Mtaa wa Muhidin Mfaume Kimario Kinondoni Moscow

Mtaa wa Muhidin Mfaume Kimario Kinondoni Moscow

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MTAA WA MUHIDIN MFAUME KIMARIO KINONDONI MOSCOW

Leo nikiwa na ndugu yangu mwanahistoria na maktaba inayotembea Hamisi Hababi tumekutana na kibao cha Mtaa wa Kimario Kinondoni Moscow tukaamua kukipiga picha kibao hicho.

Hakika inafurahisha kukuta kumbukumbu kama hizi za wazalendo walioipigania Tanzania katika hali na nyadhifa zao iwe wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika au baadae katika Tanganyika huru.

Muhidin Kimario alifikia ngazi ya Major General katika Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Muhidin Kimario nyumbani kwao Moshi, Mtaa wa Chini kulikuwa na Zawia ya Tariqa Quadirriyya ambayo ipo hadi leo na unaweza kusema inakimbilia miaka 100 sasa.

Nikiwa mtoto mdogo namkumbuka Muhidin Kimario akiwa mwalimu Muslim School Moshi pamoja na walimu wengine ambae ninaemkumbuka ni Mwalimu Badi ambae alikuwa ndiye mwalimu akisomesha Qur'an katika shule hiyo.

Miaka mingi baadae sasa mimi mtu mzima nilikutana na Mwalimu Badi jirani ya Msikiti wa Raidha na nikamkumbuka lakini yeye hakunikumbuka hata kidogo.

Mimi nilikuwa nasoma Stanley Primary School jirani sana na Muslim School na vipindi vya dini shule yetu ingawa ilikuwa ya Walutheri wanafunzi Waislam walikuwa wanaruhusiwa kwenda Muslim School kuhudhuria vipindi vya dini wakisoma darasa moja na wanafunzi wa Muslim School.

Mwalimu wetu wa dini alikuwa Mwalimu Badi.

Picha hiyo hapo chini inamuonyesha Muhidi Kimario akiwa mtoto mdogo hajafika hata miaka 10 amekaa chini ya miguu wa masheikh wake.

Picha nyingine inamuonyesha Muhidin Kimario katika ujana wake na picha ya mwisho akiwa katika mavazi yake ya Brigadier General.

Brigadier Muhidin Kimario alipata kunidokeza kuwa alikuwa anaandika historia ya maisha yake na akasema kuwa ikikamilika angependa In Shaa Allah niitupie jicho.

Hatukuonana tena baada ya siku ile.

Allah amrehemu na amweke mahali pema peponi.

1686773884816.png
1686773914897.png

1686773944955.png

 
..Ni Meja Jenerali Muhidin Mfaume Kimario.

..Jina la kivita anaitwa " Kamanda Mbogo. "

..Kimario ndiye kamanda aliyeongoza mapigano ya Sembabule au the battle of Sembabule.

..Majeshi ya Tanzania yalikuwa ktk wakati mgumu sana.

..Hapo Sembabule kulikuwa karibu na yalipo makambi ya Tiger Regiment ya Uganda.

..Kulitokea mapigano makali kati ya vijana wetu wa Jwtz [ brigade # 205] na majeshi ya Amin.

..Vijana wetu wa Jwtz walikuwa ktk hatari ya kushindwa mapigano hayo, na wajuzi wa mambo ya kivita wanasema Tanzania angepigwa Sembabule, basi angeshindwa vita.

..Hali ktk uwanja wa mapambano ilikuwa tete mno kiasi cha kulazimisha Mkuu wa Jwtz, na kamanda wa divishen kutembelea uwanja wa mapambano kuhakiki kinachoendelea.

..Kutokana na askari wetu kukwama ilibidi aitwe Brigedia Muhidin Kimario kuongoza mapambano ya kuwakwamua vijana wetu. Kimario aliifanya kazi hiyo kwa weledi mkubwa na ushindi ukapatikana.
 
MTAA WA MUHIDIN MFAUME KIMARIO KINONDONI MOSCOW

Leo nikiwa na ndugu yangu mwanahistoria na maktaba inayotembea Hamisi Hababi tumekutana na kibao cha Mtaa wa Kimario Kinondoni Moscow tukaamua kukipiga picha kibao hicho.

Hakika inafurahisha kukuta kumbukumbu kama hizi za wazalendo walioipigania Tanzania katika hali na nyadhifa zao iwe wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika au baadae katika Tanganyika huru.

Muhidin Kimario alifikia ngazi ya Major General katika Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Muhidin Kimario nyumbani kwao Moshi, Mtaa wa Chini kulikuwa na Zawia ya Tariqa Quadirriyya ambayo ipo hadi leo na unaweza kusema inakimbilia miaka 100 sasa.

Nikiwa mtoto mdogo namkumbuka Muhidin Kimario akiwa mwalimu Muslim School Moshi pamoja na walimu wengine ambae ninaemkumbuka ni Mwalimu Badi ambae alikuwa ndiye mwalimu akisomesha Qur'an katika shule hiyo.

Miaka mingi baadae sasa mimi mtu mzima nilikutana na Mwalimu Badi jirani ya Msikiti wa Raidha na nikamkumbuka lakini yeye hakunikumbuka hata kidogo.

Mimi nilikuwa nasoma Stanley Primary School jirani sana na Muslim School na vipindi vya dini shule yetu ingawa ilikuwa ya Walutheri wanafunzi Waislam walikuwa wanaruhusiwa kwenda Muslim School kuhudhuria vipindi vya dini wakisoma darasa moja na wanafunzi wa Muslim School.

Mwalimu wetu wa dini alikuwa Mwalimu Badi.

Picha hiyo hapo chini inamuonyesha Muhidi Kimario akiwa mtoto mdogo hajafika hata miaka 10 amekaa chini ya miguu wa masheikh wake.

Picha nyingine inamuonyesha Muhidin Kimario katika ujana wake na picha ya mwisho akiwa katika mavazi yake ya Brigadier General.

Brigadier Muhidin Kimario alipata kunidokeza kuwa alikuwa anaandika historia ya maisha yake na akasema kuwa ikikamilika angependa In Shaa Allah niitupie jicho.

Hatukuonana tena baada ya siku ile.

Allah amrehemu na amweke mahali pema peponi.

View attachment 2657869
Aaaaaaaaaaaaaaaamin
 
Duh, huyu mrombo nani alimsilimisha?

Wachaga waislam wanapatikana:
-Masama ukanda wa kwa Sadala
-Lyamungo ambapo ni mpakani mwa Kibosho na Machame.
 
Mshangao wa kwanza ni kuwa Kimario kumbe alikuwa Islam, okay.

Kweli nilisikia miaka ile kuwa jeshi letu lililemewa sana huko kwa nduli, japo ilikuwa siri kuu.

Kuhusu hilo alilokuambia kuwa anaandika historia yake hebu jaribu kufuatilia yawezekana makaratasi yakawepo.

Itakuwa nzuri kwenye makumbusho ya Taifa au hata hapa jf tu.
 
Mshangao wa kwanza ni kuwa Kimario kumbe alikuwa Islam, okay.

Kweli nilisikia miaka ile kuwa jeshi letu lililemewa sana huko kwa nduli, japo ilikuwa siri kuu.

Kuhusu hilo alilokuambia kuwa anaandika historia yake hebu jaribu kufuatilia yawezekana makaratasi yakawepo.

Itakuwa nzuri kwenye makumbusho ya Taifa au hata hapa jf tu.
Mam...
Ahsante.
 
..Ni Meja Jenerali Muhidin Mfaume Kimario.

..Jina la kivita anaitwa " Kamanda Mbogo. "

..Kimario ndiye kamanda aliyeongoza mapigano ya Sembabule au the battle of Sembabule.

..Majeshi ya Tanzania yalikuwa ktk wakati mgumu sana.

..Hapo Sembabule kulikuwa karibu na yalipo makambi ya Tiger Regiment ya Uganda.

..Kulitokea mapigano makali kati ya vijana wetu wa Jwtz [ brigade # 205] na majeshi ya Amin.

..Vijana wetu wa Jwtz walikuwa ktk hatari ya kushindwa mapigano hayo, na wajuzi wa mambo ya kivita wanasema Tanzania angepigwa Sembabule, basi angeshindwa vita.

..Hali ktk uwanja wa mapambano ilikuwa tete mno kiasi cha kulazimisha Mkuu wa Jwtz, na kamanda wa divishen kutembelea uwanja wa mapambano kuhakiki kinachoendelea.

..Kutokana na askari wetu kukwama ilibidi aitwe Brigedia Muhidin Kimario kuongoza mapambano ya kuwakwamua vijana wetu. Kimario aliifanya kazi hiyo kwa weledi mkubwa na ushindi ukapatikana.
Frontline hali ilikuaje na walikufa wanajeshi wangapi na kujeruhiwa wangapi???
 
..Ni Meja Jenerali Muhidin Mfaume Kimario.

..Jina la kivita anaitwa " Kamanda Mbogo. "

..Kimario ndiye kamanda aliyeongoza mapigano ya Sembabule au the battle of Sembabule.

..Majeshi ya Tanzania yalikuwa ktk wakati mgumu sana.

..Hapo Sembabule kulikuwa karibu na yalipo makambi ya Tiger Regiment ya Uganda.

..Kulitokea mapigano makali kati ya vijana wetu wa Jwtz [ brigade # 205] na majeshi ya Amin.

..Vijana wetu wa Jwtz walikuwa ktk hatari ya kushindwa mapigano hayo, na wajuzi wa mambo ya kivita wanasema Tanzania angepigwa Sembabule, basi angeshindwa vita.

..Hali ktk uwanja wa mapambano ilikuwa tete mno kiasi cha kulazimisha Mkuu wa Jwtz, na kamanda wa divishen kutembelea uwanja wa mapambano kuhakiki kinachoendelea.

..Kutokana na askari wetu kukwama ilibidi aitwe Brigedia Muhidin Kimario kuongoza mapambano ya kuwakwamua vijana wetu. Kimario aliifanya kazi hiyo kwa weledi mkubwa na ushindi ukapatikana.
Kuna askari mstaafu wa uganda aliniadithia hiyo event ya Sembabule na vikosi vya Tiger Regment
 
Mshangao wa kwanza ni kuwa Kimario kumbe alikuwa Islam, okay.

Kweli nilisikia miaka ile kuwa jeshi letu lililemewa sana huko kwa nduli, japo ilikuwa siri kuu.

Kuhusu hilo alilokuambia kuwa anaandika historia yake hebu jaribu kufuatilia yawezekana makaratasi yakawepo.

Itakuwa nzuri kwenye makumbusho ya Taifa au hata hapa jf tu.
Nadhani aandike anachokifahamu na atakachotafiti kisha aoanishe na makaratasi ya historia kama yapo
 
MTAA WA MUHIDIN MFAUME KIMARIO KINONDONI MOSCOW

Leo nikiwa na ndugu yangu mwanahistoria na maktaba inayotembea Hamisi Hababi tumekutana na kibao cha Mtaa wa Kimario Kinondoni Moscow tukaamua kukipiga picha kibao hicho.

Hakika inafurahisha kukuta kumbukumbu kama hizi za wazalendo walioipigania Tanzania katika hali na nyadhifa zao iwe wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika au baadae katika Tanganyika huru.

Muhidin Kimario alifikia ngazi ya Major General katika Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Muhidin Kimario nyumbani kwao Moshi, Mtaa wa Chini kulikuwa na Zawia ya Tariqa Quadirriyya ambayo ipo hadi leo na unaweza kusema inakimbilia miaka 100 sasa.

Nikiwa mtoto mdogo namkumbuka Muhidin Kimario akiwa mwalimu Muslim School Moshi pamoja na walimu wengine ambae ninaemkumbuka ni Mwalimu Badi ambae alikuwa ndiye mwalimu akisomesha Qur'an katika shule hiyo.

Miaka mingi baadae sasa mimi mtu mzima nilikutana na Mwalimu Badi jirani ya Msikiti wa Raidha na nikamkumbuka lakini yeye hakunikumbuka hata kidogo.

Mimi nilikuwa nasoma Stanley Primary School jirani sana na Muslim School na vipindi vya dini shule yetu ingawa ilikuwa ya Walutheri wanafunzi Waislam walikuwa wanaruhusiwa kwenda Muslim School kuhudhuria vipindi vya dini wakisoma darasa moja na wanafunzi wa Muslim School.

Mwalimu wetu wa dini alikuwa Mwalimu Badi.

Picha hiyo hapo chini inamuonyesha Muhidi Kimario akiwa mtoto mdogo hajafika hata miaka 10 amekaa chini ya miguu wa masheikh wake.

Picha nyingine inamuonyesha Muhidin Kimario katika ujana wake na picha ya mwisho akiwa katika mavazi yake ya Brigadier General.

Brigadier Muhidin Kimario alipata kunidokeza kuwa alikuwa anaandika historia ya maisha yake na akasema kuwa ikikamilika angependa In Shaa Allah niitupie jicho.

Hatukuonana tena baada ya siku ile.

Allah amrehemu na amweke mahali pema peponi.

View attachment 2657869
On a personal note, Gen Muhiddin Kimario alikwa mtu mpole, mnyenyekevu na hakuwa na makuu.
Mimi nilionana naye miaka yake ya mwishoni na alishangaa sana kuwa kumbe tulikuwa karibu.
Baba yangu ambaye vile vile alikuwa mwanajeshi aliyekuwa karibu na Gen Kimario walikuwa wote serikali ya Mwalimu Nyerere.
Alinipokea kwa bashasha na tuliongea mambo mengi.
Tulikwenda sote kwenye mmoja ya miradi yake hapa DSM akitaka ushauri.

Nitamkumbuka sana kama rafikiye na baba yangu!
 
Back
Top Bottom