Red Scorpion
JF-Expert Member
- Feb 1, 2012
- 5,736
- 4,252
Msomi na Mjinga walienda katika usaili, walipofika kabla hawajaingia wakakubaliana aanze Msomi kisha akitoka ampe majibu Mjinga ili wote wapate kazi.
Basi Msomi akaingia na maswali yakawa hivi:-
Msaili:- Tanzania ilipata Uhuru mwaka gani?
Msomi:- ilitakiwa iwe mwaka 1960 ila ikasogezwa mpaka 1961 kutokana na sababu mbalimbali..
Msaili:- Nani hasa alihusika na upatikanaji wa Uhuru huo?
Msomi:- Kuna watu wengi walihusika ila Mwl. J.K. Nyerere ndiye alikuja kumalizia.
Msaili:- Inasemekana ktk sayari ya Mars kunaviumbe wanaishi, je ni kweli?
Msomi:- Watu wengi wanasema hivyo lakini haijathibitishwa na wanasayansi.
Baada ya Msomi kutoka basi Mjinga akapewa majibu yote..
Kuingia ktk usaili maswali yakawa hivi:-
Msaili:- Tuambie ulizaliwa mwaka gani?
Mjinga:- Ilitakiwa iwe mwaka 1960 ila ikasogezwa mbele mpaka mwaka 1961 kutokana na sababu mbali mbali.
Msaili:- Mungu Wangu, BABA yako anaitwa nani?
Mjinga:- Kuna watu wengi walihusika ila Mwl. J. K. Nyerere ndiye alikuja kumalizia .
Msaili:- Hivi wewe ni chizi?
Mjinga:- watu wengi husema hivyo lakini haijathibitishwa na wanasayansi...
Haji
Basi Msomi akaingia na maswali yakawa hivi:-
Msaili:- Tanzania ilipata Uhuru mwaka gani?
Msomi:- ilitakiwa iwe mwaka 1960 ila ikasogezwa mpaka 1961 kutokana na sababu mbalimbali..
Msaili:- Nani hasa alihusika na upatikanaji wa Uhuru huo?
Msomi:- Kuna watu wengi walihusika ila Mwl. J.K. Nyerere ndiye alikuja kumalizia.
Msaili:- Inasemekana ktk sayari ya Mars kunaviumbe wanaishi, je ni kweli?
Msomi:- Watu wengi wanasema hivyo lakini haijathibitishwa na wanasayansi.
Baada ya Msomi kutoka basi Mjinga akapewa majibu yote..
Kuingia ktk usaili maswali yakawa hivi:-
Msaili:- Tuambie ulizaliwa mwaka gani?
Mjinga:- Ilitakiwa iwe mwaka 1960 ila ikasogezwa mbele mpaka mwaka 1961 kutokana na sababu mbali mbali.
Msaili:- Mungu Wangu, BABA yako anaitwa nani?
Mjinga:- Kuna watu wengi walihusika ila Mwl. J. K. Nyerere ndiye alikuja kumalizia .
Msaili:- Hivi wewe ni chizi?
Mjinga:- watu wengi husema hivyo lakini haijathibitishwa na wanasayansi...
Haji