba" siyo "mtu" - mimi ninaamini hivyo! Kwa sababu yoyote ile inayoweza kunusuru maisha ya mjamzito ni heri mimba kutolewa!
 
Huyu dada ananisikitisha sana, wewe mtoa maada naomba please kaa nae chini ummwambie yeye sio wa kwanza kupata mimba akiwa chuo, kwahiyo hata hao wazaz wake watakuwa shocked lakn baadae wataelewa tu maana am sure huyo babake anajua mwanae lazma ana mshkaji somewhere.ASITHUBUTU KUTOA MIMBA!!adhabu za Mungu ni kali kuliko anavofikiri.Wadada wengi sana wameathirika kwa kukosa watoto kwenye ndoa ikiwa ni madhara ya kutoa mimba before marriage tena sio kwamba walitoa mimba nyingi ni hio hio moja.Asione aibu maana najua inawezekana hapo chuo anaogopa vidole lakn ajue bora aibu ya sasa kuliko fedheha ya wakwe,mme na jamii kwenye ndoa atakapokosa mtoto.KOSA VYOOTE DUNIAN ILA SIO MTOTO!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…