Msijisumbue kwa lolote linalomhusu kiongozi

Msijisumbue kwa lolote linalomhusu kiongozi

ONJO

JF-Expert Member
Joined
Jun 1, 2022
Posts
216
Reaction score
265
Nasema msijisumbue kwa lolote juu ya jambo afanyalo kiongozi.

Kweli yangu ni hii.

Mtaji mkubwa wa kiongozi/mtu ni akili.Akili huamua kutenda na kutenda huleta matokeo.

*Akili huzaa fikira/mawazo
*akili huamua kipi kinafaa na kisichofaa,na badae hutengeneza imani kwenye jambo flani.Mfano nikiibinafsisha bandari italeta faida kuliko kukaa nayo bila kuleta matunda yoyote.

Angalieni!Anavyofikiri mtu ndivyo anavyokuwa,kupendeza kwa mtu ni matokeo ya kufikiri,alivyo mlevi ni matokeo ya kufikiri,alivyo mwenye hasira ni matokeo ya kufikiri.Alivyo mcha mungu ni matokeo ya kufikiri.

Kumbe point ni kwamba mambo yote wafanyayo watu ni matokeo ya kufikiri.

Akili ya mtu huleta msimamo usioyumba kwa lolote sawa sawa na jinsi alivyoifundisha akili yake.

Kila mtu amejengwa na kweli yake ndiyo maana viongozi wa Tanzania toka nyerere mpaka samia.Kila mmoja alifanya kivyake na mama samia anafanya kivyake.

akili ya mtu hubadilika kwa ukweli kwamba elimu haina mwisho na kwamba akili ni ya kujifunza siku zote.

sasa angalieni tujifunze.
tukubali kuwa kila mtu anaongozwa na mtazamo wake mfano.ukiona binti mzuri ukampenda na ukataka umuoe na yeye akakataa basi tujue kuwa mtazamo wa binti kwa mwanaume ni wa kitofauti.
tujue pia kuwa mke na mme walipokuwa nje ya ndoa kilichowakutanisha ni mitazamo yao kuwa sawa.

ukweli ni kwamba huwezi kumfanya mtu awe kama wewe ulivyo au kama wewe unavyotaka(free will).Mfano mh. Rais samia tangu aingie madarakani angefata kila wazo la mtu vipi tungekuwa na serikali ya namna gani?

Pointi ya msingi ni kwamba kile anachokifanya mtu ni sahihi kabisa 100%.
Tangu samia awe Raisi mpaka wakati huu vyote alivyofanya,anavyofanya na atakavyofanya ni sahihi kabisa 100%.

Kikubwa tumuungeni raisi wetu mkono tukijua kabisa na yeye anamtazamo wake wa kiuongozi, tuendelee kumpa pia mitazamo yetu,akiona inafaa ataifanyia kazi.

Kwa kuandika thread hii sitegemei kumuoana raia wa jamii forumu akitukana kiongozi yeyote au mtu yeyote.

See you na ONJO.
 
Kwa maelezo yako basi tusingekuwa na KATIBA. Viongozi wa kiafrika wana kawaida kulewa madaraka na kuona wao ndio wenye akili kuliko kila mtu, kuona wao wanafikiri na kuona mbali kuliko kila mtu. Na viongozi wabaya zaidi Afrika ni wale wanao tawala Nchi ambazo hazija wahi kukumbwa na misukosuko ya kijeshi au wananchi kuasi.
 
Kwa maelezo yako basi tusingekuwa na KATIBA. Viongozi wa kiafrika wana kawaida kulewa madaraka na kuona wao ndio wenye akili kuliko kila mtu, kuona wao wanafikiri na kuona mbali kuliko kila mtu. Na viongozi wabaya zaidi Afrika ni wale wanao tawala Nchi ambazo hazija wahi kukumbwa na misukosuko ya kijeshi au wananchi kuasi.
Katiba nayo ni matokeo ya akili za watu,kwa mantiki hiyo nayo iko sawa,fundisho kubwa ni kukubaliana na kila kiongozi kwa mitazamo yao.Na huwezi jua siku moja nchi akaanza upya kutokana na ukweli kwamba kiongozi aliyeingia ana mtazamo wake.Cha kufanya ni kutakatifuza kila kiongozi kuwa anafaa tusije mkufuru mungu.
 
Back
Top Bottom