Mtaji si kigezo cha kuanza biashara bali bongo lako - jadili


Sifikirii kwamba lazima mtu uwe na mtaji wa pekee, ninachofikiria akili, utashi na nguvu zetu ni mtaji tosha. Fikiria ukiamua kwenda porini kuokota mzigo wa kuni na kisha kumwuzia anayezihitaji sidhani kama kuna mtaji wa pekee isipokuwa nguvu zako na matumizi yako ya kawaida nyumbani ambayo wayatumia kila siku.

Kama leo umefanikiwa kuuza mzigo wa kuni kwa fulani umeingiza cho chote mfukoni na kisha mnunuzi atawajuza majirani nao watataka kuni, hapo umeshapanua wiko wa soko licha ya mwenyewe kutafuta wateja zaidi. Mtu wa aina hiyo unafikiri hajaanza mtaji na kisha kuamua kutunza mapato yake, sitashangaa siku akifanikiwa kununua mifuko miwili ya sement na kifyatulio cha blocks na kuanza mtaji huo kiwanda cha kufyatua block za kujengea zinazohitajika kila siku. Huhitaji kuhangaika kutafuta maji ya gharama, anzisha mradi kando ya kijito wenye nazo watakufuata tu.
 
mi naona huwa tunahamasishana tu. bila mtaji haiwezekani jamani, unaanzia wapi kwanza????
 
Mkuu Candid Scope, Heshima yako.

Kuna kitabu hapa katika pdf nakiambatanisha ili kukazia mada yako, kinaitwa ''The Science of Geting Rich''. Chukueni jamani mkisome, kama kuna mwingine anahitaji vitabu vingine kama hivi aniambie nitatoa kadri ninavyopata muda.
 

Attachments


Nimekisoma na nimekipenda, very interesting!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…