Venus Star
JF-Expert Member
- Dec 6, 2018
- 26,519
- 78,311
Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko yashuhudia ongezeko kubwa la hamasa kupitia kampeni ya Samia Legal Aid Campaign (MSLAC), ambapo elimu ya sheria inaendelea kutolewa kwa wananchi kwa kasi kubwa. Wananchi wamehamasishwa kuhusu masuala ya ardhi, mirathi, ndoa, haki za kijinsia, ajira, na mbinu za suluhisho mbadala wa migogoro.
Kampeni hii imelenga kuwaelimisha wananchi ili kupunguza migogoro na kuongeza usalama wa jamii. Wananchi wameonyesha mwitikio chanya, wakipongeza juhudi hizi zinazochochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Kampeni hii imelenga kuwaelimisha wananchi ili kupunguza migogoro na kuongeza usalama wa jamii. Wananchi wameonyesha mwitikio chanya, wakipongeza juhudi hizi zinazochochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.