Msiwasingizie Wamarekani mifumo ya kubeba jinsia ya kike katika uongozi Africa, hawahusiki

Msiwasingizie Wamarekani mifumo ya kubeba jinsia ya kike katika uongozi Africa, hawahusiki

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Haijawahi kuwa sera ya Marekani chini ya Rais wa Republican au Democrats kuchochea wanawake wapewe madaraka katika nchi za Africa, hili jambo watu wanalirudia rudia sana kuonyesha kwamba Wamarekani wameturubuni Waafrika kuwapa watu uongozi kwa kigezo cha jinsia yao huko wao wakiwa hawafanyi hivyo.

Mkutano mkubwa wa kijinsia duniani ulioleta maazimio na mabadiliko mengi ya kitaifa kwa wanawake ulifanyikia Beijing China, mikutano mengine yote mikubwa mitatu ya kimataifa iliyotangulia huo haikuwahi kufanyikia Marekani.

Suala la Diversity Equity and Inclusion (DEI) na usawa wa kijinsia bado ni mjadala mkali kwa Wamarekani wenyewe wakiwa wamegawanyika nusu kwa nusu, kama nyie mmekubali kwa wengi wenu kama taifa ni nyie wenyewe tusiwasingizie Wamarekani.

Je ni Wamarekani ndio waliotuambia inabidi tuwe na viti maalumu vya ubunge na udiwani katika katiba yetu?? Kama ni kweli ilikuaje tukalikubali hilo mapema haraka haraka sana halafu mengine wanayotuambia tukayakataa?? Kama ni wao walitushinikiza nini kinatochuzuia kuondoa hayo matakwa ya kijinsia baada ya kujua waliturubuni??

Tuwajibike kwa mambo yetu tuache kutumia Wamarekani kama kichaka cha kujifichia matatizo yetu.
 
Women are perfect,attractive and more respectable at low profile than high profile,this is law of nature,breaking this law result to a public chaos.
 
Afrika Ni machoko tu, nchi zisizo Na lengo lolote hapa duniani wao WaPo tu Kwa ajiri ya kutawaliwa
 
Hakuna Rais atakuja kukuwekea pesa mfukoni awe wakiume awe wa kike. Mtu anakuwa Rais kutimiza ndoto zake
 
Lakini si tunaambiwa hao wenzetu huongoza kwa mifumo na si kwamba rais anakuwa ndio kila kitu kama mfalme, sasa shida ipo wapi kwa mwanamke kuwa kiongozi mkuu wa nchi?
 
Waafrika ni watu wa hovyo Sana! Tulikuwa sawa na waarabu na wahindi sasa hivi wote wametuzidi! Akili tumeweka makalioni tu, shenzi kabisa!
 
Waafrika ni watu wa hovyo Sana! Tulikuwa sawa na waarabu na wahindi sasa hivi wote wametuzidi! Akili tumeweka makalioni tu, shenzi kabisa!
Ukisomesha mwanamke umeisaidia jamii nzima, huo ni msemo tuliuchukulia kinadharia miaka nyuma wakati idadi ya watu ikiwa ndogo lakini leo hii kwa vitendo tunaiona faida ya kumsomesha mwanamke. Hivyo tusilielie tuishi na uhalisia uliopo.
 
Back
Top Bottom