Mbona wa diploma husoma form six pia.Mwalimu wa Diploma anakuaje deep helezea hapo kwanza
Anasoma miaka 2 tu Chuo wakati wa degree miaka 3 plus form six yake.
Naomba nikuambie katika ualimu kinachofundishwa chuoni ni pedagogy skills mostly na few courses kwa teaching subjects.
Pedagogy skills wanasomea wote.(dipl na degree)
Management skills wanasomea wote
Teaching subjects courses na methodology wanasomea wote.
So hoja Yako ya mwalimu wa Diploma Yuko deep Haina mashiko mkuu(kwa heshima zote)
Labda nipe point zingine nitakuelewa.
Tuko pamoja, ila lazima ujue unataka elimu ya Nini kwa watu gani. Siyo ku copy copy kutoka Ulaya. Haingii akili eti mtu aliesoma BA/BSC with education ukampeleka primary akafundishe darasa la kwanza, pili, tatu au nne. Hayo ni matumizi mabaya ya rasilimali watu na uharibifu wa elimu.Ni kama unataka mambo yabaki vile vile kama zamani lakini hayana tena impact kwa Sasa Hali halisi ilivyo.
Unataka watu waliofeli ndio wabaki kufundisha huko mashuleni.
Mabadiliko haya ya Sasa kwa walimu na kiwango Cha taaluma zao ni step stone kuelekea kupandisha hadhi ya elimu yetu kiubora na maslahi ya walimu.
Achana na fikra za zamani sijui ilikuwa vipi au vile wote tumesoma huko zamani ila kwa mahitaji ya Sasa ya Dunia na mwamkonwa mabadiliko ya sayansi na teknolojia tunahitaji walimu wasomi kwa level zote.
Hii itawasaidia hata waajiri wao waone aibu wawalipe vizuri kama kada zingine.
Tatizo hata maoni yamekusanywa kwa watu km huyo hapo juu. Watoa maoni walikuwa wengi na wengi wao waliongea tu bila kujua wanaongea Nini km huyo hapo juu.Mbona wa diploma husoma form six pia.
Na hili mkalitizame upyaUtekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 na mitaala ya elimu toleo la 2023 utaanza kwa awamu mwakani, huku walimu watakaofundisha shule ya msingi wakipaswa kuwa na stashahada ya ualimu.
Walimu na Wadai wa Elimu endeleeni kutoa maoni ya Sera Mpya ya Elimu,mchakato unaendelea kabla ya kuja na final.
Akiwasilisha rasimu za sera na mitaala hiyo kwenye semina ya wabunge jijini hapo, Kamishna wa Elimu Tanzania, Dk. Lyabwene Mtahabwa, alisema katika mapendekezo ya rasimu hizo, walimu watakaofundisha elimu ya msingi itakuwa lazima wawe na stashahada ya ualimu baada ya kumaliza kidato cha sita.
Alisema kwa watakaofundisha elimu ya sekondari, ni lazima wawe na shahada ya ualimu, hivyo walimu waliopo kazini ambao hawatokuwa na sifa hawataondolewa kwenye ajira bali watapewa fursa ya kujiendeleza ili kufikia viwango.
Akitoa ufafanuzi kwa wabunge, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, alisema hakutokuwa na mtihani wa kumaliza elimu ya msingi badala yake kutakuwa na mtihani wa upimaji, ili kuendelea na elimu ya sekondari ngazi ya chini.
Chanzo: Nipashe
Nahisi wanatengeneza Mazingira ya upigajiHio ndio mistake kubwa wamefanya wanaongeza idadi nyingine ya walimu wenye certificate wakati wanataka kuachana na huo mfumo.
Hilo ni tatizo . Sijui wamejipangaje!?
Hapo unaongelea utendaji kazi wa kada za ufundi ni tofauti na Ualimu.walimu wa masters hawezi kujituma kama walimu wa diploma na digri wao muda mwingi mikoni mfukoni tu ndo maana makampuni mengi yaliyofanikiwa watenda kazi wazuri ni ma-technicians na artisans
Hapo ilikuwa ni baada ya kufundisha kwa mafanikio makubwa ila baadae wakaja wanasiasa km sasa wakalazimisha wajiendeleze. Si unajua Tz Kila anae shika mpini anakuwa na yake.Nakumbuka enzi ya UPE, walitakiwa wawe na cheti cha kidato cha nne. Sikumbuki walioshindwa walifanywaje!!
mwanangu mkenda na jopo lako,najua unatimu nzuri na wewe ni msomi mwanazuoni ebu lifanyieni kazi watanzania wanawategemea msiwaangusheNa hili mkalitizame upya
Vyema.Sio lazima walimo wote wa diploma waomdoke kwenda masomoni wakiiacha shule Haina walimu
Dunia imebadilika sana mkuu siku hizi.
Kuna vyuo vinatoa shahada za elimu katika njia huria na masafa( Open and distance learning)
Una Chuo kikuu huria(OUT) taasisi ya elimu ya watu wazima (IAE) huko watoa degree za
Bachelor of education
Bachelor of science
Bachelor of arts with education.
Wanaweza jiendeleza huko na wakafikia lengo.
Tena nimesikia serikali imeanza ukarabati wa teachers resources centers (maarufu kama Clasta). Ili kuwapa walimu mazingira mazuri ya kujiendeleza wakiwa ndani ya vituo vya kazi bila kuathiri ufundishaji na ujifunzaji mashuleni.
So Kila kitu kinawezakana jambo la kwanza kabisa ni attitude Yako na ya yule. Unajiset vipi kukabiliana na changes.
Km kuna ukweli vile.Serikal igharamie hzo cost za walimu kwenda soma, ila wakisema mtu akajisomeshe tena kwa mshahara ambao mtu kajaa madeni telee asee itakuwa mazingaombwe.....
Nakumbuka zamani mwajiri alikuwa akimgharamia mtumishi wake katika masomo.
Ila yote kwa yote pamoja na mabadiliko ayo ya mtaala wasisahau maslahi ya hao walimu, leo ukiulza vijana wanataka kufanya kaz wap mtu atakutajia TRA, Bandarin, airport n.k lkn hautosikia mtu akisema ataka akasomee ualim cz wanajua kuwa maslah ya ualim n duni,
Leo tumelijadili hili,mishahara ina viraka sana,hao wakujisomesha itakuaje,na je wasiposoma muafaka utakua ni upi,any way,tuendelee kuvuta mtori nyama tutazikuta chiniSerikal igharamie hzo cost za walimu kwenda soma, ila wakisema mtu akajisomeshe tena kwa mshahara ambao mtu kajaa madeni telee asee itakuwa mazingaombwe.....
Nakumbuka zamani mwajiri alikuwa akimgharamia mtumishi wake katika masomo.
Ila yote kwa yote pamoja na mabadiliko ayo ya mtaala wasisahau maslahi ya hao walimu, leo ukiulza vijana wanataka kufanya kaz wap mtu atakutajia TRA, Bandarin, airport n.k lkn hautosikia mtu akisema ataka akasomee ualim cz wanajua kuwa maslah ya ualim n duni,
Sidhani kama kulipa vimalimbizo vya walimu wetu vinavyodaiwa tangu mwaka 2017 wameshindwa wataweza kuafford gharama za kuendesha shule kwa kuzingatia sera hiyo mpyawataboresha wanasema wamejipanga
You are right, in private schools the graduates are needed only during the registration of a school. After that it is form six leavers who are cheaper and more efficient at work.Unaongea usilolijua ww ..
Private schools never prefer graduates employee...
Nenda kesho private yeyote utakuta vijana form six...fresh kabisa wanapiga kazi..
Private shida yao content bas...
Yakupasa uutazame mchakato wenyewe na usitazame mtu.....Elimu ya Tz mnawapa wanasiasa wasiojitambua that way watu hupeleka watoto wao kusoma nje
Yaani kila kichaa akipata uwaziri anakuja na Ajenda na sera Mpya kuhusu Elimu yetu ...ujinga mtupu
Watasambaza computer na walimu wake?Umeisoma sera? Yote hayo yameshughulikiwa.
Sera zilizopo hazijawahi leta tija, zina avrg implementation, binafsi sitegemei makubwa maana viongizi wetu hawana hamu ya ukweli to transform our education and life. We have mediocre leaders, hatuna exceptional leaders wanaoweza kutuvusha ktk mkwamo wa mtu mweusi.Sawa lakini lazima tuanzie somewhere, na pa kuanzia ni SERA na MITAALA then hayo mengine yatafuata mkuu...