Mtaji wa Sh. Mil 5 unafaa kwa biashara gani?

 
hiyo ni kweli kabisa. Tujifunze kuwa na idea mpya ili tutamaniwe siyo kutamani. Kaka hapo juu umenikuna.....


tunataka wajasiriamali wenye financial stability kama kina Aliko Dangote, sasa bodaboda sioni kama kuna nafasi ya kukua zaidi ya kupata hela ya kula tu.
 
hiyo ni kweli kabisa. Tujifunze kuwa na idea mpya ili tutamaniwe siyo kutamani. Kaka hapo juu umenikuna.....


tunataka wajasiriamali wenye financial stability kama kina Aliko Dangote, sasa bodaboda sioni kama kuna nafasi ya kukua zaidi ya kupata hela ya kula tu.
 
Nenda Kerege. Kamata ekari za shamba. Miaka miwili unauza mara tatu ya bei uliyonunulia.
 
Kama upo Dar nakushauri tafuta sehemu karibu na kituo cha daladala fungua TiGO-Pesa, Airtel Money,Voda M-Pesa..uza na vocha tena siku hizi unapitishiwa vocha na mawakala jioni wanapitia pesa yao.
 
Nunua bodaboda 3 wape vijana boda moja kwa siku ni tsh 6000 mara 3=18000, ndani ya miaka miwili utakua umetengeneza faida ya m 7.

Sikushauri boda boda! Too risk, hao unaowakabidhi pikipiki ni wehu hawana roho ya uthamini mali ya mmiliki. Try something else.
 
Vipi duka la spare za bajaj au hata boda boda - hapa itategemea location mkubwa. Mtaji ukikua unakuza biznez.
 
nipo tabata Segerea. nadhani hii ya boda boda itakuwa nzuri.

Sikushauri ununue bodaboda. utapata presha bure. nimeshaifanya inausumbufu sana. Nenda kibaigwa nunua alizeti kwa sasa gunia ni elfu 35 , kaifadhi kwenye mashine za kukamulia ,kaa miezi mi4 uza gunia kwa elfu 55. Ushauri zaidi ni pm
 

Umenena vyema, waTZ wengi wavivu wa kufikiri.....wenzetu marekani watu wana idea za kwenda kujenga hotel na kuanzisha mashamba kwenye space....sisi tunashindwa kufikiri biashara ambazo zingeweza kutatua matatizo yanayotuzunguka, boda boda sio biashara, hiyo ni biashara ya wachina. leo hii tunakimbilia boda boda kwa kuwa wachina wameumiza vichwa katika kutafuta njia za kurahisisha usafiri, na wao walifocus kwenye shida iliyopo Africa na sisi tunapaswa kufocus kwenye shida zilizopo katika vijiji vyetu na hata maeneo ya mjini.

Ushauri wangu wa biashara kwako - Loy; tumia 1 milioni kutembea mikoa mbalimbali tanzania ukirudi kwako utapata wazo la biashara. sasa mtu amekaa dar tu halafu anauliza wazo la biashara.......!!!! unafikiri watu wanpokuja kutalii wanakuja kustarehe.....wanaelewa nini maana ya kutembea, akirudi kwao amepata wazo la biashara, utashangaa anakuja kuwekeza kwenu.
 
mtu kasema ni mwanafunzi unamwambia azunguke tanzania huu ni ushauri au matope?
 
Mimi ni mdada miaka 26 elimu yangu ni form six nilikua nafanya kazi ktk kampuni moja jijini dar ila sasa nimeacha kutokana na mambo tu ya kazini. Niko rombo kilimanjaro naomba mnipe wazo la kufanya na hiyo milion tano. Niko tayari kufanya biashara kati ya dar au rombo cose kote nina sehemu ya kukaa bila kulipa kodi. Ushauri tafadhali
 
Mjasiriamali Wa kweli hawezi uliza swali Kama hili, wazo la biashara hutangulia kabla a fedha, kuna watu Wengi sana ambao akipata hata Laki moja in mind Anakuwa anajua exactly atakachofanya!

Ni kweli kabisa , lakini sio wajasiliamali tu wanaopaswa kufanya biashara ? na wafanyabiashara(waliofanikisha) sio wote ni wajasiriamali, na pia sio wajasiliamali wota lazima wafanikiwe ? jifunze GETs General Enterprising Tendecies

Unawe kujitambua kama wewe ni mjasiriamali au sio kwa kujipima hapa http://get2test.net/test/index.htm
 
mkuu nipe mimi then kila mwezi nikuletee laki tatu au unasemaje ? km imekaa vzr niambie the tupange jinsi ya kuonana na uone ofisi yangu na biashara yangu.... imetulia
 
Da utaniua kwa kucheka sana,ila inasikitisha sana na comment yako ni very challenging
 
True ndio maana hili kuavoid kutosa tosa madereva bora upate kijana muaminfu ili mambo yaende vizuri.

Uaminifu unatakiwa sana. Vijana wengi wakikabidhiwa biashara wanajiangalia wao tu. Wanapata hesabu ya siku ila kwa tajiri wanapeleka hadithi tupu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…