Mtaji wa tzs milioni 10 biashara kwa wale walio busy sana yenye faida ya tzs 1.5m

Mtaji wa tzs milioni 10 biashara kwa wale walio busy sana yenye faida ya tzs 1.5m

miamiatz

JF-Expert Member
Joined
Dec 4, 2017
Posts
505
Reaction score
941
A friend of mine aliguswa na makala yangu ya biashara ya nafaka kwa wenye mtaji mdogo. Alipoguswa akaamua kuingia kwa akiba yake ya TZS 10M aliyokuwa nayo benki.

Akanunua gunia 300 kwa wastani wa TZS 30,000 kwa gunia. Alitumia TZS 1M kwenye madawa na usafiri. Alikuwa na room aliyoiita ya wageni pale home kwake japo room hiyo ilikuwa ikipata wageni mara chache sana.

Aliigeuza room hiyo kuwa store ya mahindi aliyonunua. Mengine akayaweka kichumba kilichoitwa store na mengine akayajengea kisehemu cha kuhifadhia ndani ya fence ya nyumba aliyopanga.

Alinunua baada ya mavuno July mwaka jana 2019 na miezi sita ikapita wiki iliyopita alienda sokoni na akuliza bei ya mahindi na kuomba kusupply gunia 300. Bei ya rejareja ilifika TZS 750 kwa kilo. Bei ya jumla akauza TZS 650 kwa kilo.

Jamaa akajipatia TZS 19.5M ikiwa ni TZS 9.5M zaidi ya pesa aliyotumia kununua yale mahindi. Anasema faida yake anahesabu hiyo TZS 9M mana kuna matumizi tumizi yalimbidi kulipia pale sokoni japo haikufika TZS 500,000.

Ongezeko la TZS 9M ni sawa na wastani wa ongezeko la TZS 1.5M kwa mwezi. Sio wote tufanye hii ila kwa wale wachache hata kama una TZS 30M we nunua gunia zako 1000 July ijayo Mungu hamtupi mja wake. Penye jitihada ndipo penye mafanikio.
 
Hivi ilitokea ajali ya moto hapo home inakuwaje? Una bima?

Wizi na uporaji? Gharama za usafiri kutoka kwa wakulima hadi nyumbani halafu tena kupeleka sokoni.

Ni heri kwenda kuhifadhi kwenye godowns zenye bima kwa ajili ya usalama na probably kupunguza gharama ya usafirishaji maana hizo godowns nyingi zipo mashineni ambako wanunuzi wanapatikana muda wote.

NB: Hii biashara nimefanya for years japokuwa ni mpunga lakini kwa sasa huwezi kumkuta mfanyabiashara serious kaweka gunia 300 ndani kwake we did back in 90s.
 
Mkumbuke.
Social risks,Environmental risks,Economic risks nk nk..
Pia Expectations na Reality hua ni tofauti
 
Aisee.
tapatalk_1579515466813.jpeg


dodge
 
Duh, hakuna biashara isiyo na risk ndugu yangu

Sent using Jamii Forums mobile app
Najua,lakini kama mtu upo serious kweli gunia 300 ni nyingi mno kuziweka home kwenye risk kubwa.

Weka hata godown za mashineni wana bima na kama ni mpunga hawakutozi hata storage isipokuwa unatakiwa ukobolee mashineni kwao na pumba uwaachie
 
Kwa mawazo hayo mjomba,sahau maendelleoo
Mambo ya kuficha mazao nyumbani tena gunia 300 yamepitwa wakati.

Hizo risk zingine siyo uthubutu bali ni uzembe tu.

Kwa sasa hata vijijini ziada ya chakula hawaweki nyumbani itakuwa gunia 300!
 
  • Thanks
Reactions: amu
miamiatz,
Ki ukweli kwa mwaka jana watu kwenye mahindi walilamba dume kwa walio jitoa muhanga kwani ni miaka mingi sana wamekuwa wanalia!!!! Sometimes lazima mjasiriamali uwe risk taker,!!! Ila msimu uliopita kuna factors ambazo zilifanya hali hii kutokea, hasa ni ukame uliokumba sehemu kubwa ya nchi, hada kanda ya ziwa!!
 
miamiatz, KakA,baadh ya watu wa jf ni was.enge sana ,usitegemee hata sku1 wanaweza sapoti mambo chanya,mfano hapo umetoa mchanganuo ila watu wanakuja na critics za ajab ajab,sasa unajiuliza,tukae tuu tusifanye mrad wowote,mtu anasema nyumba kuungua..mf..nyumba inaunguaje,bas asiwe analala humo kuogopa paa kumwangukia or kuungua..non sense,..na mtu anakomaa kabisa kutoa critics,...mim nawaitaga hawa jamaa wa hvo ni maskiniii.

Mim nina ekari 20 hapo bagamoyo mwaka huu nalima mahind na natarajia kuhifadh baada ya mavuno.ila umenipa wazo la faida pia kua naweza pia nunua,...m10 kitu gan bwana,et nyumba kuungua,mbona huofii kuungua familia,st.upid,..mim nitafanya hii kitu uliyosugest hapa
 
Mambo ya kuficha mazao nyumbani tena gunia 300 yamepitwa wakati.

Hizo risk zingine siyo uthubutu bali ni uzembe tu.

Kwa sasa hata vijijini ziada ya chakula hawaweki nyumbani itakuwa gunia 300!
Nipe sabab za kutoweka nyumban kama una mahala pakuweka,..usinambie et kuungua...maana kama unahofia kuungua nyumba bas uhofie pia kuzaa watoto na kuoa mke uish nae nyumban sabab wanaweza ungua ndan ya nyumba...nonsense
 
Najua,lakini kama mtu upo serious kweli gunia 300 ni nyingi mno kuziweka home kwenye risk kubwa.

Weka hata godown za mashineni wana bima na kama ni mpunga hawakutozi hata storage isipokuwa unatakiwa ukobolee mashineni kwao na pumba uwaachie
Biashara nyingi za kibongo ni kuomba mungu tu zinafanyika kimazoea tu, nenda katavi huko uone ni ma ghara mangapi yenye bima!! Hakuna, unakuta ghara(mashine) imehifadhi zaidi ya gunia 50000,lakini hakuna bima!! Ni kuomba mungu tu, na huna hata risiti ya kuhifadhiwa mzigo wako humo, zaidi ya mwenye mashine ameandika kwenye counter book lake!!!
 
Nipe sabab za kutoweka nyumban kama una mahala pakuweka,..usinambie et kuungua...maana kama unahofia kuungua nyumba bas uhofie pia kuzaa watoto na kuoa mke uish nae nyumban sabab wanaweza ungua ndan ya nyumba...nonsense
Una reasoning ya kijinga mno.
 
Hivi ilitokea ajali ya moto hapo home inakuwaje?
Kwa mawazo haya mkuu, utatafuta mchawi wa maendeleo yako kumbe ni wewe!!!! Ndio maana wengi waliofanikiwa ktk ujasiriamali ni wale hata shule hawakwenda/hawakufika mbali, wao risk sio inshu, lakini nyie ma prof. Utachukua calculator fomula nyingi, risk assessment,*fire/floods=project not viable
 
Kwa mawazo haya mkuu, utatafuta mchawi wa maendeleo yako kumbe ni wewe!!!! Ndio maana wengi waliofanikiwa ktk ujasiriamali ni wale hata shule hawakwenda/hawakufika mbali, wao risk sio inshu, lakini nyie ma prof. Utachukua calculator fomula nyingi, risk assessment,*fire/floods=project not viable
Tatizo watu mnachanganya kati ya ku-take RISK na UZEMBE.

Hivi mbona pesa mnapeleka benk ilhali mna mabegi nyumbani? Si mziweke tu nyumbani kama biashara ni ku-take risk.
 
Kwa mawazo haya mkuu, utatafuta mchawi wa maendeleo yako kumbe ni wewe!!!! Ndio maana wengi waliofanikiwa ktk ujasiriamali ni wale hata shule hawakwenda/hawakufika mbali, wao risk sio inshu, lakini nyie ma prof. Utachukua calculator fomula nyingi, risk assessment,*fire/floods=project not viable
Bro watu wa namna hii weng ni hohehahe.achana nao wala hata usimjib comment yake atakukera tuu...ni sawa mtu aogope kumtia mimba mwanamke sabab anaweza kufa in process of givin birth.non sense...ila nimemwambia mtoa mada asikatishwe tamaa na watu kama hawa wala asiwajibu
 
KakA,baadh ya watu wa jf ni was.enge sana ,usitegemee hata sku1 wanaweza sapoti mambo chanya,mfano hapo umetoa mchanganuo ila watu wanakuja na critics za ajab ajab,sasa unajiuliza,tukae tuu tusifanye mrad wowote,mtu anasema nyumba kuungua..mf..nyumba inaunguaje,bas asiwe analala humo kuogopa paa kumwangukia or kuungua..non sense,..na mtu anakomaa kabisa kutoa critics,...mim nawaitaga hawa jamaa wa hvo ni maskiniii.

Mim nina ekari 20 hapo bagamoyo mwaka huu nalima mahind na natarajia kuhifadh baada ya mavuno.ila umenipa wazo la faida pia kua naweza pia nunua,...m10 kitu gan bwana,et nyumba kuungua,mbona huofii kuungua familia,st.upid,..mim nitafanya hii kitu uliyosugest hapa
Haa haa! Mtu anasema anaogopa kuweka sh mil 10 ndani ''eti nyumba ikiungua je?'' wakati analala huko yeye, mke na watoto kila siku na hajawahi kuogopa kulala ndani kwa sababu ya moto!
 
Back
Top Bottom