Mtazamo wa Mkulu na wanawake weupe

Mtazamo wa Mkulu na wanawake weupe

Mikono yenye Sugu

Senior Member
Joined
Jul 1, 2020
Posts
133
Reaction score
215
Pamoja na kumuunga mkono Mkulu wetu kwa kiasi kikubwa katika maamuzi yake mengi, upenzi wangu haunizuii kuyasemea madhaifu yake kadhaa.

Mara kadha Mkulu akimtambulisha msaidizi wake (Makamu) amekuwa akimsifia kwa "weupe na uzuri". Kwangu hilo linanichefua kwani kwa hadhi na nafasi yake akitoa kauli inakuwa na athari kubwa kwa jamii.

Mathalan, kwa kauli kama hiyo huwa anajiuliza wanawake weusi wanajisikiaje? Bila shaka jambo hilo sio zuri kwani wengine huku mitaani hatuishi kuwajengea "confidence" wanawake weusi wajikubali na wasisumbuke kujichubua kwani uzuri hautafsiriwi kwa weupe au weusi wa mtu.

Tunatoa wito kwa walio karibu na Mkulu, kumshauri juu ya hilo kwani, hata kama anatania, matokeo yake kwa dada zetu ni maumivu mioyoni. Hongereni wanawake wote wa Tanzania, weusi kwa weupe, ninyi ni wazuri na tunawapenda.

Kwa kuwa Mkulu huwa anawasilisha kama "kautani", namshauri pia mama yetu naye amrekebishe kama "kautani" kwa kuwasifia weusi.

Ni hayo tu kwa leo.
 
Pamoja na kumuunga mkono Mkulu wetu kwa kiasi kikubwa katika maamuzi yake mengi, upenzi wangu haunizuii kuyasemea madhaifu yake kadhaa. Mara kadha Mkulu akimtambulisha msaidizi wake (Makamu) amekuwa akimsifia kwa "weupe na uzuri"....
Ndio maana mama yetu namaanisha yule mama wa zimbabwe aligoma kugombea kwa madai ya sexual harrasment, anadai alishachapwa vibao na mwenyekiti wa cahama tawala zimbabwe, na kuna wakati almanusura achaniqe hadi nguo maana mwenye kigoda alishindwa kuvumilia ule weupe alitaka auone live

Ila jamani Zimbabwe kuna mambo, sisi weupe tuna tabu sana
 
Pamoja na kumuunga mkono Mkulu wetu kwa kiasi kikubwa katika maamuzi yake mengi, upenzi wangu haunizuii kuyasemea madhaifu yake kadhaa. Mara kadha Mkulu akimtambulisha msaidizi wake (Makamu) amekuwa akimsifia kwa "weupe na uzuri"...
Hayo ni mambo ya UTANI kwa ajili ya kusherehesha mikutano. Rais Magufuli ni binadamu kama binadamu wengine wote, suala la utani na kutania watu si kosa eti jamani?
 
Ndio maana mama yetu namaanisha yule mama wa zimbabwe aligoma kugombea kwa madai ya sexual harrasment, anadai alishachapwa vibao na mwenyekiti wa cahama tawala zimbabwe, na kuna wakati almanusura achaniqe hadi nguo maana mwenye kigoda alishindwa kuvumilia ule weupe alitaka auone live

Ila jamani zimbabwe kuna mambo, sisi weupe tuna tabu sana

Pole dada yangu! Bahati mbaya ni kwamba wanawake ndio wanaoyumbishwa na mitazamo hiyo kwa kiasi kikubwa kwani hutamani kuwaridhisha akina "sisi". Lakini na akina "sisi" tuna mapendeleo tofauti.

Baadhi ya akina "sisi"tunapenda weupe asubuhi na jioni tunapenda weusi. Wengine usiku wanapenda wafupi mchana wanapenda warefu. Jikubali ulivyo kwa kuwa kuna wanaowapenda wa aina yako wala sio wa aina ile! Wamama/wadada msifukuzane na upepo wa kuturidhisha akina "sisi", HATUWEZEKANI!
 
Pamoja na kumuunga mkono Mkulu wetu kwa kiasi kikubwa katika maamuzi yake mengi, upenzi wangu haunizuii kuyasemea madhaifu yake kadhaa.

Mara kadha Mkulu akimtambulisha msaidizi wake (Makamu) amekuwa akimsifia kwa "weupe na uzuri". Kwangu hilo linanichefua kwani kwa hadhi na nafasi yake akitoa kauli inakuwa na athari kubwa kwa jamii...
Ninamkumbuka marehemu mzee Kingunge (RIP) alisema """ huyu anastahili kuwa mnyampala wa barabara na si vinginavyo"" sasa yametimia.
 
Pole dada yangu! Bahati mbaya ni kwamba wanawake ndio wanaoyumbishwa na mitazamo hiyo kwa kiasi kikubwa kwani hutamani kuwaridhisha akina "sisi". Lakini na akina "sisi" tuna mapendeleo tofauti. Baadhi ya akina "sisi"tunapenda weupe asubuhi na jioni tunapenda weusi. Wengine usiku wanapenda wafupi mchana wanapenda warefu. Jikubali ulivyo kwa kuwa kuna wanaowapenda wa aina yako wala sio wa aina ile! Wamama/wadada msifukuzane na upepo wa kuturidhisha akina "sisi", HATUWEZEKANI!
Mwambieni basi mwenyekiti wa zimbabwe abadili sera kuanza kumsifia huyo mama jukwaani sio sera
 
Hayo ni mambo ya UTANI kwa ajili ya kusherehesha mikutano. Rais Magufuli ni binadamu kama binadamu wengine wote, suala la utani na kutania watu si kosa eti jamani?

Ndugu yangu ikizidi inapanda mbegu hasi katika jamii! Urais ni taasisi yenye ushawishi wa kuanzisha jambo ama kulikomesha. Ndio maana nilichotoa ni tahadhari ya kiushauri. Sitaki kupenda uongozi wake kugeuke kuwa upofu wa fikra kwangu, natamani kuhusika kuonesha kasoro za kiongozi ninayempenda kama huyu.
 
Kiukweli kabisa mama Samia ni kisu,jicho limenakshiwa unaweza dhani kama anakausingizi kwa mbaali hivi au alipita na ka K-vant kale kadoogo.alafu ni "powerfull woman"hii inazidi kuongeza uzuri wake.
 
Pole dada yangu! Bahati mbaya ni kwamba wanawake ndio wanaoyumbishwa na mitazamo hiyo kwa kiasi kikubwa kwani hutamani kuwaridhisha akina "sisi". Lakini na akina "sisi" tuna mapendeleo tofauti. Baadhi ya akina "sisi"tunapenda weupe asubuhi na jioni tunapenda weusi. Wengine usiku wanapenda wafupi mchana wanapenda warefu. Jikubali ulivyo kwa kuwa kuna wanaowapenda wa aina yako wala sio wa aina ile! Wamama/wadada msifukuzane na upepo wa kuturidhisha akina "sisi", HATUWEZEKANI!
Leo amewaambia mzae kama panya kwasababu matiti ya kunyonyesha mnayo.
 
Kila mtu ana chaguo lake, Kama wewe unapenda blak Magu anapenda white! hivyoo
 
Ndugu yangu ikizidi inapanda mbegu hasi katika jamii! Urais ni taasisi yenye ushawishi wa kuanzisha jambo ama kulikomesha. Ndio maana nilichotoa ni tahadhari ya kiushauri. Sitaki kupenda uongozi wake kugeuke kuwa upofu wa fikra kwangu, natamani kuhusika kuonesha kasoro za kiongozi ninayempenda kama huyu.
Sawa that is your take na mawazo yako. Sawa kabisa. Tuko pamoja.
 
mnazidi na nyie... Kwahiyo hamuwezi kutofautisha masihala na ukweli?
 
Umewafikiria wanawake weusi waliopo mtaani hujamfikiria mkewe anajisikiaje? Maana kwa jinsi ninavyomuona sio mweupe yule

Ndio maana nashauri yeye kama Mkulu atunze kila neno linalotoka kinywani mwake kwani mamlaka aliyonayo ni "taasisi". Nakumbuka siku moja tukiwa darasani chuoni na wenzangu tulianzisha mjadala wa utani tu kusifia wanawake wenye umbo na rangi fulani. Katikati ya mzaha huo dada mmoja alianza kulia.

Tulipomdodosa kumbe aliachana na mpenzi wake kwa kuwa mpenzie aliporwa na mwanamke mwenye vigezo tulivyokuwa tunazungumzia. Bahati mbaya lilikuwa darasa la MA- in Sociology. Niliumia sana na tokea hapo nimekuwa mwngalifu sana kujadili tabia au wajihi wa watu, hususan wanawake.
 
mnazidi na nyie... Kwahiyo hamuwezi kutofautisha masihala na ukweli?

Sijasema Mkulu anamaanisha. Soma bandiko langu vizuri. Isipokuwa nasisitiza "asizidishe" kwani wakati mwingine maneno na vijineno husababisha maumivu ya nafsia kwa baadhi ya watu.
 
Ndio maana nashauri yeye kama Mkulu atunze kila neno linalotoka kinywani mwake kwani mamlaka aliyonayo ni "taasisi".
Nakumbuka siku moja tukiwa darasani chuoni na wenzangu tulianzisha mjadala wa utani tu kusifia wanawake wenye umbo na rangi fulani. Katikati ya mzaha huo dada mmoja alianza kulia...
Mimi ni mweusi, ila mtu akisifia weupe hata sijisikii vibaya....Cha ajabu mambo mengine huwa najisikia vibaya, sijui kwa nini sijawahi kuona weusi ni tatizo kama watu wengine wanavyotazama
 
Back
Top Bottom