Mtanganyika wa kwanza kuhutubia UN

Mtanganyika wa kwanza kuhutubia UN

kuna mengi yamefichwa kuhusu historia ya nchi hii,sijui makusudi au bahati mbaya??!!!
 
Kuna kitabu kinaitwa 'Mzozo wa ardhi ya WaMeru' kina maelezo kamili ila nilikisoma miaka ya 1970 sijui kitakuwa kinapatikana wapi kwa sasa jamani.
Ni kitabu kilichoandikwa na ndugu Mbise au nani mkuu ?
 
Kimeandikwa na mwenyewe Hayati Kirilo Japhet kimeeleza mambo mengi hata kuhusu tiketi ya ndege kwenda New York kuwa ililipwa na Mangi Mareale kama kumbukumbu zangu zipo sahihi
 
Historia nzuri sana vipi inafundshwa kwenye shule zetu hii historia
Unataka kuanzisha balaa kama analilokutana nalo Mohamed Said. Kwa ujumla historia ya Tanzania ina mengi ambayo hatufundishwi mashuleni.
 
Kimeandikwa na mwenyewe Hayati Kirilo Japhet kimeeleza mambo mengi hata kuhusu tiketi ya ndege kwenda New York kuwa ililipwa na Mangi Mareale kama kumbukumbu zangu zipo sahihi
Aisee si ajabu hicho kitabu kilishakatazwa na kilishachomwa moto..
 
Sina uhakika ila kwa kipindi hicho kama chapisho lolote lina mushkeli lisingeweza kusomwa.Kilikuwa kitabu cha kupinga ubepari na ukabaila
 
Ngoja na Mimi nidai uhuru wa wilaya ya Kino
 
Kitambo nlipata kujuzwa kuwa kuna mtanzania mmoja kutoka jamii moja iliyoko Kaskazini mwa Tanzania alienda mpaka Umoja wa mataifa(UN) kudai uhuru wa Eneo lake alilotoka na sio Uhuru wa Tanzania Nzima.
Ni ya kweli hayo? mwenye historia juu ya jambo hili Atujuze basi.
Bryan,
Utangulizi

oP5SVymLNxNKt5dhab_v_nz2eU7DYEJYLlm7CpVl5rtKi8Qy2JpOmSdMX5p_O43cbCCzlhcyfZ510BiatD-PEnRrXOtACJKy7uWd1s_4nQWB9YZx2NObH9-0AvNkT-eG7Dz5zAHBqmRgdmdPPeVggomHwPQTvBrR1PoxtBE_uF3VpFfGKlCyi6o-QZD_LNW6ji4hb_pFXlSxjg5teyyYmIEfIcAQcegfZbcOT5rpr19aLur6gI9Snd2irNiTSzLUY-rsPiQzr4lcnNWG2QHTFswXOYBxqlUwQQHZWt-h-eNtxmAL7Iwz5FKx8OV5Tsm7AWf_d67MxKpxmEBVpwZKgoU_Db2ACRJVa8cAKlVioV7eSGMojdN-nvsA-aoexxN9Tw_BVp5qeiNY48oV4QeNFhelwr7yg-h3jln67sQ_8YC8RgsKFYvuNtaGPmoRrfGkO2Pr1aQVUnalrKsUNgrx08aRy4MMjDHwaV2lKuGGjnD79ibPvkOMKMBK5IjBe-YFI1d0YvZO6ctozAtQm-I5nTE0MA50lv4C-teAnpPXG4wUc-ak_aRHYRkshpNr0uv9OVJffshVGfTqjjkQ49ts96wEAiD5wvNn=w876-h657-no

Wakwanza kushoto waliokaa ni Japher Kirilo na wanne waliosimama ni Abdul Sykes
katika picha ya Waasisi wa TANU.


Japhet Kirilo na Earle Seaton wameandika kitabu, ‘’The Meru Land Case,’’ kuhusu mgogoro wa ardhi ya Wameru ambayo ardhi yao ilichukuliwa na Wazungu bila fidia. Mimi nimekieleza kisa hiki kufuatana na jinsi Abdulwahid Sykes akiwa kiongozi wa TAA alivyokishughulikia akishirikiana na Earle Seaton na Japhet Kirilo kwa nia ya kuongeza ufahamu wa mkasa huu. Naweka hapo chini kipande kidogo kutoka kitabu cha maisha ya Abdul Sykes:


1952

Baada ya Dr Kyaruzi kuhamishiwa Nzega nafasi ya rais ikawa wazi. Abdulwahid akakaimu nafasi hiyo sasa akiwa katibu na kaimu rais wa TAA. Mgogoro wa ardhi ya Wameru ulikuwa umekwishaanza lakini bado haujalipuka kuwa suala lililowahusu Watanganyika wote. Umoja wa Mataifa ulipotuma ujumbe wake wa pili kuzuru Tanganyika mwaka wa 1950, Wameru waliwasilisha rasmi malalamiko yao kwa ujumbe huo. Abdulwahid aliwaomba wajumbe wa Baraza la Kutunga Sheria washirikiane na TAA katika kutatua baadhi ya matatizo yanayokabili jamii ya Waafrika. Abdulwahid alifadhaishwa na wajumbe Waafrika katika Baraza la Kutunga Sheria pale waliposhindwa kuipinga Wilson Report ambayo ilipendekeza kuondolewa kwa wananchi wa Meru kutoka kwenye ardhi yao. Katika barua aliyoiandikia Meru Citizenís Union, Abdulwahid, kwa niaba ya makao makuu ya TAA, aliwahakikishia watu wa Meru kuwa tatizo lao llilikuwa tatizo la Watanganyika wote.

Abdulwahid aliamua kutumia mgogoro wa ardhi ya Wameru kuwaunganisha Watanganyika wote dhidi ya serikali ya kikoloni. Uamuzi wa serikali juu ya mapendekezo ya TAA kwa Constitutional Development Committee ulikuwa bado umo akilini mwake. Alitambua kwamba uamuzi wa Gavana ulikuwa ni mpango wa muda mrefu wa kuwadhalilisha Waafrika katika utumwa wa daima. Abdulwahid sasa akiwa na ghera kubwa alianza kufanya kazi ya kuwahamasisha watu wa Tanganyika chini ya vuguvugu la kuunganisha umma dhidi ya utawala wa Waingereza. Abdulwahid aliwasiliana na Earle Seaton mjini Moshi kutaka ushauri wa kisheria juu ya tatizo la Meru. Seaton alikuja Dar es Salaam na kukutana na Abdulwahid na uongozi wa TAA. Ilikubaliwa na pande zote mbili kuwa makao makuu ya TAA, Meru Citizenís Union ikiongozwa na Japhet Kirilo na Seaton lazima waunganishe shughuli zao katika kesi hiyo na kwa pamoja watume rufaa yao kwenye Baraza la Udhamini la Umoja wa Mataifa huko New York. Kwa sasa uongozi wa chama cha TAA ulitambua kwamba nusura yao ilitegemea uwezo wao wa kudhibiti na kushawishi matukio na maamuzi ndani ya Baraza la Kutunga Sheria. Ili kuweza kufanya hayo shinikizo lilitakiwa kuwekwa katika Baraza la Udhamini huko New York, nchini Amerika na siyo katika Ofisi ya Makoloni pale London Uingereza.

Tawi la chama cha TAA la Tabora lilichukua changamoto hiyo kwa kupitia juhudi za Kandoro aliyeuona mgogoro wa ardhi ya Wameru kama jukumu lake binafsi. Kandoro aliitisha mkutano wa matawi ya TAA ya Mwanza, Kigoma na Tabora kujadili suala hilo. Mwanza iliwakilishwa na Bhoke Munanka, Mzee Mkama Mlaji na Mohamed Kihaka Kitenge; kutoka Kigoma mjumbe aliyekuja alikuwa Jumanne Mawimbi na Tabora iliwakilishwa na Sheikh Kinana, Kandoro na George Magembe kama rais wa TAA tawi la Tabora. Mkutano wa Tabora uliahidi mshikamano wa pamoja na watu wa Meru katika mapambano dhidi ya walowezi.

Mgogoro wa ardhi ya Meru ni wa pekee katika historia ya Tanganyika. Ilikuwa kupitia katika mgogoro huo ndiyo Mtanganyika, Japhet Kirilo, akifuatana na Earle Seaton kama mkalimani na mshauri wa sheria, kwa mara ya kwanza alizungumza mbele ya Baraza la Udhamini la Umoja wa Mataifa huko New York, na kuonyesha udhalimu wa ukoloni. Mnamo November, 1952 Kirilo alizungumza mbele ya Kamati ya Nne ya Baraza Kuu. Watu wa Tanganyika sasa walikuwa wanayachukua mapambano yao toka mipaka yao hadi kwenye kumbi za Umoja wa Mataifa, mjini New York kutafuta haki. Lakini Kirilo alirudi mikono mitupu. Rufaa ya mgogoro wa ardhi ya Wameru ilitupiliwa mbali. Kirilo aliuhakikishia Umoja wa Mataifa kuwa watu wake kamwe hawatachukua silaha kuikomboa ardhi yao kama Wakikuyu wa Kenya walivyojaribu kufanya. Kwa kweli hapakuwa na sababu ya kutoa kauli hii, kwa kuwa uhakikisho wa kutokuwepo mapambano uliwafanya walowezi washushe pumzi na kujiona wako salama. Tangu mwanzo wa mgogoro wazalendo nchini Kenya kama Fred Kubai na Kung'u Karumba walikuwa wakitoa ushauri kwa Meru Citizenís Union kwa kuwa wao walikuwa na ujuzi zaidi wa matatizo ya walowezi kuliko watu wa Tanganyika.

Kwa mtazamo wa juu juu mtu anaweza kudhani kuwa Abdulwahid alikuwa akipata kipigo kutoka sehemu zote alizojaribu kuipenyeza TAA kutoka mwaka wa 1948 katika enzi za chama cha makuli, kufikia marekebisho ya katiba hadi kumalizikia kwa mgogoro wa ardhi ya Wameru. Kushindwa huku si kwa sababu TAA ilikuwa ina viongozi dhaifu au ilikuwa haiuingwi mkono na umma. TAA ilikuwa haifanikiwa katika madai yake kwa sababu serikali ya kikoloni ilikuwa imeamua kutosikiliza lolote kuhusu matatizo ya Waafrika. Matokeo ya hali hii ilimfanya Abdulwahid aamue kuwa njia iliyobakia ya Tanganyika kujitoa katika makucha ya Waingereza ni kuuandaa umma wa Tanganyika chini ya chama cha siasa. Mara tu baada ya Kirilo kurejea kutoka New York, mpango wa kuanzisha chama cha siasa cha kushirikisha umma wote ulianza.

Uongozi wa TAA Makao Makuu ulianza kampeni ya nchi nzima kuueleza umma matokeo ya safari ya Kirilo kwenye Umoja wa Mataifa kuhusu mgogoro wa ardhi ya Wameru na vilevile kuchangisha fedha za kupeleka msafara mwingine katika Umoja wa Mataifa kuueleza umoja huo kuwa Tanganyika ilikuwa chini ya udhamini na Watanganyika walikuwa sasa na haki ya kudai uhuru wao. Kamati ya TAA ya watu watatu iliyowajumuisha Kandoro, Kirilo na Abbas Sykes iliundwa kwa ajili hiyo. Ally Sykes akiwa mweka hazina msaidizi wa TAA aliombwa ampelekee Kirilo hawala ya posta Usa River kama nauli ya kumwezesha kusafiri hadi Dodoma kujiunga na ile kamati ya watu watatu. Kulikuwa hakuna huduma ya fedha katika posta ya Usa River na fedha zile zilikaa hapo kwa muda bila ya kuchukuliwa hadi hapo zilipopelekwa posta ya Arusha mjini ambako Kirilo alizichukua.Kuanzia tarehe 26 Septemba, 1953 kwa takriban mwezi mmoja ile kamati ilitembelea na kuhutubia mikutano ya hadhara, ikikusanya fedha Dodoma, Mwanza, Bukoba, Ukerewe, Tarime, Musoma na Shinyanga. Rais wa chama cha TAA, kanda ya ziwa, Paul Bomani aliipokea ile kamati ya watu watatu na kuhutubia mikutano pamoja nao katika jimbo lote. Bomani aliwaambia wanachama wa TAA na wananchi wote mjini Mwanza kuhusu umuhimu wa kuchanga fedha kwa kwa kusudio hilo.

proxy

Katika miaka ya 1950 Cosy Cafe ilikuwa hotel ikipendwa sana na viongozi wa TAA
Abdulwahid Sykes akipenda sana kuja hoteli hii na marafiki zake kama Earle Seaton.


20140129_140544.jpg

Kushoto Abdulwahid Ally Sykes na Mwandishi Nyumbani kwa Japhet Kirilo Usa River,
Arusha mwala wa 1989 wakati wa utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes.
 
Kimeandikwa na mwenyewe Hayati Kirilo Japhet kimeeleza mambo mengi hata kuhusu tiketi ya ndege kwenda New York kuwa ililipwa na Mangi Mareale kama kumbukumbu zangu zipo sahihi
Babusuma,
Nimekisoma kitabu na hata katika tafiti zangu sikuona popote ambapo
Chief Marealle ametajwa.

Sikumbuki.
Kama kuna mtu anacho hicho kitabu atalii kisha atujuze.
 
Unataka kuanzisha balaa kama analilokutana nalo Mohamed Said. Kwa ujumla historia ya Tanzania ina mengi ambayo hatufundishwi mashuleni.
Hii historian ni muhimu ukweli ni lazima usemwe tu.

Kaka ...
 
Hii historian ni muhimu ukweli ni lazima usemwe tu.

Kaka ...
Tatizo la wanahistoria wengi hawataki kuijulisha jamii ukweli wa historia ya Tanzania. Sijui huu woga utaisha lini. Huyu Bwana Japher Kirilo wengi hatumjui, ingawa alisaidia kuleta kashkash kwa wazungu ili waelewe Watanzania wameshaanza kujitambua. Lakini watawala hawataki ajulikane kabisaa!
 
Fisadi,
Hiki kitabu kilikuwa kinauzwa madukani na mimi nilinunua
nakala yangu Tanzania Elimu Supplies, Dar es Salaam.
Asante sana Mzee... Itabidi nami niipate nakala ngumu niiweke Library kwa ajili ya watoto na wajukuu wangu..

Shukrani..
 
Back
Top Bottom