Mtanzania ateuliwa kuiongoza Mamlaka ya Mapato ya Sudan Kusini (NRA)

Wangechukua na rais pia tumeshampata mbadala wake
 
Mwenye CV ya huyu jamaa
Mmoja ya wasomi nguli wa kodi TZ

Alikuzwa na TRA ya Kitilya miaka ya 2000, baadae akawa mkuu wa chuo cha kodi, Mikocheni, alihamishwa na kupelekwa idara ya forodha kama naibu kamishina chini ya bwana Tiagi Masamaki . 25 november 2015 baada fumua fumua ya JPM alikaimu kama kamishina mkuu wa forodha haikuchukua miezi 2 akatumbuliwa TRA/utumishi wa umma akarudi sector binafsi kwenye NGOS Kama mshauri na kufundisha part time kwenye vyuo ya elimu ya juu.

Pia ana uhusiano mzuri na South Sudan kwani baadhi wa wanafunzi wake ITA Mikocheni ndio walikuwa waanzilishi wa Revenue authority ya SUDAN Kusini, wakati wa JK na Kitliya aliwapeleka Watanzania wengi kutoka TRA kwenda kusaidia kuanzisha REVENUE AUTHORITY ya sudan Kusini.

Hakika anastahili.
 
Kama tuna mtu kama huyo, na tunao wengi tu, iweje wasipewe nafasi, tupewe mtu wa kutoka nje? Tz tumeshawasomesha raia wetu wengi tangu baada ya uhuru na sifa na vigezo wanazo, sio sawa na SS ambao ndio wanaanza safari baada ya uhuru wao.
 
Duuh, ni mchaga?
 
Jinga sana tunapiga kelele sababu hao wataalamu tunao.

Na nikwambie tu Mimi ntaongoza makelele kama wakiajili MTU ambae sifa zake tunazo.
 
Jinga sana tunapiga kelele sababu hao wataalamu tunao
Na nikwambie tuu Mimi ntaongoza makelele kama wakiajili MTU ambae sifa zake tunazo
Kwahiyo unadhan huko SS hakuna wenye sifa kama za huyo Mtanzania, kwenye Competence hawaangalii elimu pekee Mkuu, fikiria nje ya Box uwe GT. Hivi unadhan hakuna mwenye vyeti kama Senzo Pale Yanga GSM? Endelea kukaa na mavyeti yako ukidhan ndio kila kitu with no Global Experience, Expossure nk nk utaishia kutukana wakubwa zako ndio uwezo wako umeishia hapo na akili zako kama James Dell
 
Nimekuelewa mzee baba.

Kumbe pande la huko ni juhudi binafsi

Ova
 
nakukumbusha tu!

Ni ujinga kwa mtu msomi na mwelewa kutumia abbreviations zisizo rasmi ,ni upunguani kwenye paragraph unapoandika SS (southern Sudan ),wengine kuandika vifupisho vya majina ya watu ,huo ukilaza tumieni na wake zenu siyo kwenye public
 
South Sudan uchumi wao unategemea sana mauzo ya kunguru na sungura.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…