Msimhukumu Rais Samia pasipokuwa na uhakika

Msimhukumu Rais Samia pasipokuwa na uhakika

Wewe umewahi kusimamia kesi za migogoro ya kibiashara? Umewahi kuishauri serikali inapotaka kuingia katika international treaties? Una ujuzi na utaalam zaidi ya Warioba katika masuala ya international treaties? Hapa tunazungumza bilateral agreement kati ya nchi mbili wewe unakazania commercial agreements kati ya business entities!
Mimi kwa arguments zako ambazo ziko all over the place naamini kabisa haujui lolote kuhusu contracts. Una regurgitate mambo uliyocram bila kuyaelewa.

Amandla...
Autakuja kuelewa milele, kwa sababu umeshajiwekea barrier.
 
Article 97.1 (p.37)of the Constitution of Tanzania states that :
Subject to the provisions in this Constitution, the National Assembly shall exercise its legislative power through the process of debating and passing Bills which eventually ( baadae) shall have to be assented by the President, and a Bill shall NOT become law unless it is passed by the National assembly and assented by the President in accordance with the provisions of this Article.

Haya, learned person, wapi katika Katiba yetu panaposema kuwa Bill ikipitishwa tu na Bunge inakuwa sheria? Badala ya kwenda kwenye Katiba kama learned person, were unaenda kwenye kamusi!

Naona unanipotezea wakati.

Amandla....
Sasa unajuaje raisi aja sign hiyo sheria baada ya bunge kupitisha.
 
Bado unaonyesha kuwa haujui unachokisema. Report ya mater Thesis ndio nini? Ulikuwa ni examiner wakati mtu huyo unayemwita kilaza ana defend Thesis yake au uli defend Master's thesis ya kwako? Unataka kutuambia kuwa ulipitia mikataba ya 'oil and gas' ili ujifunze reasoning katika foundation level? Umewahi kweli wewe kukaa katika academia?

Unaleta vitabu vya foundation level kuonyesha umahiri wako wakati hao unaowaponda wameandika vitabu na articles kibao katika peer-reviewed journals! Wewe umeandika ngapi katika peer-reviewed journals? Najua hata maana ya peer-reviewed hauijui. Kwa kweli unasikitisha.

Amandla....
Chukua ushauri wako, mimi sielewi huna sababu ya kuendelea na mimi nisikupotezee muda wako.
 
Sasa unajuaje raisi aja sign hiyo sheria baada ya bunge kupitisha.
Ndio maana nasema arguments zako ziko all over the place. Umekuwa ukikazania kuwa Bunge likipitisha Bill, Bill hiyo inakuwa sheria. Sasa unataka ku hint kuwa Rais aliisaini baada ya kupitishwa na Bunge! Argument ya kitoto kabisa .

Kwa kifupi, ile IGA iliishakuwa signed na mtu aliyepewa POA na Rais kwa hiyo imekuwa tayari kwa kutekelezwa baada tu ya kuridhiwa na Bunge. Na hii ni kwa sababu tuu ule ni Mkataba (ambao unaongozwa na sheria) na sio sheria. Sheria inaanza kwenye Bill, na serikali haikuisubmit kama Bill katika National Assembly.

Amandla...
 
Ndio maana nasema arguments zako ziko all over the place. Umekuwa ukikazania kuwa Bunge likipitisha Bill, Bill hiyo inakuwa sheria. Sasa unataka ku hint kuwa Rais aliisaini baada ya kupitishwa na Bunge! Argument ya kitoto kabisa .

Kwa kifupi, ile IGA iliishakuwa signed na mtu aliyepewa POA na Rais kwa hiyo imekuwa tayari kwa kutekelezwa baada tu ya kuridhiwa na Bunge. Na hii ni kwa sababu tuu ule ni Mkataba (ambao unaongozwa na sheria) na sio sheria. Sheria inaanza kwenye Bill, na serikali haikuisubmit kama Bill katika National Assembly.

Amandla...
Shida yako ni kusoma vitu kwenye katiba au hiyo IGA halafu uwezi kujiongeza.

Swali kwako how do international treaties zote nchi ilizoingia, become laws in Tanzania?

Ata huyo Lissu kama umemsikiliza anatuambia IGA sasa hivi ni sheria ya nchi, wewe hutaki kuelewa.
 
Ndugu zangu mengi yameibuka tangu kusainiwa kwa mkataba wa DP World. Hii nchi haiongozwi na kiongozi mmoja. Kuna idadi kubwa sana ya viongozi kuanzia wastaafu na waliopo madarakani.

Uamuzi wa kuwakabidhi DP World hakuufanya mwenyewe, aidha alishinikizwa ama lah. Tunaweza kumnyooshea kidole kumbe wapo waliomsababishia hilo tatizo.

Nashauri badala ya kumtuhumu tumtafute na kushauriana naye pengine tutaweza kumsaidia kuondokana na kipindi hiki kigumu.
Huyu Samia anahusika.moja kwa.moja. Unaona sasa anapeleka miswada bungeni kurekebisha sheria zinazopingana na wizi na uuzwaji wa bandari. Amedhamiria watanganyika tukatae kuuzwa
 
Ndugu zangu mengi yameibuka tangu kusainiwa kwa mkataba wa DP World. Hii nchi haiongozwi na kiongozi mmoja. Kuna idadi kubwa sana ya viongozi kuanzia wastaafu na waliopo madarakani.

Uamuzi wa kuwakabidhi DP World hakuufanya mwenyewe, aidha alishinikizwa ama lah. Tunaweza kumnyooshea kidole kumbe wapo waliomsababishia hilo tatizo.

Nashauri badala ya kumtuhumu tumtafute na kushauriana naye pengine tutaweza kumsaidia kuondokana na kipindi hiki kigumu.
Waliomzunguka ndiyo tatizo,lakini utampataje ili umshauri?
Nahisi wanaomzunguka wanafanya hivyo kwa manufaa yao
 
Nipeni ikulu , alafu muone , ndio lazima rais shirikisha wazee na watu mbalimbali ili kutenda vizuri katika kazi yake , ila hawezi mpelekesha ,zipo njia nyingi moja si unasimama kama kuhutubia taifa na unamchambua kama karanga ,shida nini hapa ,tatizo upo mfumo wa wa kusema usifanye vile kisa yule mtu flani , ndo upumbavu watuangusha

We kama rais unawezaje na utetezi kwamba unashauriwa na mtu flani nje ya utawala wako akulazimishe fanya kile waona wataka ,uhuni ,
Ndugu yangu raisi anatoka ndani ya chama. Chama ndio boss wake lazima usikilize chama bila hivyo unapokonywa kiti
 
Ndugu zangu mengi yameibuka tangu kusainiwa kwa mkataba wa DP World. Hii nchi haiongozwi na kiongozi mmoja. Kuna idadi kubwa sana ya viongozi kuanzia wastaafu na waliopo madarakani.

Uamuzi wa kuwakabidhi DP World hakuufanya mwenyewe, aidha alishinikizwa ama lah. Tunaweza kumnyooshea kidole kumbe wapo waliomsababishia hilo tatizo.

Nashauri badala ya kumtuhumu tumtafute na kushauriana naye pengine tutaweza kumsaidia kuondokana na kipindi hiki kigumu.
Bado mikataba 30 alisaini pale Dubai
 
Swala la uendeshwaji wa bandari ni devolved matter toka mwaka 97, na Zanzibar wana mamlaka yao kuendesha bandari ambayo inasimamiwa na serikali ya mapinduzi.

Samia ni raisi wa muungano ata kama ni mzanzibari hana mamlaka ya kuwapangia Zanzibar on devolved matters; hayo ni mambo ya Mwinyi kwa sasa na baraza lake la mawaziri na bandari yao washampangisha mtu hivi tunavyoandika.

Hayo yakumpa bandari Mwarabu milele hayapo mahala popote ni upotoshaji tu, vinginevyo taja hiko kifungu.
Mpaka hapa post hii nakuona huna tofauti na kina steve ake
 
Mimi si mdini, wala siwezi kumdharau mtu anayeamini dini iwaye yoyote ile. Natambua binadamu hulazimika kufanya hivyo ili afanye mapatano na mamlaka ya kiroho iliyo kuu kwake.Lakini natambua ukweli mmoja tu, ni vyema kiongozi atangulize sifa na utukufu kwa Mola wetu. Kiongozi hapswi kukwepa kulitaja kwa makusudi jina kuu kuliko yote, mbinguni na duniani, Jina la Bwana Yesu Kristo.

Ni machukizo mbele za Mungu, kusalimu watu kwa jina la JMT. Hii ni alama ya upagani kabisa.
Katika andiko lako, nakubaliana na wewe kwenye kutaja jina la JMT kwenye salamau badala ya jina la Mungu. Lakini sikubaliani nawe kwenye hoja ya kuwa 'Jina kubwa kuliko yote Mbinguni na duniani kuwa ni Yesu'. Jina Kubwa zaidi ni Mungu Muumba, aliyemuumba huyo Yesu na pia kumtuma duniani, Mungu ambaye ni muweza wa Yote hajaumbwa na yeyote, hajazaliwa, wala hajazaa hajawahi kufa na hatakuja afe.

Mpe heshima yule mwenye kustahiki. Mkuu wa Wilaya hawezi kuwa Mkubwa kumzidi rais aliyemtuma majukumu huko wilayani. Yeye ni mtumishi ila boss yupo pale pale.
 
Ndugu zangu mengi yameibuka tangu kusainiwa kwa mkataba wa DP World. Hii nchi haiongozwi na kiongozi mmoja. Kuna idadi kubwa sana ya viongozi kuanzia wastaafu na waliopo madarakani.

Uamuzi wa kuwakabidhi DP World hakuufanya mwenyewe, aidha alishinikizwa ama lah. Tunaweza kumnyooshea kidole kumbe wapo waliomsababishia hilo tatizo.

Nashauri badala ya kumtuhumu tumtafute na kushauriana naye pengine tutaweza kumsaidia kuondokana na kipindi hiki kigumu.
Kaka, kwenye aya yako ya mwisho umetutaka 'tumtafute tushauriane nate'. Hivi hapo umekusudia rais ama tumtafute nani? Ni kwamba kila mtanzania ambaye hajaelewa juu ya habari hiyo kuhusu DP world, tukamtafute rais tumshauri ama umekusudia nani hasa wakutafutwa? Je unaona uliloshauri linatekelezeka? Wewe ulishawahi mtafuta mkakaa na kushauriana?
 
Ndugu yangu raisi anatoka ndani ya chama. Chama ndio boss wake lazima usikilize chama bila hivyo unapokonywa kiti
Ila ndo mwenyekiti ,sasa asikilize na kuchukua kila aina ya takataka , kama mwenyekiti bado anayo nafasi ya kusema hili sawa lile hapana ,

So hata kuuza bandari zetu aliposhauriwa akaona ni sawa
 
Kaka, kwenye aya yako ya mwisho umetutaka 'tumtafute tushauriane nate'. Hivi hapo umekusudia rais ama tumtafute nani? Ni kwamba kila mtanzania ambaye hajaelewa juu ya habari hiyo kuhusu DP world, tukamtafute rais tumshauri ama umekusudia nani hasa wakutafutwa? Je unaona uliloshauri linatekelezeka? Wewe ulishawahi mtafuta mkakaa na kushauriana?
Njia nzuri ni kumtafuta kushauriana nae kwasababu kaajiriwa na CCM mambo yote anayofanya huwa hapangi mwenyewe analetewa na chama chake
 
Ndio kazi ya bunge??
Tushike lipi??
[emoji116][emoji116]

Ndugu treaty ni mkataba wa makubaliano ambayo inakuwa sehemu sheria unapo ratify. Na mwenye mamlaka ya kufanya ratification ni bunge.

Lakini treaty pekee sio mkataba wa biashara ambao unaweza mshitaki nao mtu, pasipo na mikataba mingine ya utekelezaji.

Badala ya kwenda google na kutumia muda wako kuingia website ya UN kupata maelezo treaty ni kitu gani; we unakimbilia kusikiliza upuuzi wa mkimbizi ambae kutwa ana ugomvi na serikali.
 
Ndugu treaty ni mkataba wa makubaliano ambayo inakuwa sehemu sheria unapo ratify. Na mwenye mamlaka ya kufanya ratification ni bunge.

Lakini treaty pekee sio mkataba wa biashara ambao unaweza mshitaki nao mtu, pasipo na mikataba mingine ya utekelezaji.

Badala ya kwenda google na kutumia muda wako kuingia website ya UN kupata maelezo treaty ni kitu gani; we unakimbilia kusikiliza upuuzi wa mkimbizi ambae kutwa ana ugomvi na serikali.
Kwani google wanaandika malaika?
 
Back
Top Bottom