Mtaji wa milioni saba

golden pride

JF-Expert Member
Joined
Oct 24, 2014
Posts
847
Reaction score
435
Wakuu habari zenu,
Mi ni muajiriwa wa kampuni binafsi.Nataka niache kazi nijikite kwenye biashara, ila mtaji wangu ni milioni saba.Naomba ushauri wenu, ni biashara gani naweza kufanya, na mchanganuo wake upoje.
Nawasilisha
 
Naona ukishindwa vibaya kibiashara. Huwa inaanza business idea, then unasaka mtaji. Kuanza na mtaji then business idea ni sawa na ndoa iliyofungwa sababu mmepeana mimba bila utashi wa kuishi pamoja, ni mojawapo ya sababu za kushindwa, utarukia kitu chochote mradi una hela.

Tunza hiyo hela yako kwanza bank, endelea na kazi kwa muda kwanza hadi ujipange.

Jinsi ya kufanya.
Anza kuorodhesha kila idea ya kibiashara unayoipata, hata zifike 10 sawa tu.
Anza kuangalia viability kwa kila moja
Linganisha viablility ya biashara na mtaji wako
Chagua most realistic idea.
 
Wakuu habari zenu,
Mi ni muajiriwa wa kampuni binafsi.Nataka niache kazi nijikite kwenye biashara, ila mtaji wangu ni milioni saba.Naomba ushauri wenu, ni biashara gani naweza kufanya, na mchanganuo wake upoje.
Nawasilisha
Angalia hapo kwa juu kuna sticky kibao zina ideas nyingi za biashara.Isitoshe katika jukwaa hili kuna watu kibao washapost thread zenye maswali ka lao.Usiwe mvivu.Anza kusoma mwanzo mwisho wa post za jukwaa hili nina uhakika utatoka na kitu
 
Tumia hiyo Milion Saba kufungua biashara ambayo utakuwa unaipenda na unaiweza kuisimamia hata ukiwa kazini.
Chukua mkopo benki kupitia mgongo wa kazi yako,namaanisha utakuwa ukikatwa kwenye mshahara kuza biashara yako...,ukiona biashara yako imesimama freshi na umesort deni lote la benki hapo then utaweza ku-shit hiyo kazi unayofanya.

Usiwe na Haraka Mkuu mambo mazuri hayaitaji haraka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…