Msikilize Jerry Muro akimdhalilisha Mwandishi wa kike

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2013
Posts
10,931
Reaction score
24,816
Katika mahojiano hayo ambayo nmeyapata kwenye audio anasikika jerry muro akimuuliza mwandishi huyo wa kike kuwa mapumziko ya kocha wa yanga yanamhusu nini?akasisitiza yule ni mume wa mtu baba mwnye watoto wanne je mwandishi anataka akapumzike naye?

Kiuhalisia hakupaswa kumdhalilisha mwandishi wa kike kiasi cha kumuuliza huyo mwajiri wake anamlipa kwa nini wakat "anaonekana hopeless" kwa tafsiri ya reasoning. Dada wa watu ikabidi aombe mapumziko. Nikawaza kama ameolewa na mumewe kasikia yale maswal nadhan itakuwa shida.

Huyo ndo jerry muro bwatubwatu.
 

Attachments

Kwani ukiwa yanga au simba usipokuwa na akili za kibangibangi utadumu?
 
Wakati mwingine maswali ya waandishi yanaboa ila alishalitolea ufafanuzi.
 
Tulimuonea huruma alivyobambikiwa ile kesi ila tumegundua huyu ni mwehu kabisa. Ni mropokaji wa hali ya juu,hata wanayanga tunamchukia
 
Mbona mikasi huwa kuna maswali ya kutatanisha klk hayo!huyo jerry anajarib kumtetea kocha labda shemej yke hataki awe na mchepuko
 
Mambo ya mpira wa miguu kwa Tanzania,
yanaendana na lugha na matendo ya hivyo.''UTANI WA JADI''
 
Serious?
Huyu jamaa ni tatizo sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…