bongodili tele
JF-Expert Member
- Jun 8, 2024
- 1,520
- 3,022
UTAJIRI ULIOMO KWENYE MAGROUP YA WHATSAPP
Idadi ya wanakundi zidisha kwa Tsh 1000
Huu ni mchango wa siku moja kwa kila mwanakundi
Kisha zidisha kwa wiki
Kisha zidisha kwa mwezi
Kisha zidisha kwa mwaka
Hapo utaweza kupata jibu la watu waliomakini kwenye kutumia fursa utaona ni kiasi gani cha pesa kwa mwaka wanaweza kukikusanya kama mtaji
Mfano:
▶️Kundi la watu 200
(WNC = 257)
▶️Kila mtu kwa siku atoe 1000
▶️Itakusanywa 200,000
▶️Kwa siku 7 hitakusanywa 1,400,000
▶️Kwa wiki 4 itakusanywa 5,600,000
▶️Kwa mwaka itakusanywa 67,200,000
Jambo hili huweza kufanyika kwa malengo ya mwaka mmoja au miwili kukusanya mtaji
Mradi utakaoanzishwa ukawa na mgao kwa wanakundi kila mwaka
MTAFIKAJE HAPO
▶️Kwanza kundi liwe na watu wenye malengo ya pamoja wakweli waliodhamiria kusaidiana kuondoka kwenye lindi la umasikini
▶️Pili lazima muwe watu wa eneo moja mnaloweza kukutana kwa urahisi
▶️Tatu lazima mfanye mkutano wa pamoja wa maaamuzi ya kuliendea lengo hilo kwa kuchagua viongozi wakweli wenye dira na hilo jambo
▶️Nne lazima ujirasimishe kwa mamlaka husika na kujisajili na muwe na Uongozi na mfungue akaunti ya benki wanakundi wote wawe wanachama wa hiyo taasisi ili waweze kuhoji na kushiriki katika uendeshwaji wa jambo kihalali
Hapa nitakuwa nimewafumbua macho wenye akili
Watu wamo kwenye makundi mengi tu ila hayanafaida zaidi ya kupiga soga kuchekeshana na kutumiana maujingaujinga 🤔
Tuzinduke
Unakuta mtu simu yake ina kundi la:
Shule ya msingi,
Secondary,
A level,
Chuo kikuu,
Bado makundi ya kazini,
Bado makundi ya familia,
Bado makundi ya mitaaani, nk.
Katika makundi haya yote ni liability ya kuomuongezea gharama ya data tu na kusogoa hana kundi hata moja lenye uwezo kumnyanyua kipato chake huku ni kupoteza muda sana🤔🤔
Mwisho wa siku ni umasikini tu uliokithiri🤔
Amkeni, tumelala
Idadi ya wanakundi zidisha kwa Tsh 1000
Huu ni mchango wa siku moja kwa kila mwanakundi
Kisha zidisha kwa wiki
Kisha zidisha kwa mwezi
Kisha zidisha kwa mwaka
Hapo utaweza kupata jibu la watu waliomakini kwenye kutumia fursa utaona ni kiasi gani cha pesa kwa mwaka wanaweza kukikusanya kama mtaji
Mfano:
▶️Kundi la watu 200
(WNC = 257)
▶️Kila mtu kwa siku atoe 1000
▶️Itakusanywa 200,000
▶️Kwa siku 7 hitakusanywa 1,400,000
▶️Kwa wiki 4 itakusanywa 5,600,000
▶️Kwa mwaka itakusanywa 67,200,000
Jambo hili huweza kufanyika kwa malengo ya mwaka mmoja au miwili kukusanya mtaji
Mradi utakaoanzishwa ukawa na mgao kwa wanakundi kila mwaka
MTAFIKAJE HAPO
▶️Kwanza kundi liwe na watu wenye malengo ya pamoja wakweli waliodhamiria kusaidiana kuondoka kwenye lindi la umasikini
▶️Pili lazima muwe watu wa eneo moja mnaloweza kukutana kwa urahisi
▶️Tatu lazima mfanye mkutano wa pamoja wa maaamuzi ya kuliendea lengo hilo kwa kuchagua viongozi wakweli wenye dira na hilo jambo
▶️Nne lazima ujirasimishe kwa mamlaka husika na kujisajili na muwe na Uongozi na mfungue akaunti ya benki wanakundi wote wawe wanachama wa hiyo taasisi ili waweze kuhoji na kushiriki katika uendeshwaji wa jambo kihalali
Hapa nitakuwa nimewafumbua macho wenye akili
Watu wamo kwenye makundi mengi tu ila hayanafaida zaidi ya kupiga soga kuchekeshana na kutumiana maujingaujinga 🤔
Tuzinduke
Unakuta mtu simu yake ina kundi la:
Shule ya msingi,
Secondary,
A level,
Chuo kikuu,
Bado makundi ya kazini,
Bado makundi ya familia,
Bado makundi ya mitaaani, nk.
Katika makundi haya yote ni liability ya kuomuongezea gharama ya data tu na kusogoa hana kundi hata moja lenye uwezo kumnyanyua kipato chake huku ni kupoteza muda sana🤔🤔
Mwisho wa siku ni umasikini tu uliokithiri🤔
Amkeni, tumelala