Msimhukumu Rais Samia pasipokuwa na uhakika

Ni wapi katiba/sheria ya Tanzania inasema lazima unayetaka wewe aweke sign ndio makubaliano yawe halali? Vinginevyo ayatambuliki Tanzania.
Ni wapi katika katiba au Sheria yetu inasema masuala yetu ya kisheria yaende kutatuliwa south Africa?
Unajua maana ya IGA wewe au unakurupuka kutetea usilolijua
 
Sasa unajuaje raisi aja sign hiyo sheria baada ya bunge kupitisha.
Wewe kilaza tofautisha kazi ya bunge ya kutunga Sheria na kazi ya bunge ya kuridhia ( ratify) mkataba.
Sheria ikipitishwa na bunge kabla ya kuanza kazi lazima Rais aisaini.
Kwenye mikataba serikali ikiingia mkataba ya kimataifq , mkataba hiyo kabla ya kuanza kutumika Tanzania lazima bunge iipitishe ( ratify) kabla ya kuanza kutumika.
Bunge likisha ratify mkataba basi mkataba huo unaanza kufanya kazi hayahitaji saini ya Rais .
Wewe jamaa utakuwa ulikwenda shule kusomea ujinga mpuudhi sana
 
Inaitwa mihemko !! 😂😂
Hivi unadhani waarab wao ni wajinga huo mnaouita mkataba sijui makubaliano wafanye wao ndio wenye kufaidika zaidi halafu sisi ndio wakutekeleza wajibu?
Yani IGA ionekane haina nguvu wala maana kama mnavyotaka watu waamini? Ingekuwa haina maana kwanini watake wajibu wa TZ kwa DP world ubainishwe mle ndani?
 
Ni wapi katika katiba au Sheria yetu inasema masuala yetu ya kisheria yaende kutatuliwa south Africa?
Unajua maana ya IGA wewe au unakurupuka kutetea usilolijua
Mnaishi kwenye dunia yenu na kujitungia sheria zenu na kudhani that’s how the world works.

Hakuna mwekezaji wa kimataifa mjinga atakae ingia mkataba bila ya stabilisation clause popote atakapowekeza ata akienda USA.

Ndio maana ukienda ICISD unakutana na kesi luluki za arbitration kwenye kila nchi na hakuna nchi itakayoweka sheria kama hizo zenu because that’s not how things work since the 1960’s.

Kwa watu wanaoelewa maswala ya mikataba ya kimataifa hilo ni jambo la kawaida kabisa, utoto ni kudhani unaweza fanya mambo tofauti na dunia.
 
Watu wanapotaka ufanye ratification ya mikataba ya kimataifa maana yake ni kwamba kukubali hayo mambo ni sheria kwenye nchi yako.

Na kama hayo mambo yanahusu biashara ukishafanya ratification ya BIT au IGA or anyother moja kwa moja yaliyomo kwenye hayo makubaliano ni implied terms by law za nchi husika kwa mikataba ya uwekezaji itakayofuata baadae.

Ndio msingi wa kufanya ratification, ungekuwa na abc za contract law ungeelewa zaidi the reason behind kwenye kulinda uwekezaji.

Kama nilivyosema mara kadhaa kwenye mada hii na nyingine za sakata la bandari; shida kubwa kwenye jamii ni uelewa mdogo wa contract law including wanasheria mnao wasifia. Huo ndio ukweli wenyewe.
 
Inawezekana kweli kwamba wale wote waliohusika na huo mkataba kwa upande wa Serikali yetu hawajui chochote kuhusu Hiyo IGA na mambo mengine kuhusu huo mkataba. ??!! Nitakuwa mtu wa mwisho kuamini hivyo. !!
 
Kumbe pilipili imekolea? na Unyumbu taratibu umeenza kuondoka kwa baadhi ya wakeleketwa wa CCM
 
Wewe jamaa nakukumbusha hoja ilikuwa kwamba ulieleza kwamba bunge likiridhia ( ratify) mkataba inabidi upelekwe Kwa Rais ausaini ili uwe Sheria.
Ndio nikakuelewesha kwamba bunge Liki ratify mkataba haupelekwi tena Kwa Rais kusainiwa na Rais eti ili uwe Sheria ya nchi.
Acha kuchanganya Sheria za Nchi na Mikataba inayoingia Nchi . Hivyo ni vitu tofauti yanajifanya mjuaji kwembe hujui kitu
 
Embu soma vizuri mada wapi nimesema hayo?

Nilichosema mimi bunge likishafanya ratification inakuwa sheria ya nchi and thus implied terms on future contracts.

Aliyesema aiwezi kuwa sheria ya nchi bila ya sign ya raisi ni Fundi Mchundo usiniwekee maneno.
 
Wewe utakuwa hujielewi kwenye hili hoja ilikuwa kwanini hiyo Document IGA Kati ya Tz Govt na DP world signatories upande wa Tz ni Rais na Waziri pamoja na power of attorney ya Rais kumruhusu waziri asaini lakini upande wa DP world hakuna signature ya kiongozi wa Dubai wala power of attorney yake ya kumruhusu mtu mwingine asaini Kwa niaba hivyo.Wewe ndio ukaja na hoja ni wapi kwenye katiba yetu au Sheria yetu ipi inataka hivyo.
Ndipo nikakuhoji kwa kukutega mbona ukitokea mgogoro kwenye hiyo IGA utaenda kutatuliwa South Africa.
Ni hivi nakuelewesha kwamba IGA ni makubaliano baina ya serikali na ni lazima yasainiwe na viongozi wa serikali .
Hiyo document ya IGA Kati ya TZ na DP world hakuna sehemu yeyote ambayo imesainiwa na Kiongozi wa Serikali ya Dubai wala hakuna power of attorney yake ya kuridhia mtu asaini Kwa niaba yake.
Acha kuchanganya madesa wewe kilaza
 

Kwanza inabidi utoe kwenye akili yako wrong assumptions ulizonazo.

Kwa kuanzia nimekueleza wewe hujui sheria za Dubai who is entitled to sign what documents, lakini umekadhana lazima Sheikh Makhtoom awepo.

Pili nimekwambia it doesn’t matter whose signatures are there, mkataba wenyewe unakwambia for it to be enforceable it needs to be ratified by those with legal powers to do so.

Unapofanya ratification ya treaty yoyote maana yake unakubali hilo jambo ni sheria nchini kwako (ndio maana yake).

Kama hilo jambo ni sheria kwako na linazungumzia maswala ya mikataba elewa yaliyomo humo ni implied terms kwenye mikataba ya baadae. That is to say sio IGA tu bali BIT zote are applicable the same way.

Kingine nimekueleza hakuna mkataba au makubaliano ya kimataifa nchi moja itangia na nyingine utakosa stabilisation clause ya neutral ground kwenye kutatua migogoro. Tafuta BIT yeyote Tanzania iliyoingia utakutana na kitu kilichofanana na article 20. Kama unadhani huko duniani kwengine ni tofauti tafuta BIT au IGA za nchi nyingine yeyote duniani utakutana na kitu kama article 20 hivyo ndio mambo yanavyofanyika.

Baada ya hapo siwezi kukuelezea jambo hilo hilo mtu ambae utaki kubadili wrong premises zako. Tunaenda in circles ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu kwa upande wangu.
 
Inawezekana kweli kwamba wale wote waliohusika na huo mkataba kwa upande wa Serikali yetu hawajui chochote kuhusu Hiyo IGA na mambo mengine kuhusu huo mkataba. ??!! Nitakuwa mtu wa mwisho kuamini hivyo. !!
Kwani ni mikataba mingapi nchi hii imeingiwa na serikali halafu inakuwa ya kinyonyaji, sasa kwanini ushangae hili?
Loliondo, madini, gas ya mtwara, EPA na mengine. Au ile hakuingiwa na serikali na timu ambayo serikali inawaita wataalamu? Kwani ni jambo jipya mkuu?
 
 
Watu wengi wanao uelewa mzuri tu kuhusu suala zima la DPW tatizo wanaamua kwa makusudi kabisa kupotosha kila kitu kinachofanyika.

Kwanini wanafanya hivyo? Aidha wamepewa pesa na wakubwa wa dunia hii kwa nia ya kuikomoa Tanzania isifaidike na SGR iliyogharimu pesa nyingi. Au wanapinga tu bila ya kuwa na picha pana vichwani mwao.

Hivi sasa Zambia, Angola na DRC wanaangalia uwezekano wa kuitumia bandari ya Lobito ya Angola kupitisha mizigo yao yaani waachane na hii ya Dar, aliye nyuma ya haya yote ni USA na world bank baada ya kuona Tanzania amemuamini DPW.

Ni ushindani wa hao super powers unaoendelea. Marekani anataka kumuharibia huyo mwarabu kwenye biashara yake aliyoikamata huku Congo. Humu ndani wamo vibaraka wengi sana wa USA wanaofanya kazi kwa kujua na baadhi yao wanafuata tu mkumbo.
 
Duh 🙄!
 
anashinikizwaje Rais mkuu we ni mgeni wa mamlaka aliyokuwa nayo Rais aliepo madarakani ?
 
Ka
Kamwambie aliyekudanganya anakuvua nguo stend
 
Ka

Kamwambie aliyekudanganya anakuvua nguo stend
Nenda kasome article 18 ya Vienna Convention on the law of treaties.

Signatories wa treaties awafanyi huo mkataba kuwa sheria ya nchi husika bali ni kuonyesha willingness ya kuingia kwenye hayo makubaliano baada ya sign hiyo sio legal binding document.

Kuwa sheria ni kupitia process ya ratification tu ndio unafanya hayo makubaliano kuwa enforceable.

Sasa nani anaweza sign treaties kila nchi inaamua kutokana na sheria zao.

Shida yenu mnaongopewa sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…