Msumbiji Wamekodisha Bandari ya Nacala Kwa Malawi & Zambia Kwa Miaka 100. Tanzania Kupoteza Mteja namba 2 wa Dar Port

Wawaondoe magaidi kwanza. Tuna muda wa kujipanga.
 
Uko na maarifa mingi ndugu mnaitajika
 
Suala la Bandari ya Nacaram Msumbiji na Lobito Angola ni wazo la siku nyingi la hao watu.

Bahati mbaya sana wametukuta tunachelewa kufikiria na tunafikiri na kila mtu anachelewa kufikiria kama sisi.

Kuna kitu kinaitwa Blackmailing, blackmailing hutumika pia kwenye uchumi kwenye dunia ya kimafia na kibepari.
Tungekuwa tunawahi kufikiria basi tungeshafanya blackmailing kwenye mataifa mengi ya kusini na africa mashariki upande wa LOGISTIC NA ENERGY - na hela yake ingetosha kabisa kuendesha uchumi wa hii nchi.

Unapozungumzia LOGISTIC, unaziweka Bandari tatu kama main hub, unaziunganisha hizi bandari na Bandari kavu kwenye kila border yetu, pale tunduma unaweka Dry port kubwa na mizigo yote ya kusini Destination inakuwa Tunduma dry port. Reli kutoka Mtwara port via Songea inaunga pale Makambako, unaipeleka Tunduma.
Unajenga Dry port kuubwa pale Isaka kahama kuhudumia Rwanda, Burundi na baadhi ya maeneo ya DRC kutokea ISAKA na mizigo yao yote destination inakuwa pale Isaka.
Unajenga Dry port pale Mwanza karibu ya Ziwa Victoria kuhudumia baadhi ya maeneo ya Uganda na hata Kenya nk
Serikali ihakikishe inakuwa na shipping line ya Meli za uhakika za mizigo lake Tanganyika na lake Victoria kuhudia maeneo ya Uganda na DRC kwa kuyaconnect na hizi Dry port.
Kuwe na shipping line baharini Kwa ajili ya mizigo kuanganisha Bandari zote tatu.

Kuifanya hayo yote hapo juu unapunguza gharama za ushuru ukilenga kuongeza volume na cost unazicover volume ikiwa kubwa.

Kwenye upande wa Gas na Maji, kupitia hydro plants na Gas plants tungeweza kuzarisha umeme mwingiiii na kuuza Kwa gharama nafuu Kwa majirani wote hawa kuanzia kusini, mashariki mpaka magharibi, tungewalemaza Kwa kuwauzia umeme Kwa gharama ndoogo kabisa kiasi kwamba wasingefikiria tena kuzarisha umeme wao ilihali upo umeme wa gharama nafuu kutokea Tanzania.

Hivyo vyote tungekuwa tumefanya tungekuwa tumeshawablackmail majirani woote wa ukanda huu na Taifa hili lingekuwa economic giant wa Africa.
 
Hiyo Nacala(Nashala) kasikazini ya msumbiji kuna miji ya Mpemba na Palmas hayo maeneo yana reli inayotoka Nashala hadi Nampula kwahiyo kwenda Malawi ni kuongezea tu kutoka Nampula hadi Bulawayo/Lilongwe huko Malawi. Hii imekaa vizuri kwa Malawi/ Zambia na ni Mbaya kwa Tanzania. Changamoto. 1. Msumbiji ina waasi wa IS wameenea kasikazini ya nchi katika maeneo hayo ya Palmas, Pemba, Nashala, Montpuez, na na Nampula kiuslama ni changamoto kwa mradi. 2. Msumbiji ina changamoto z kiusalama katika eneo lake na mpaka na Malawi jimbo la NIASA ambapo reli inapita, kuna Waasi wa RENAMO kiongozi wao Dracama, wanaopingana na FRELIMO. 3. Mizigo mingi kwa nchi za Afrika inatoka Bahari ya Hindi China, India, Japan sasa ili meli ifike bandari ya Nacala lazima ipite Afrika mashariki kijiografia (Mombasa na Dar Es Salaam) kwahiyo Tanzania ina nafasi kibiashara. 4. Mozambique na Malawi ni maskini hasa, na ni wavivu wa kufanya lobbying za kutafuta na kufanya miradi mikubwa kwahiyo mpaka mradi ufike Zambia labda ni 2050 ambapo sisi tutakua hatua nyingine. 5. Tanzania itengeneze bomba la gas ya LPG, liende Malawi, Zambia, Zimbabwe, Botswana, South Afrika, Congo ,Burundi, Rwanda, pamoja na kiwanda cha LPG, hii itamuahi Mozambique maana Mozambique ana kiwanda tayari cha LPG pale Palmas ila hajapata akili ya kusambaza kwa waafrika wenzie, gas inaripa ukisambaza kwa jirani zako angalia Urusi na Qatara wanavyofanikiwa. 6. Tanzania iwekeze SGR kwenda Burundi, Rwanda na Congo tu, hao ndio wateja walio kiganjani kwetu, Uganda tumuachie Kenya, Malawi tumuachie Mozambique sio kutaka kila nchi uchukue wewe hiyo sio Uafrika. 7. Tujenge uchumi wa Tanzania na miundombinu yake, kwa ajili ya Tanzania na watu wake, si kwa ajili ya kuipata nchi fulani, maana biashara hubadilika, lakini ustawi wa nchi ubaki pale pale, kwahiyo Mozambique kuipa bandari Malawi huo ndio Uafrika, Tanzania haitaji kujitukana na kujilaumu.
 
Kuna Banana Deep sea port inajengwa DRC na DP world kuongeza volume ya mizigo hapo DRC

Japo ni linchi likubwa na maeneo mengi kijografia hayafikiki ila zipo Cargo planes nyingi zinaoperate DRC, maana yake tunakwenda pia kupoteza kiasi fulani cha mizigo ya DRC.
 
Tatizo la Viongozi wetu mda mwingi wamewekeza kwenye siasa kila kitu,kuwaruhusu watu wenye akili ndogo ndiyo wabebe maono ya inchi hii yaani chawa, huku wakiwaacha wenye akili kubwa ilimradi tu wanapingana nao kisiasa
Tena siasa uchwara na nyepesi
 
Tanzania bado itabaki kuwa njia salama zaidi katika maswala ya Bandari kutokana na hali za kiusalama
 
Unajua mtu unapoiongelea inchi ya watu lazima uwe na uhakika wa unachokiongea, RENAMO ni chama pendwa Mozambique kama ilivyo Chadema Tanzania sababu wao wako kwa ajili ya kuwatetea wananchi dhidi ya zuruma za selikari
Na kimepoteza nguvu baada ya Alfonso dhalakama kufa,selikari imepenyeza rupia hawana nguvu kivile,ingawa bado wanaushawishi kwenye miji mikubwa kama Maputo na Nampula
Magaidi hawa wa Cabdelgado no Pemba walioko kaskazini hawa ndiyo adui wa Mozambique,na ni Watanzania kwa asilimia kubwa ndiyo wanaofanya uharibifu lakini wanasaport kutoka kwa baadhi ya viongozi wa selikali
 
TRA ni jipu lisilokamulika,jamaa wapo kizamani sana
 
hii ngonjera tu
 
Tutakuja kushituka hizo Bandari zimesalia kuhudumia Mikoa yetu pekee,washindani Wetu wamechukua keki.

Lazima tuingie kufanya mambo ya umafia Kwa maslahi ya Nchi
Mama Samia huo uwezo wa kuwaza hivyo hana,kamkumbatia Kagame na anamuogopa haswa,aliacha kwenda kwenye uapisho wa Tshisekedi lakini juzi kwa Kagame alikwenda haraka sana,kapeleka kule jeshi lakini sidhani kama yeye analipa sapoti yoyote,ni kama linasukumwa tu na CDF
 
Samia ndio anatakiwa kuwaza badala ya Wizara husika? Acha kuwa mjinga ,huo ni wajibu wa wataalamu wa Wizara za Ujenzi,uchukuzi, Usafirishaji na biashara
 
Hao Malawi na Zambia ni masikini sana, tusipoteze muda shindana nao.
Sisi tuondoe umazoea
Kwanza hiyo ni mipango tu ya serikali za kiafrika na hela zao za kuunga unga. Uongozi ukibadilika kwenye nchi moja tu, mipango yote kwishney. Pesa yenyewe ya kujengea reli hawaipati leo wala kesho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…