Mtaji siyo tatizo kwa walio wengi, tatizo ni sisi wenyewe kutojua jinsi ya kuanza.

Mtaji siyo tatizo kwa walio wengi, tatizo ni sisi wenyewe kutojua jinsi ya kuanza.

Mr. Aweda hii ni shule kubwa na nzuri kabisa.. Umeieleza katika lugha rahisi kabisa.. Mimi nilikuwa mbishi sana na muoga wa kuanzia chini, Kisa nilihudhuria tu darasani na kupata vyeti visivyosaidia kwa mtu kujiajiri.. Nilifanya kazi, tena katika nafasi nzuri kwa miaka saba ila sikuweza kujikwamua kiuchumi zaidi ya kuwa na madeni makubwa ya magari na nyumba ambayo sikuweza kuimaliza.. Nilifanikiwa kwenda kusoma nje kwa miaka 4.. Nilikutana na watu wengi toka west africa wenye spirit ya ujasiriamali.. Niliporudi Tz sikutaka kabisa kurudi kwenye ufungwa wa kazi.. Kwa mtaji mdogo sana nilioanza nao sasa ni karibia mwaka mmoja nauona mwanga na nimeshajikomboa kwenye MTEGO WA MSHAHARA.. Mimi ndio nimewaingiza vijana sasa wanitumikie..
 
Mr. Aweda hii ni shule kubwa na nzuri kabisa.. Umeieleza katika lugha rahisi kabisa.. Mimi nilikuwa mbishi sana na muoga wa kuanzia chini, Kisa nilihudhuria tu darasani na kupata vyeti visivyosaidia kwa mtu kujiajiri.. Nilifanya kazi, tena katika nafasi nzuri kwa miaka saba ila sikuweza kujikwamua kiuchumi zaidi ya kuwa na madeni makubwa ya magari na nyumba ambayo sikuweza kuimaliza.. Nilifanikiwa kwenda kusoma nje kwa miaka 4.. Nilikutana na watu wengi toka west africa wenye spirit ya ujasiriamali.. Niliporudi Tz sikutaka kabisa kurudi kwenye ufungwa wa kazi.. Kwa mtaji mdogo sana nilioanza nao sasa ni karibia mwaka mmoja nauona mwanga na nimeshajikomboa kwenye MTEGO WA MSHAHARA.. Mimi ndio nimewaingiza vijana sasa wanitumikie..

Safi sana mkuu,
 
Kuna watu wengi sana wanaolalamika
kushindwa kuanza kufanya biashara kwa madai kwamba hawana mitaji. Ukweli
ni kwamba kwa walio wengi madai ya kutokuwa na mtaji siyo ya kweli
badala yake ukweli ni ukosefu wa elimu ya ujasiria mali.

Mfanya biashara Reginald Mengi aliwahi kusema, nami nakubaliana naye
kwamba, kama mtu hawezi kufanya biashara kwa kutumia laki 1 na
kufanikiwa hata akipwe mtaji wa Mil 100 hawezi kuibadilisha kuwa milion
150 - Haiwezekani kwa sababu Kanuni zinafanana.

Utakuta mtu ni mwl, anataka mtaji, wakati mtaji ni sebule ya nyumbani
kwake na wanafunzi watatu hadi 5 wa kuanzia.
Niliwahi kumwuliza rafiki yangu hivi ukipata mtaji wo wote unaotaka wewe
ungefanya nini? Akaniambia yafuatayo.
Nitanunua kiwanja kikubwa na kujenga shule kubwa ya sekondary yenye kila
kitu - yaani madarasa, mabweni, walimu, maabara, vitabu vyote, viwanja
nk - yaani kila kitu. Kisha nitatangaza kwa nguvu ktk vyombo vya habari.


Ukweli ni kwamba huyu rafiki yangu atafeli kwa uhakika kwa sababu, mimi
siwezi kumpeleka mwanangu kwenye shule ambayo sijui historia yake hata
kama ni kubwa namna gani - it is too risky. Lazima uanze chini kidogo
kidogo ili ujenge jina zuri ( reputation). Huyu rafiki yangu, lazima
angekwama kulipa mkopo. Kama atafanikiwa ni baada ya muda mrefu. Hapo
lazima atakuwa ameshagombana na mwenye pesa - benki.

Shule nyingi ninazofahamu mimi hapa mjini zenye majina makubwa hakuna
iliyoanza na wanafunzi 100 au zaidi kama alivyotaka rafiki yangu. Wengi
wameanza na watoto chini 10 mfano Esacs, kamene nk.

Ndugu zangu, tujifunze kuanza chini na kupanda juu taratibu. Tusitake
makubwa kuliko uwezo wetu. Biashara iko kichwani kwanza kabla haijwa
halisi ktk hali halisi.

Biashara NI lazima ianze na kila unachokijua wewe ama una uzoefu nacho
na kukipenda. Siyo kile ulichoambiwa kinalipa - hapana. kila Kitu
kinalipa, hata kuimba au kuigiza kunalipa. Hoja ni kwamba je,
unajua,unazoefu, unapenda na una uwezo kuimba au kuigiza? Na kwa kawaida
ukishazingatia hilo, mtaji hauwi tatizo kama ilivyo tatizo kwa wengi
sasa. Tatizo la wengi ni ufahamu.

Utakuta mwanasheria anatafuta mtaji wa kufungua ofisi ya huduma YA
kisheria Ubungo Plaza - Haiwezekani. Ukimwuliza nani wateja wako wa
kukuwezesha kulipa kodi na gharama zingine, Hana jibu. Kumbe alipaswa
kuanza kutoa huduma hiyo kuanzia sebulen kwake then ofisi ndogo 80,000
mitaani, kabla ya ubungo Plaza.

Utakuta mtu anataka kwenda china kuchukua mzigo wa mil 50, kabla
hajafanya biashara hiyo hiyo hapa bongo na kupata uzoefu kidogo kwa
mtaji wa milioni moja au laki 1.

Hoja yangu si kwamba mtaji siyo tatizo la hasha, hoja yangu ni kwamba
kwa walio wengi humu jf, tatizo ni ufahamu wa kutojua kitu cha kufanya
kuliko tatizo la mtaji. Wapo wachache ambao kweli wana uzoefu na uwezo
na wana matatizo la mtaji, lakini si wengi kama tunavyoona vilio vingi
hapa JF- jukwaa la uchumi na kwinginepo mtaani. Tatizo la wengi ni
ufahamu, agree or not.

Hivi unajua kwanini benki zinawanyima baadhi ya watu fedha na kuwapa
wengine. Wanataka kujua kama una uzoefu na kama umeanza chini kuja juu
au laa. Wengi hatuwaelewi watu wa benki lakini ukweli ni kwamba benki
wana nia njema na sisi. Hataki kutupa pesa nyingi kuliko uwezo na uzoefu
wetu wa kulipa. Wanajua kuliko sisi. kutunyima sisi mitaji tunayotaka
ni kutusaidia kwamba tukaanzie chini kwanza. Kumbuka benki wapo ili
kukopesha. Wanaokopa ndo faida, wanaoweka tu fedha siyo deal kwao.
Ukiona wanatunyima maana yake tunakosa uzoefu, tunaka kuanzia juu kama
rafiki hapo juu. which is wrong.

Nahitimisha kwa kusema tuwe tayari kuanza chini kidogo kwa faida yetu
kwa sababu kanuni ya kubadilisha au kufanya biashara kwa mtaji wa mil
100 kuwa mil 150 ni sawa na kanuni ya kuanzia na laki 1 na kuibadisha
kuwa laki 2 kibiashara.
Nawasilisha.

thank you
 
Mu israeli,
Hapa changamoto mbili ntakupa.
Kwanza ni karibu umetoka nje ya mada.
Mimi niko wa wajasiria mali wa chini kabisa. Mimi nataka kuwapa mbinu hawa wajasiria mali wadogo sana ambao mil moja tu anaisikia kwenye redio. Wengine mshahara ni laki moja. Jana niliongea na mtu aliyefanya kazi ya kuuuza duka la mtu miaka 9. Hajui kitu cha ufanya. Huyu ndo namwambia aanze chini kwenda juu. Hao wenye mil 20 kwenda juu ni sio wajasiriamali wadogo. Mtu ambaye benk inaweza kumpa kiasi hicho lazima ana dhamana kubwa - Amesha toka.


Pili, Huwezi u kutoka unakojua ukatafuta mil 20 ukaanza biashara ya dala dala au ukaanza kujenga nyumba za kupanga nk. Mimi nilifanya kosa hilo ktk biashara fulani likanigharimu sana.( Kumbuka natumia ID halisi,ukitaka unaweza kujua kunitembelea). Lazima ujue kwanza in and out ya biashara yo yote unayotaka kufanya. Mwekezaji tu ndo anaweza kufanya hivyo kwa sababu yeye ni pesa ndo inamfanyia kazi. Hahitaji uzoefu.

Kila kitu ni lazima tupinge! Usijali, ndio zetu JF.
 
Ila mimi napingana na Mtoa maada hapo kwenye Elimu ya Ujasirimali, Tatizo la watu wengi si Elimu bali ni Sprit ya Ujasirimali ndo watu hawana, kama huna Spirt hata Ukiwa na Phd Ya Ujasirimali ni kazi Bure, na hata hivyo Kwa Duniani hakuna Chuo kinacho weza kumfanya mtu akawa Mjasiromali bali kuna Vuo vya Kufundisha Business skills kama Marketing, Business palning, Customer care na kazalika,

Hakuna Chuo cha Kufundisham Commitment, Inovation, Risk taking, Uvumilivu, na zinginezo, that is wahy ni vigumu kufundisha mtu Ujasirimali, unaweza mfundisha kufanya biashara lakini si Entrprenership.

Na pamoja na kwamba kuna Born and Made Entrpreners, Lakini hata Made Entrepreners lazima anakuwa na spriti ya Entrprenership, watu kama wakina Dell, Thomas Edson, Honda na wengineo ni BORN kwa sababu hawa kujifunza popote pale,

Tanzania inatakiwa elimu ya Biashara itolewe kwa Rough Diomond, kuna watu ambao ukiwaona ni sawa na Alumasi ambayo haijasafishwa na ukiisafisha tu inakuwa rear Diaomond, na kosa linalo fanyika ni kwenda kutoa elimu ya Biashara bila kujalisha huyu ana muelekeao wa ujasirimali au la,

So ni lazima Tujue kwamba Ujasirimali ni zaidi ya Elimu, Huhitaji elimu ya aina yoyote ile wewe kuwa mjasirimali,ila unahitaji elimu ya biashara ili ufanye biashara, Ila kuwa mjasirimali huhitaji chochote kile,

Hakuna kitu ambacho mtu nahitaji ili awe mjasirimali, si pesa wala si nini, na wala huhitaji program za Serikali ili uwe Entrepreners, Unahitaji tum kuwa na Spirit ya Ujasirimali basi na si kingine kile

Nazani wakuu mtakua mmenipata vyema

Thank you. Umeeleweka vizuru sana.
 
Na kwa kuongezea Mkuu

Kwa hapa Tanzania Kuna Tatizo kubwa sana katika swala zima la Kuhamasisha Ujasirimali, Tofauti na Mataifa Mengine hata ya Africa, Ulaya, na Asia, Nchi kama China kwa sasa Entreprenership iko juu sana kutokana na Mwamko, India ndo kabisa Spriti iko juu mno,

Kwa Tanzania tuna kwaza na vitu vifutavo

1. Mfumo wa Uchumi wetu zamani- UJAMAA
Ujamaa ni mbaya sana katika swala zima la kujenga Entreprenership, na Mataifa kama Urusi kwa sasa wanapata shida sana, na China sema ilishutuka mapema inagwa hata wao wana matatizo na wawekezaji wengi walioko China wametokea JAPAN,KOREA, USA NA ULAYA
'Ujamaa hautoi nafasi kwa ukuwaji wa Ujasirimali na hii ni kutokana na serikali kufnya kila kitu,

2. MAZINGIRA
Vijana wengi mazingira walio kuria haya hamasishi ujasirimali kabisa, Tukiwa watoto Wazazi wetu walikuwa ni Wafanya kazi, Ndugu zetu wengi ni wafanya kazi, Majirani ni wafanya kazi, so tumekuwa tukishuhudia Wazazi wakija kuchukuliwa na Magari ya Ofisi, tukawa na sisi tunatamnai kuwa kama wao

Baba anaenda safari na Gari la Ofisi akirudi anakuja na Mizigo kibao iliyo bebwa kwenye hilo gari kama Mkaa, na kazalika, tukawa tunatamnai, Wazazi wanaleta baadhi ya Vitu vya kazini kwao tukawa na sisi tunatamnai sana

Majinari wote ni wafanya kazi na tunatamani kuwa kama wao

Ndugu wote ni wafanya kazi na tunatamani kuwa kama wao

Cheki watoto wa Kihindi- baba mfanya baisahara, Mama mfanya biashara, Majirani wafanya biashara, Marafiki wafanya biashara, wajomba wafanya biashara, hapa usitegemee watoto waje kuwa wafanya kazi NEVER

3. MAKUZI KUTOKA KWA WAZAZI
Haya yanachangia asilimia zaidi ya 50 katika kuondoa hari ya Ujasirimali nchini, Tumekuwa tukikuzwa na kuambiwa inatakiwa tusome tuje kuwa Mameneja, Wakurugenzi, tufanya kazi Benki na kazalika, hii inajengeka kichwani mwa Mtoto anaenda Shule akiamini anatakiwa asome aje kuwa Meneja

KWA STAILI HII NI LAZIMA KIJANA AWE NA HARI YA KUTAFUTA KAZI NA SIO KUJIAJIRI

5. MASHULENI
Hapa ni kama wazazi, nako walimu story ni za kiajiriwa tu na hata wano tufundisha wameajiriwa so ni kwa nini sisi tujiajiri

6. MFUMO WA ELIMU
Ingawa si kwa sana, but hata mfumo wa elimu yetu unatufanya tuogope biashara sana, Elimu ya Kukaririshana, Elimu ya Kusoma Handout, Elimu ya kusomea siku ya paper, Elimu ya Kusoma Mapast paper mwanzo mwisho,

Hizi aina za kusoma kwa kweli zinaondoa udadisi, zinatufanya tuwe tegemezi zaidi na zaidi


7. SERIKALI YETU KUKOSA UHAMASISHAJI
Nchi nyingi Duniani zaina vitu vya kuvutia Vijana kuwa wajasirimali ikiwemo Mikopo au Grants za kuanzishia biashara, na Nchi kama India vyuo vikuu vyao vingi vijana wanao jiajiri ni wengi kuliko wanao enda mtaani kutafuta kazi, sasa njoo Bongo nenda hata SUA uone 99% ya wanachuo wanataka waajiriwe


8. MFUMO WA WATANZANIA
Nchi kama Kenya au Nigeria na kwingineko hari ya Kujiajiri iko juu sana kutokana na Mfumo wa Maisha yao, Nchi kama Kenya Maisha ni Magumu sana na hakuna Ndugu wa kukusaidia, hakuna Pesa ya Bure, hakuna cha Shangazi, Mjomba, shemeji wala nini, kwa staili hii kijana ni lazima akomae make no way out,

Nchi kama Nigeria maisha ni magumu sana na ndo maana vijana wanakuwa hadi matapeli wa kimataifa ni kutokana na kwamba hakuna wa kumsaidia,

TANZANIA, Huku maisha ni rahisi sana, mtu ukiona hakieleweki unaibuka Kwa shemeji unaishi hata miaka mitano kule na unakula na kulala bure, ni kwa nini uhangaike wakatiu unakula na kulala Bure? Ukiwa nyumbani kwenu ndo kabisa unaweza Oa na ukaleta mke nyumbani kwenu na Baba na Mama wakawa wanawahudumia bila tatizo kabisa, so ni kwa nini uhangaike wakati kwenu hujafukuzwa?

Ukiona vipi unajichanganya kwa Baba mdogo, Shangazi, Mjomba, Kaka, Binamu, Bibi, Babu, kwa BABA WA UBATIZO na kazalika,

Kwa wenzetu hakuna kitu kama hicho hapo Kenya hakuna mambo kama haya, so kijana ni lazima hata akimaliza Chuo kikuu awe mpiga DEBE make hana njia nyingine ya kushi, hakuna wa kumsaidi

SO HAYA MAMBO YA KUENDEKEZANA YANALEMAZA SANA TENA MNO, NA YANAFANYA VIJNA WAWE DEPENDANT
 
Hii ndio elimu kwa njia ya mtandao, sio mpaka cheti ndio ujue umefuzu!
Na hii tabia ya kudai huna mtaji wakati mtaji mkubwa na wa muhimu ni uzoefu wa kile unachotaka kwenda kufanya. Ndio maana mabenki wako rahisi sana kumpa mtu mkopo kwa mara ya pili na ya tatu kwani rekodi yake inamlinda, na rekodi ni nini? Ni ule uzoefu wako usiotiliwa mashaka. Tujizoeze kwanza wadau.
 
mkuu nakushauri uanzishe ofisi ya ushauri juu ya masuala ya ujasiriamali. ukianzisha ni-pm nitakuwa mteja wako!
 
mkuu nakushauri uanzishe ofisi ya ushauri juu ya masuala ya ujasiriamali. ukianzisha ni-pm nitakuwa mteja wako!

Consultance business hapa Tanzania Ni ngumu sana, jamaa haijaamka kabisa, mtu akisha ona ana duka na wateja wanakuja kila siku yeye ni basi, Hizi biashara zinalipa sana huko kwa wenzetu, ila sio Tanzania, niliwahi kuifanya huku Arusha kwa kweli ni shida jamii yetu bado sana katika swla zima la Ushauri wa Biashara, wanataka uwashauri bure,
 
Consultance business hapa Tanzania Ni ngumu sana, jamaa haijaamka kabisa, mtu akisha ona ana duka na wateja wanakuja kila siku yeye ni basi, Hizi biashara zinalipa sana huko kwa wenzetu, ila sio Tanzania, niliwahi kuifanya huku Arusha kwa kweli ni shida jamii yetu bado sana katika swla zima la Ushauri wa Biashara, wanataka uwashauri bure,
ni kweli sisi watanzania hatujajua umuhimu wa kupata ushauri elekezi kuhusu masuala ya biashara na miradi. ndio maana ukifanya utafiti utabaini kuwa watanzania tunabadiri aina ya biashara kila baada ya kipindi kifupi na pia watu wengi wanafunga biashara zao kwa kushindwa kuziendeleza! halafu hapo penye red: ushauri wa bure ni jambo lisilowezekana hata kama ni hapa TZ. siku hizi baadhi ya maeneo hasa DSM imeanza biashara ya kuelekezwa mitaa au ofisi kwa kutoza pesa!
 
ni kweli sisi watanzania hatujajua umuhimu wa kupata ushauri elekezi kuhusu masuala ya biashara na miradi. ndio maana ukifanya utafiti utabaini kuwa watanzania tunabadiri aina ya biashara kila baada ya kipindi kifupi na pia watu wengi wanafunga biashara zao kwa kushindwa kuziendeleza! halafu hapo penye red: ushauri wa bure ni jambo lisilowezekana hata kama ni hapa TZ. siku hizi baadhi ya maeneo hasa DSM imeanza biashara ya kuelekezwa mitaa au ofisi kwa kutoza pesa!

Ndo hivyo watanzani wanashindwa kuelewa kwamba hata Makampuni kama VODACOM, TIGO, NA HATA MAKAMPUNI YA MADINI NA HATA YA BIA KAMA TBL pamoja na kwamba ni the reading lakini still wana Consulance firm ambayo kazi yao ni kuwashauri maswala ya masoko, uzalishaji, ushindani na kazalika,

Kwa kifupi Wabongo ni Pasua Kichwa kabisa, Mimi nilisha wahi kukonduct Semina ya kuwapa watu elimu ya Biashara hasa katika Masoko, Ushindani, maswala ya mitaji na kazalika, Cha kusikitisha wale watu waliniuliza kama Kuna Posho, yaani nijitolee and then niwalipe Posho, Tangu siku hiyo niliapa kuto fanya ujinga kama huo kamwe, Ila time is coming amapo watu watakuja kujua hayo mambo,

MWatanzani tunataka tupewe Elimu na Tulipwe, nakumbuka hata NGO Moja ambalo nilikuwa na fanya nalo kazi, tulikuwa tunatoa elimu kwa wakulima huko Bushi sasa ikifika kipindi cha semina, ingawa semina ilikuwa inafanyikia kwenye maeneo yao, wao walikuwa wakiomba Posho na kama hakuna Posho hawaji, Kuna mzungu mmoja ambaye ndo walikuwa wafadhili, baada ya kujionea kwa Macho yake, alimuru muradi ufungwe mara moja na kuapa kuto saidia kamwe,
 
Nakubaliana kabisa na wewe. Kwa kuongezea tu, ningependa kuongelea suala la vijana wengi kushindwa kufanikiwa kwa kuanzia chini kupanda juu. Sababu zifuatazo zinachangia vijana kutaka kuanza biashara kwa milioni 50, 100, 150 n.k kitu ambacho ni ndoto za alinacha:

1. Kwa sasa tunaishi katia ulimwengu wa material world kwa maana ya kwamba, mtu unaheshimika ukiwa na pesa nyingi. Hii inawapa presha sana vijana kufikiria kuanza biashara kwa mitaji mikubwa. Zamani mtu alikuwa anaheshimika kwa busara na mchango wake katika jamii. Hii ilifanya wengi wafanikiwe kwa sababu heshima wanayoihitaji wanayo so wana concentrate kukuza biashara. Siku hizi watu wanaoheshimika ni mapedeshee wanaoimbwa kwenye miziki wakati wazee wenye busara zao wamesahaulika

2. Vijana wengi wa siku hizi hawajiamini na hawana uwezo wa kufikiri kivyao. Vijana wengi siku hizi ni waoga wa kufanya mambo kutokana na woga wa kufikiria watu wengine watawafikiriaje wakiwaona wanafanya biashara ndogondogo. Hii inatokana na malezi tunayopata ambayo hayasaidii kupandisha morali na kujiamini kwa watoto wa kitanzania.

3. Ukosefu wa elimu ya biashara. Watu wengi wanaopenda kupata faida za haraka haraka hawajui kwamba ukiwa na elimu ya biashara itakusaidia kupata yote hayo badala ya kuiba, kwenda kwa waganga wala kuua watu. Ukiwa na elimu ya biashara itakusaidia kujua jinsi gani ya kuvutia wateja na kukuza biashara fasta.

Nasema haya yote kwasababu mimi mzazi wangu ameshawahi kushika nafasi kubwa kiaina serikalini, so mimi tokea mdogo ninaona mashangingi yakimchukua na kumpeleka kzini na pia kuishi kwenye nyumba za kifahari za serikali. So akili yangu ilikuwa ni kuanza biashara kwa milioni 100 ili kuweza kuishi lifestyle kama hiyo. But nilipoenda kusomea bishara ndo nikagundua kwamba hata nikiwa na 500,000 naweza ikuza na ikanipa yote hayo. Ni ishu ya kupata elimu na kuchange mindset kiaina.
 
Uko sahihi sana mkuu, hata mimi mwenyewe najishangaa kwani najiuliza ninaweza kufanya biashara gani, nimekuja kugundua kuwa mtaji ninao ila wazo la biashara ndo sina, japo mtaji si mkubwa (ni mdogo sana lakini ninawafahamu watu wengi ambao wan biashara zenye mtaji mdogo zaid ya mtaji wangu.
Kweli umesema sawa jambo kubwa ni kuwa na elimu ya ujasiriamali.
Ahsante sana ndugu yangu
 
Samahani kwa kutofautiana kidogo,kwa mtazamo nilionao nafikiri kitu kikubwa kabisa kinachotushinda ni ule uthubutu/Nia wa/ya kufanya maamuzi kwa kuogopa changamoto zilizopo.Mawazo yetu labda yanakuwa yanafikiri eti biashara ni kama mchezo wa kamali ya kubahatisha,na wakati mwingine ni kweli kotokana na aina ya biashara husika.

Hivyo basi tuliowengi tunaogopa kuingia katika majanga yaliyo katika biashara,ambayo wakati mwingine ni hatari sana kibiashara na kwa mhusika mwenyewe.
 
Back
Top Bottom