Mtaje yeyote unayemjua pichani

Una idhini au baraka za wahusika wa kwenye hiyo picha mkuu?
 
Haruna moshi

Mmoja wa vijana waliokuwa na vipaji vikubwa nilimjua toka yupo reli morogoro sijui kwa nin vijana wetu hawadumu kwenye maisha yao ya soka
Haruna MOSHI "BOBAN" hajawahi kucheza Reli Morogoro! Alivotoka Tabora alienda Tanga - Coastal Union. Kutoka Tanga akaenda Morogoro - Moro United ya Merley Balhabou!

Akiwa Moro United, akacheza na Kaseja na Nsajigwa! Na Balhabou (mnazi wa Simba) akampeleka JKJ Simba!
 
asante kaka kitambo kumbukumbu zinaondoka

nadhani ulimboka ndo alipitia reli
 
Reli 2. Ulimboka Mwakingwe na Christopher Alex
Reli nyuma kidogo. Fikiri Magoso na Mtwa Kiwhelu
Reli: Golini Athumani Msomali (sub yake Duncan Mwamba), mbele kuna watu wa ukweli David Mihambo, Peter Mjata na Mbuyi Yondani, pembeni kulikuwa na Marehemu Duncan Butinini.... katikati kuna Boniface Njohole ama Ramadhani Kilambo! Kuna wkt Pale nyuma alikuwa anasimama Prof. Madundo Mtambo (Prof. SUA, ndiye anaewatoa wachezaji wengi wa Morogoro kupitia academy yake then Mtibwa kwenda timu za Dsm) na Habib Kondo!

Wachezaji wengi wa Reli walichezea Timu ya Taifa ya pili iliokuwa ikiitwa KAKAKUONA!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…