Msipende kujitafutia faraja humu kwa maamuzi mliofanya ya kutoa watoto English Elementaries na kuwapeleka kayumba. Hakika mna Inferiority complex

Msipende kujitafutia faraja humu kwa maamuzi mliofanya ya kutoa watoto English Elementaries na kuwapeleka kayumba. Hakika mna Inferiority complex

Milioni Moja na nusu Hadi milioni mbili na nusu ni Hela kubwa Kwa mwaka?hiyo ni Hela ndogo sana sema tu watanzania wengi ni masikini sana wa kupindukia ndiyo maana wanaona hizi shule za EM ni gharama wakati hakuna.Zenye gharama ni International kama IST ambayo Kwa mwaka Huwa inafika Hadi milioni sabini
Hakika mkuu
 
Hii mada nilikua naiangalia tu nafanya yangu lakini nilichokuja kugundua kikubwa kabisa,


UKATA

UKATA


UKATA


mtu kaanza kuziponda EMs baada ya mambo kumuendea mrama, itoshe kusema kama una uwezo wa Kayumba ni sawa kwako
Kama una uwezo wa Ems ni sawa pia na kama huna uwezo wa Ems na unajitutumua ni sawa na kongole kwako,

Upuuzi wenu pelekeni kwa wake zenu huko mnakuja humu kupima je uamuzi uliochukua kumuhamisha mtoto EMs ni sahihi kwa kuanzisha mada zenu kwani ulipompeleka mwanzo hukuangalia hizo sababu?

Hicho kilichokufanya umpeleke ni kwamba ulikua nazo na sasa huna ,tafuta pa kuponea

Kuna watu humu kumaliza laki tatu nne baa kila siku kitu cha kawaida unataka akasomeshe mwanae mtimbwani primary nafsi imsute?

We kama umemuhamisha mwanao ni maisha yako hayo usitake huruma huruma za watu ,
Hapa ukishaanza kuona ufagio wa nyumbani njiti zinapungua ujue mwanao huyo anaenda kufagia shule usiseme wachawi🤣🤣
Mkuu unachamba kumzidi Hadija Kopa. Lazima nikupe maua yako.
 
Sio inferiority complex bali ni kugutuka kutoka kwenye usingizi mzito; najua kwamba asilimia kubwa ya Watu wanaotoa watoto English Medium kuwarudisha saint kayumba maisha yanakuwa yameporomoka kidogo lakini tukumbuke mara nyingine inahitajika crisis ya aina hiyo kwa mtu kujitambua

Yaani unalipa ada ya tshs 2M mpaka 3M kwa mwaka ili mtoto aende kusoma shule ambayo ina:
1. Majengo mazuri
2. Inazingatia sana kumkaririsha mwanao majibu kwajili ya mitihani ya taifa
3. Inafundisha kimombo (ambacho kingepatikana English course kwa theluthi ya gharama)

Kiufupi, kama mwanao hasomi shule kama FEZA au International School of Tanganyika (ISJ) basi hizo ada zote unazochoma bila juhudi yako binafsi kama mzazi kuchochea utamaduni wa kujifunza kwa mtoto wako na drive yake mwenyewe basi kazi unayofanya ni bure; yaani bora usupplement elimu ya saint kayumba na tuition heavy afu hela iliyobaki nunua hata viwanja
You are the true son of your Father. Wewe jamaa una akili nyingi mno kiasi unaweza hata kuwaibia kura CCM.

This is what I have been talking about . Aisee ambae hatoelewa hoja yako he will never be wise again
 
Shifa Ni kwamba fainali kwenye ajira.... Ajira hiyo hiyo inapambaniwa Na waliosoma kayumba Na EMS Na wakipata ajira wote training Na mshahara wanalipwa Sawa ...Io ela ya kumpeleka EMS kheri ungemfungulia account umuwekee pesa then akija kujitambua afanye anachokipenda
Mwanamke una akili nyingi Sana wewe. I like the way u think
 
Jibu hoja wanapoteza pesa au hawapotezi? Pitia majumbani fanya utafiti wa vijana waliosomeshwa kwa mamilioni kwa sasa wanamchango gani kwa taifa? Wameweza kujiegemea? Wanaweza kutegemewa? Wazazi wamepata walichokitegemea?
Wote tumesoma nao vyuoni na vilevile tunafanya nao kazi hizi hizi
 
Jibu hoja wanapoteza pesa au hawapotezi? Pitia majumbani fanya utafiti wa vijana waliosomeshwa kwa mamilioni kwa sasa wanamchango gani kwa taifa? Wameweza kujiegemea? Wanaweza kutegemewa? Wazazi wamepata walichokitegemea?
Unataka kijana alietoka chuo moja kwa moja ajitegemee?

UKiweza mpeleke mwanao pvt, akimaliza anaweza amua asideal na alivyosoma kabisa an
 
You are the true son of your Father. Wewe jamaa una akili nyingi mno kiasi unaweza hata kuwaibia kura CCM.

This is what I have been talking about . Aisee ambae hatoelewa hoja yako he will never be wise again
Hicho alichosema @rorsni sahihi kabisa
 
Yani unakuta mtu anakuja na theories sijui ame-google wapi, anaziunganisha unganisha ili tu muonekane mnaosomesha watu shule EMs ni maboya.

Hii yote ajipatie faraja kwa maamuzi magumu aliyoyafanya.

Anasahau kila mtu ana uhuru wa kufanya maamuzi ya kuendana na uwezo wake.

Hakuna aliewahi kuja na nyuzi hapa kuponda wazazi wanaosemesha watoto magomboko praimari ila nyie kwa sababu mna hangaika na maamuzi yenu kutafuta validation basi mnaanza kuponda watu mkiwaita wanapoteza pesa. Mnawaita wapoteza pesa wakati nyie wenyewe mmepangishia milupo kila mitaa ya kati.

UMASIKINI SIO KUKOSA PESA TU.
Mkuu,

Kama kila mtu ana uhuru wa kufanya maamuzi ya kuendana na uwezo wake mbona huwaachii wao kufanya maamuzi, hata kama ni ya kujipa faraja, kutokana na uwezo wao ama wa kifedha ama wa kiakili?

Ukisema uwapotezee hawa wanajifariji tu, kwa kanuni yako hiyo hiyo ya kila mtu ana uhuru wa kufanya maamuzi ya kuendana na uwezo wake, ama wa kifedha, ama wa kiakili, utapungukiwa nini?

Kwa nini hii inakuwa ligi?
 
Mkuu,

Kama kila mtu ana uhuru wa kufanya maamuzi ya kuendana na uwezo wake mbona huwaachii wao kufanya maamuzi, hata kama ni ya kujipa faraja, kutokana na uwezo wao ama wa kifedha ama wa kiakili?

Ukisema uwapotezee hawa wanajifariji tu, kwa kanuni yako hiyo hiyo ya kila mtu ana uhuru wa kufanya maamuzi ya kuendana na uwezo wake, ama wa kifedha, ama wa kiakili, utapungukiwa nini?

Kwa nini hii inakuwa ligi?
100% Fact
 
Mbona hili umeliandikia nyuzi sana. Si kila mtu ana maamuzi juu ya elimu ya mwanae vile atakavyo.
 
Back
Top Bottom