Msumbiji: Akutwa na kichwa na viungo vya siri vya mtu kwenye mfuko

Msumbiji: Akutwa na kichwa na viungo vya siri vya mtu kwenye mfuko

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
pexels-kat-wilcox-923681-scaled.jpg

JESHI la Polisi nchini Msumbiji linamshikilia mwanaume mmoja baada ya kumkuta na kichwa na sehemu za siri za mwanaume ambaye amekiri kuuua mtu na kukata viungo hivyo.

Msemaji wa kamandi ya polisi ya Sofala, Dércio Chacate, amesema Watoto waligundua sehemu za miili hiyo kwenye mfuko wa plastiki katika wilaya ya Nhamatanda na kutoa taarifa kwa mamlaka.

“Mshukiwa alikiri kuua na kukata vichwa vya watu wengine watatu, uchunguzi unaendelea ili kuwakamata wanaodaiwa kuwa wapangaji na wanunuzi wa viungo hivyo” amesema Chacate.

Viungo vya mwili hutumiwa na baadhi ya wanaoitwa madaktari wa jadi kutengeneza dawa, ambazo kwa uwongo wanadai zinaweza kutibu magonjwa, kuondoa dalili mbaya na kuboresha maisha ya watu.
 
Back
Top Bottom