Mtanzania, Alphonce Simbu ashika nafasi ya tatu Marathon IAAF LONDON

Kuna Dada aliwapita wenzake kama mita 100 hivi lakini akawa wa mwisho.

Sent using Jamii Forums mobile app

Tunamshukuru mleta mada kwa taarifa hii.
Pia ninakushukuru wewe kwa updates juu ya kina mama.
Zaidi ninakushukuru kwa updates za huyo dada wa mwisho maana wakati anaanza nilimuona(alivaa kijani chini) ila nilishindwa kufuatilia mpaka mwisho kujua hatima yake.
 
Anaitwa Magdalena Shauri, sijui alimaliza wa ngapi, mwanzoni alikuwa kundi moja na wakenya.
 
Wawakilishi wetu kwa wanawake walikuwa 3 ,sijajua matokeo yao
 
Huyo mkenya apimwe mkojo kama ametumia dawa za kuongeza nguvu au la.
maana wakenya wamekumbwa na kashfa ya kutumia madawa ya kuongeza nguvu kwa muda mrefu
 
Hivi huyu jamaa si ni muajiriwa wa Jkt inakuaje mwanajeshi anashiriki mashindano ya kiraia,Nijuavyo wanajeshi wana mashindano yao
 
Watu wa ukanda wa mashariki ya Afrika tumebarikiwa sana stamina katika mbio
 
Duuhhh..., aisee hongera sana, huyu akirudi JPM amnunulie gari nzuri, apewe nyumba nzuri hata mbezi au kimara na aolewe mke mzuri kabisa kama hana, hii itasaidia kutengeneza morale boost kwa upcoming talents, hivi ndivyo Kenya wanavyo wa-motivate athletes wao. DO THIS PLEASE. Hizo pesa zitarudi kupitia utalii maana ameitangaza Tanzania dunia nzima
 
..umesahau pia kuwa hata kwa maendeleo ni Arusha Na Moshi ziko juu...Na pia elimu....shule bora ziko Arusha Na Kili....pia watu vichwa Na wenye mafanikio Na wasomi wengi wanatoka Arusha Na Kilimanjaro... Ndio maana hata JPM anaumia....kwa mafanikio ya mikoa hii....wanasahau kuwa watu wa huku ni wenye juhudi sana Na wenye kupenda maendeleo...

 
Ni kweli kabisa,
 
JPM inabidi amuite ikulu, amuite tuu maana hakuna namna, nimefurahi sanaaaaaaaaa, ningeweza nimgemnunulia hata Jet kama ya Gwajima, basi tu..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…