Naona watu wanajadili hili suala kwa hisia zaidi kuliko uhalisia wa sheria za haki miliki...za kitaifa na kimataifa ni hivi:
1) Protection ya copyright ni automatic i.e sio lazima uisajili kazi yako ndio ipate legal protection la hasha..hii ni tofauti na ishu kama vile Trade marks na patents/innovations/inventions hizi ili zipate ulinzi kisheria ni lazima zisajiliwe katika mamlaka husika,ili mtu mwengine akitumia kimakosa (bila idhini) uweze kumshtaki na kumdai fidia kwa kutumia trademark/uvumbuzi yako/wako kibiashara...
Huku kwenye copyright kinachohitajika ni msanii kuweza kuipublish kazi yake tu kwa umma basi,legal protection after that comes into play automatically no need for registration. Kwa hiyo kinacholindwa na sheria ni "expression of idea and not the idea itself" kwa mfano,umetayarisha kazi yako ya sanaa kisha ukaiweka ndani,lets say, kitabu cha riwaya ikawa bado hujakitoa kwa jamii ili watu waione hiyo kazi yako. Na baadae mimi nikaja kwako na kukiona hicho kitabu nikakichukua bila ridhaa yako nikaenda kukikopi chote half jina la mtunzi nikaweka langu baada ya muda mfupi nikawahi kukitoa kwa jamii kabla yako.
Katika mazingira kama hayo basi sheria itanilinda mimi mwizi na sio wewe original writer hii ni kwa sababu sheria na jamii now inanitambua mimi ndo kama original owner of the work coz ndo kwa mara ya kwanza waliiisikia/kuiona kutoka kwangu...sasa hata wewe ukija kuclaim baadae kwamba ile kazi ilikuwa ni ya kwako, watu wataona unatafuta kiki tu...rejea ishu ya diamond na dayana nyange kwenye wimbo wa "Namba one Orig."
2) Ili kuonekane kuna breach of copyrighted work for the purpose of enforcing it for compensation...lazima wrongdoer awe amecopy "the substantial part of the artistic work and not just little part". kwa mujibu wa sheria kinacho determine breach of copyright ni the extent/substantiality of the said breach and not mere breach, kuna wadau wamesema hapo juu kwamba at least ifikie 20% ya copied work .na lazima hiyo kazi iliyokopiwa itumiwe na huyo wrongdoer for economic gain,mere fair use does not amount to breach of copyrighted work.
Kwa hiyo wazee wetu wa Msondo kwenye hii kesi yao hawataambulia kitu..kwa sababu sehemu wanayodai kuibiwa kazi yao ni nduchu sana kwenye kazi nzima ya Zilipendwa...yaani ni kule mwisho mwisho wa wimbo ktk kukazia kazia tu utamu wa beats.
All in all, so far hakuna haki iliyovunjwa kwa hao wazee...na hapo mimi nimetaja point moja tu ila kuna hoja nyingi hapo zitaibuka,ikiwemo umiliki wa huo wimbo/beats,kama kweli wcb wamecopy au ni mfanano tu wa mapigo ambacho ni kitu cha kawaida. Kama ni rahisi kiasi hicho nazani watoto wa marehemu Rajabu Marijani nao waje wawadai WCB hususani Harmonize kwa kutia kionjo kidgo cha wimbo wa Sina Makosa kule mwisho mwa wimbo wa Zilipendwa..."yelelelileleeeeee"
Mawakili wao ni ama hawajui vyema sheria za copyright au wanajua ila wanataka tu kula hela za maskini hao kwa kuwa vyuma vimekaza,hivyo hata ule ubinaadamu umewaondoka.