Mtaa mgumu sana aisee

Mtaa mgumu sana aisee

Lexus SUV

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2016
Posts
4,493
Reaction score
5,591
Japo leo nimegonga ghorofa ya 3 net. ila naona mtaa siusomi kabisa na ni hali halisi pesa inayopatikana ni kulisha tumbo tu. Hata investments nazo anzisha ni pesa zinahitaji ili na zenyewe zilete pesa kama return on investments (ROI) ila dah

Najikaribisha mtaani kwa mara nyingine.
 
Unagundua ,wale uliokuwa unawaita kina anko na baba wadogo enzi ukiwa mtoto ndiyo umekuwa wewe sasa kwa machalii/ma ankoli.

Mbaya zaidi wale kina anko na baba wadogo ambao ulikuwa unawaomba Hela ya kalamu na daftari kwa ajili ya matumizi ya shule alafu walikujibu hawana au watakupa siku nyingine kisha ukawaona wakuda na kuwasemea kwa mama yako.

Wale kina anko na wajomba waliokuwa wanakuja kusalimia kwenu miss ya jioni kisha wanaambiwa na mama yako wasiondoke hadi wale,wewe ukawaona kama wakuda wanamaliza msosi wenu.

Hao jamaa wote Leo ndiyo umegeuka wewe sasa.

Ukiona simu za wajomba na watoto wa dada unasonya n kusema " Hawa wapuuzi wanadhani Hela zinaokotwa tu Huku mjini".

Mungu atuhurumie wanaume.

Maisha yetu,wazazi wetu,watoto wetu,wanawake na ndugu zetu,wote hao maisha yao yanatutegemea sisi tuokoe jahazi na mbaya zaidi ramani zimepotea tunakwenda bila dira. Tunasubiri kudura ya Mungu tu kutunusuru!!

Mkuu pole sana. siku yako inakuja.
 
Japo leo nimegonga ghorofa ya 3 net . ila naona mtaa siusomi kabisa na ni hali halisi pesa inayopatikana ni kulisha tumbo tuu......hata investments nazo anzisha ni pesa zinahitaji ili na zenyewe zilete pesa kama return on investments (ROI) ila dah


najikaribisha mtaani kwa mara nyingine............
Unajenga ghorafa tatu alafu unasema mtaa mgumu!
Omba radhi mkuu
 
Yaani wewe jamaa una miaka 30? Kwa hizi comment zako na nyuzi za kipuuzi nilidhani utakuwa dogo wa miaka 17-21 something. Kwa akili zako kwa mujibu wa posts na threads zako basi ina make sense kuona maisha ni magumu yasiyo na njia ya kutokea.

Watanzania mnakwama wapi aisee?
 
Back
Top Bottom