Msigwa: Nilipokuwa CHADEMA nilikuwa Mjinga

Msigwa: Nilipokuwa CHADEMA nilikuwa Mjinga

Ulikuwa mjinga!!!! na bado uliendelea kuwa mchungaji means mchungaji mjinga alikuwa na kanisa lake lenye waumini. Waumini wajinga
 
Kuna jamaa nae alipotoka ukatoliki akakandia kuwa kanisa ni freemanson, alipokuwepo alikuwa mjinga, alipotoka akagundua hilo.
 
Mwanachama mpya CCM akitokea Upinzani, Mchungaji Peter Msigwa, amesema wakati alipokuwa CHADEMA hakuwa na ufahamu kwamba Mchakato wa Katiba Mpya ulikuwa unakwamishwa na baadhi ya Viongozi wa CHADEMA lakini amelijua hilo baada ya kujiunga na CCM.

Alipoulziwa na Mtangazaji wa Kipindi cha Medani za Siasa cha StarTv, Edwin Odemba, kwamba alikuwa Mjinga akiwa CHADEMA, Mchungaji Msigwa amejibu "Ndio, kuna kipindi nilikuwa sina ufahamu nimeongezewa ufahamu nilikuwa napigania vitu ambavyo havipo".

Kuhusu nani aliyepoteza ushawishi baada ya yeye kujiondoa CHADEMA, Msigwa amesema "Nadhani CHADEMA wamenipoteza mimi, ukiangalia timu iliyobaki pale ni Lissu na Heche na Lissu naye anasema hoja za Msigwa zijibiwe, angekuwa haoni kama nina hoja asingesema nijibiwe".


Pia soma > Kuelekea 2025 - Freeman Mbowe amtaka Mchungaji Peter Msigwa kumuomba radhi kwenye Magazeti Frontpage, au Kulipa fidia ya Bilioni 5 kwa kumkashifu na kumchafua jina
Kaenda kuungana na wauaji
Wamekiri wenyewe ni wauaji
 
Back
Top Bottom