Mtazamo kuhusu ndoa

usioe au kuolewa kisa umri umeenda, coz unampenda mtu fulani ukamlazimisha kuingia kwenye mahusiano kwa ahadi ya ndoa kwamba ukinikubali nakuoa au ukibeba mimba yangu nakuoa, na usioe au kuolewa kisq mtu fulani anakufikisha kilele au sure he/she z the right person for you na wengine wanaoa na kuolewa kisa jamaa au mdada ni mzuri ndo maana mnashauriwa mchunguzane kwanza ujue tabia za mwenza wako anafaa kuqa wife or husband
 

Pole hujawahi kupendwa wala kupenda,sitashangaa km wewe ni product ya mchepuko...mtoto aliyelelewa na baba na mama kwa upendo..na yeye huwa na upendo....na siku moja atataka kuanzisha familia yake na kuhakikisha anailea kwa upendo....upendo hauangalii gharama....mwana JF...mmoja hapo juu amesema ni unconditional....badilika mkuu dada poa sio solution...utaambulia magonjwa bure.....
 
Reactions: BAK

Ni mimi niliyesema unconditional. Huyu mdau anahitaji counseling
 
Watu wengi wanafikii kwa kwa kukaririshwa bila kutumia akili zao. Wanafundishwa utumwa wa mawazo tangu wakiwa wadogo kama wewe kama wewe. Hata kama wazazi wako waliishi vibaya basi nawe uishi vibaya? Tumia akili yako badilisha maisha yako yawe bora zaidi na yenye uhuru zaidi na yenye ukweli kuliko hayo maisha ya kuigiza yenye kuidanganya nafsi yako. Suala kama ni product ya mchepuko au la halihusiani na hili, hapa ni utumwa na uhuru wa kufikiri kwa uhalisia bila kujidanganya. Kuhusu maradhi ndiyo umenichekesha kweli. Hivi hata kwa akili kidogo tu umeshindwa kujua kama asiye mtumwa wa ndoa yuko 100% safe kuliko aliye utumwani ambaye yuko 50% safe kwani 50% nyingine anatembea nayo bwana wake ambaye hujui yuko wapi saahizi!
 

Mkuu unahitaji msaada kuliko unavyofikiri,km ulizaliwa kny ndoa ya Baba na mama na kwa upendo,utataka siku moja uwe na familia yako na uilee kwa upendo,.. ............hamna cha kukariri hio ni 'given'...au constant lol........ila km ulikuwa na difficult ubringing i mean umeona baba yako au mama yako akichepuka then your trust on people will be limited....na siku zote utaonyesha anger yako unknowingly........

Usisambaze chuki zako plz,pale juu nimeona umelist hadi gharama utakazoencounter ukiwa na mke....mpk nimejiuliza huyu mwana JF km ni mzima?!...maanake ina maana wewe huudumii wazazi wako au ndugu zako??...mnh

Mwisho piga picha,wote hatuuoani watoto wetu ambao ndio Taifa la kesho,watakua katika mazingira gani?...namaanisha hujui kuwa watoto wanahitaji ukaribu wa baba na mama..ili kukua sio tu kimaadili bali academically...?

Hio ya kuambukizwa niliiongelea baada ya wewe kusema dada poa ndio solution yako....hio ni your own preference km umeamua kujilipua,condoms haziko 100%safe.............shaurilo!
 
Jestina ,
Bado naona unanipiga mapanga mimi binafsi bila kunijibu hoja zangu. Unachanganya mambo hapa tunazungumzia NDOA na si familia wala upendo. Kukuelewesha vizuri mimi nimezaliwa ndani ya NDOA tena zile za zamani zenye utumwa wa upendo, furaha na amani
Sijawahi kuona wakiwa hawana furaha pamoja hadi leo hii lakini ninahakika furaha ya kitumwa. Mimekuwa mtu mzima sasa nahitaji kurekebisha makosa yaliyofanya vizazi vilivyopita kwa kufikiri njia iliyo bora zaidi yenye uhalisia iliyo huru itakayofanya watu waishi kwa uhuru mpana zaidi wa kuwajibika. Dec last year I fired staff wangu mwenye CV nzuri sana nilikuwa namlipa 4x ya alichokuwa akilipwa kabla alishindwa kufanya kazi ndogo muhimu iliyosababishia hasara kubwa kwa sababu ya ndoa yake. Na kwa ujinga wake tena akamtuma mkewe aje kuniomba nimrudishe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…