Mtazamo wa Tanzania kuhusu Nuclear

Hisia zako tu hizo. Watanzania tujiamini.

Kama wasema hivyo na wakenya je, waganda je na....na....na....

Iran kama China ina haja sana ya marafiki toka Afrika na imeshatembelea nchi nyingi sana tu za Afrika. Haikutembelea Tanzania kwa sababu eti Tuna Kikwete bali ni sababu ya kibiashara.
 
Zawadi hivi TANZANIA IKO KARNE YA NGAPI KIHALISIA?
 
Zawadi hivi TANZANIA IKO KARNE YA NGAPI KIHALISIA?
Umeuliza swali zuri sana. Tanzania ikiwa ni moja yanchi za Afrika ni vigumu kuziweka katika karne 10-21, kama ukipima karne kama Nchi za ulaya na marekani zilivyopitia.

Ukiniuliza Tanzania iko karne ya Ngapi, mara moja napiga taswira katika maendeleo, na hapo ndio inakuwa vigumu kuitafutia nafasi Tanzania. Niulize kwa nini?

Sababu ni za wazi kabisa na ni kama zifuatazo:

1. Tanzania inawasomi wengi kuliko Ujerumani, uingereza n.k zilipoanza maendeleo ya viwanda katika karne ya 18.

2. Tanzania ina msukuma mkokoteni aliye na mobile tel inayemrahisishia mawasiliano ambaye muendesha farasi wa ulaya katika karne ya 18 hakuwa naye.

3. Tanzania leo ina 68% ya watanzania wanojua kusoma na kuandika, wakati ambapo kulikuwana 45% ya wafaransa waliojua kusoma wakati wa maendeleo ya viwanda karne ya 18.

4. tanzania inasumbuliwa na njaa kama ulaya ilivyokuwa katika karne ya 19.

5. Usafiri wa kwanza wa gari mshi ulizinduliwa uhispania mwaka 1850, wakati sisi tunalo hilo miaka kibao japo linatuwekaweka.

Nisaidie kuorodhesha mambo mengine kibao ambayo yanaweza kujaza ukurasa huu, bila ya kusahau umeme na mtandao.

Kwa muhtasari ningeweza kusema Tanzania ni nchi iliyokatika karne mchanganyiko, nikimaanisha ina teknolojia za stone age na za kisasa.

Sijui kama nimekujibu swali lako.
 

Lini utaanza kujibu maswali unayoulizwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…