Hizi kesi zinaweza kumkuta hata asie na hatia kutokana na Hayo maeneo ni makazi ya watu na wanafanya shughuli zao za kila Siku
Kwa mfano mvuvu anaweza kuuza samaki kwa mtu anahestuhumiwa ugaidi na ww ukajumlishwa kwenye kesi
Unaweza kuwa muuza duka magaidi wakanunua hapo ukaambiwa ww ni suppliers wa magaidi
Unaweza kuwa unavusha watu bila kujua ukaambiwa ww Ndio unawavusha
Ilimradi basi tu.
Kwa hiyo wengi wanapata misala na hawana WA kuwatetea na wanaishia kupigwa nyundo na kutangulia akhera.
HILI SAKATA LILIANZA KAMA KWA SURA YA UISLAMU NA ALSHABAB LAKIN UKWELI WANAUJUA WENYEWE KWAMBA HAPA UISLAMU NA UGAIDI UKITUMIWA TU NA MEDIA KAMA KIKI ILI KULIPAISHA JAMBO NA KULETA HOFU KWA WANANCHI
WALE JAMAA WAPO MBALI NA UISLAMU KABISA YALE MAENEO YENYE VURUGU KUNA GESI PALE NDIO MAANA WATU WANAUANA
SASA TUSEME WAISLAMU WA MOZAMBIQUE AU TANZANIA HATA WAKICHUKUA MAENEO YALE HIYO GESI WATAIFANYIA NINI ?????? FIKIRI KABLA YA KUSEMA UGAIDI
PALE KUNA MIKONO YA NCHI ZINAZOTAKA KUPORA NDIO MAANA VURUGU HAZITAISHA LEO! KAMA KILE KINACHOTOKEA GOMA.
NB NASIKIA VYOMBO VYABHABARI VYA MOZAMBIQUE VIMEKATAZWA KUANDIKA HABARI ZA ILE KANDA NI KAMA WANAWAPA AIRTIME NA KUWEKA HOFU KWA WANANCHI NA UKIONEKANA UMEANDIKA HABARI ZA KULE UNAKULA MIAKA JELA.!
Kwa kiasi fulani uko sahihi sana.
Ukichunguza kwa umakini Sana utagundua kwamba yale maeneo karibia yote yenye vurugu kule Msumbiji yana historia kongwe sana kuhusiana na suala la vurugu za kisiasa, hata kabla ya Taifa hilo la Msumbiji halijapata uhuru wake kutoka kwa mkoloni wao Ureno. Kambi nyingi sana za Makundi ya kisiasa ya Wapigania Uhuru wa nchi hiyo ya Msumbiji ziliwekwa katika ukanda huo wa Kaskazini mwa nchi hiyo, maeneo ambayo hadi leo hii bado yanaendelea kukumbwa na vurugu. Makundi ya Wapigania Uhuru ya vyama vya Siasa vya FRELIMO na RENAMO vilikuwa na Kambi zao nyingi za wazi na za siri kubwa ktk maeneo hayo yenye vurugu kwa sasa. Baada ya kufanikisha suala la kuuangusha utawala wa mkoloni wao Ureno, maeneo hayo tayari yalikuwa yamevurugwa vibaya sana na vita vya ukombozi, miundombinu yote ya kujenga uchumi kama vile viwanda viliharabiwa kabisa na mapigano ya vita.
Mbaya zaidi, hata chama cha Siasa cha FRELIMO kilipofanikiwa kushika madaraka ktk nchi hiyo ya Msumbiji, haikukishirikisha Chama cha RENAMO ktk kuitawala nchi hiyo ya Msumbiji, badala yake vyama hivyo viligawanyika na kuwa vyama vinavyohasimiana, vikapigana vita tena wao kwa wao ili kugombea kupata udhibiti wa madaraka ktk nchi hiyo, hatimaye Chama cha RENAMO kilizidiwa nguvu na kushindwa vita. Chama cha FRELIMO kutokana na msaada mkubwa waliopata kutoka kwa Mwl. J. K. Nyerere na CCM yake, walifanikiwa kuhodhi na kudhibiti mamlaka na madaraka yote ya nchi hiyo ya Msumbiji, na RENAMO kikawa Chama kikuu cha Upinzani dhidi ya FRELIMO.
Mbaya zaidi tena, utawala wa FRELIMO ulikichukulia Chama cha RENAMO kama Kundi la Waasi wala siyo Chama cha Siasa, Matokeo yake Wanachama na Wapiganaji wa RENAMO wakakimbilia msituni na kuweka Kambi zao nyingi za Siri kwenye huo Upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo ya Msumbiji.
Serikali ya Msumbiji Kama ililitelekeza kabisa kwa muda mrefu eneo hilo lililopo Kaskazini mwa nchi hiyo kwa sababu ililiona kama eneo lenye maficho ya Waasi wa RENAMO, hata huduma za kijamii zilikuwa duni sana kwenye maeneo hayo. Wananchi wengi wa upande huo wa Kaskazini mwa nchi waliona kama Serikali ya Msumbiji imewatenga na haikuwa inawajali. Serikali ilijichimbia mizizi kwenye eneo la Kusini mwa nchi hiyo ya Msumbiji na kuigawa nchi ktk mapande mawili ya Kaskazini na Kusini. Serikali hiyo ya Msumbiji ilirudi tena kwa kasi upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo baada ya Ugunduzi wa Nishati ya Gesi kwenye maeneo hayo ya Kaskazini, hapo ndipo ukawa mwanzo mpya wa kuibuka kwa Vurugu hizi zinazoendelea hivi sasa ktk eneo hilo la Kaskazini mwa nchi hiyo ya Msumbiji.
Suala la Dini au Udini ktk vurugu hizo za huko Msumbiji linatumika tu na wahusika kama "SCAPEGOAT" ili kuweza kupata msaada wa kijeshi na wa silaha za kupigania vita dhidi ya maadui zao.