Mtazamo wangu kwa sasa Taifa halihitaji Katiba mpya, Rais Samia Hassan anatosha

Mtazamo wangu kwa sasa Taifa halihitaji Katiba mpya, Rais Samia Hassan anatosha

TheDreamer Thebeliever

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2018
Posts
2,490
Reaction score
3,584
Habari wadau,

Awamu iliyopita wengi waliililia katiba mpya sababu utawala uliopita wa awamu ya tano kiukweli uliwabana sana mbavu kila kona mpaka wakajiona kama wao sio sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Lakini SAP baada ya kuingia Mama Samia katika kiti cha Urais kwa kipindi hiki kifupi naona ametosha vya kutosha katika kiti chake cha Urais, amekuwa akiwatendea haki watu wa aina zote bila kujali vyama vyao na Utawala wa Sheria umerudi tena.

Kwa sisi makada imefikia point tunaona kama Mama anawapendelea sana Watoto wa kambo kuliko Watoto wake wa kuwazaa mwenyewe na hii ndio kariba ya Mwanadamu, sasa Wapinzani naamini wamekosa ajenda kilichobaki ni kungoja tu Mama kuwaruhusu kina Tundu Lissu warudi na atawaakikishia ulinzi wa kutosha maana ameshaanza kuwaandalia mazingira ya pakufikia bila shaka.

Sasa katika muktadha kama huu binafsi sioni kama Katiba Mpya ina umuhimu tena, tumuache Mama aendelee tu kutekeleza Ilani ya chama na kile ambacho anakiona sahihi. Wengine wanasema tumuache maama ajiandikie kitabu chake mwenyewe wala tusimshike mkono.

Kuhusu masuala ya tume huru, Uhuru wa vyombo vya habari, Utawala wa haki na Sheria na mengine mengi muachieni Mama najua kwa kipindi kichache wote tumenuelewa anapotupeleka sisi kama Taifa ni pazuri zaidi ya tulipotoka.
 
Mahitaji ya Katiba Mpya ni ya Watanzania walio wengi. Hivyo kwa upande wangu, nitapenda kuona mchakato unarejeshwa haraka iwezekanavyo.

Na irejejeshwe ile Rasimu ya Warioba kwenye Bunge Jipya la Katiba, litakalo undwa na Wanasiasa wachache kutoka vyama vya siasa, na wataalamu wengi kutoka sekta mbalimbali za kijamii, kiuchumi, kisiasa, nk.

Na iundwe pia by law ya kupinga aina yoyote ile ya coalition wakati wa majadiliano! Kusiwepo na UKAWA, sijui MATAGA! Nk.
 
Ni haki yake hata kama hana point kwa mm na wewe ila nampa pole hii nchi kama ilivyo inchi nyingene hazihitaje ten viongozi wazzuri wacha mungu wanaotenda haki bali MIFumo IMARA AMBAYO ITAFUATWA NA WATAWALA NA INAYOWEWAWAJIBISHA WOTE BILA KUJALI NYADHIFA ZAO . MIGUMU AMBAYO WENYE NCHI WANA HAKI YA KUFANYA MAAMUZI YEYOTE MUDA WOWOTE.
 
Usitulishe maneno katiba ni hitaji muhimu,isipokuwa kwa wanaonufaika na miata iliyopo kwenye hii ya sasa.
 
Tangu kuzuka kwa Corona nchini China mwaka 2019, mataifa mengi duniani yaliamua kuja na mbinu za kupambana na Corona kwa kufungia watu ndani(lockdown) kuvaa barakoa, social distance na mengine mengi ikiwemo Chanjo.

Tanzania tuliamua kuishi na Corona kwa kukataa kujifungia (lockdown) na shughuli ziliendelea kama kawaida na watu wakisafiri huku na huko, hata watalii kipindi cha Corona walikuwa wengi sana Tanzania.

Baada ya miaka miwili kupita tangu Corona izuke mataifa yaliyoongoza kwa vifo ni Marekani, China, India Brazil etc hayo mataifa ni tajiri yana mitungi ya oxygen mingi ,wana barakoa, na walijifungia.

Tanzania chini ya hayati rais Magufuli tuliamua kutumia njia za asili kama kunywa juice ya Tangawizi na malimao, kupiga nyungu na kumtanguliza Mungu mbele etc na matokeo yake impact ya Corona ni ndogo sana na tuliweza kuingia uchumi wa kati.

Cha kusikitisha baada ya miaka 2 ya Corona kupita ,tume iloyoundwa na rais Samia Suluhu licha ya hiyo kamati kujaa maprofesa wa afya inataka kutuaminisha kwamba watanzania si lolote si chochote na tunatakiwa tujifunze kwa waliofanya lockdown huko nchi za nje.!!!
Lakini ukweli ni kwamba ukipima impact ya Corona Tanzania inaonyesha tumefanikiwa sana na tulitakiwa tujivunie haya mafanikio hadharani na kuitaka dunia ije ijifunze Tanzania mbinu tulizotumia.

Hivi sisi watanzania nani aliyeturoga? Pamoja na ushahidi wote uliotuzunguka ukionyesha tumefaulu vita ya Corona bado maprofesa wetu wanataka tufanye kama walivyofanya India, Marekani, Rwanda?

Na Chadema nao wanashqngilia?
 
Hatuitaji katiba ya kumsaidia mtu, tunataka katiba ya watanzania wote. Kwa hiyo hoja yako ni kwamba akija rais usiyemtaka tudai katiba, akija umtakaye katiba uendelee???? Sasa hiyo ni akili au tope tu!.

Katiba tuitakayo ni katiba bora, ya kuheshimu haki za watu, inayomuwajibisha kiongozi hata kama ni rais, inayofuatia kiongozi tumtakaye kwa njia ya kura, inayosimamia raslimali za nchi, inayoweka mazingira sawa kwa wakulima, wafanyakazi na wafanyabishara, isiyopendelea chama au jamii fulani na kunyanyasa wengine, inayowapa wananchi mamlaka ya kuajiri na kuwaondoa viongozi, KATIBA INAYOZINGATIA SIASA SAFI, UONGOZI BORA NA UTAWALA WA SHERIA. TUNATAKA KATIBA MPYA!
 
Hatuitaji katiba ya kumsaidia mtu, tunataka katiba ya watanzania wote. Kwa hiyo hoja yako ni kwamba akija rais usiyemtaka tudai katiba, akija umtakaye katiba uendelee???? Sasa hiyo ni akili au tope tu!.

Katiba tuitakayo ni katiba bora, ya kuheshimu haki za watu, inayomuwajibisha kiongozi hata kama ni rais, inayofuatia kiongozi tumtakaye kwa njia ya kura, inayosimamia raslimali za nchi, inayoweka mazingira sawa kwa wakulima, wafanyakazi na wafanyabishara, isiyopendelea chama au jamii fulani na kunyanyasa wengine, inayowapa wananchi mamlaka ya kuajiri na kuwaondoa viongozi, KATIBA INAYOZINGATIA SIASA SAFI, UONGOZI BORA NA UTAWALA WA SHERIA. TUNATAKA KATIBA MPYA!
Huyo amelaaniwa
 
Baba yako angesoma mpaka University kwa mfumo rasmi tusingeshuhudia upumbavu huu uliouweka hapa.
Angekuwa ashakutupa chooni kwa njia ya punyeto.
Sasa shida ya kuzaa mapema ndio hii, unaleta duniani machizi fresh.
 
Habari wadau,

Awamu iliyopita wengi waliililia katiba mpya sababu utawala uliopita wa awamu ya tano kiukweli uliwabana sana mbavu kila kona mpaka wakajiona kama wao sio sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Lakini SAP baada ya kuingia Mama Samia katika kiti cha Urais kwa kipindi hiki kifupi naona ametosha vya kutosha katika kiti chake cha Urais, amekuwa akiwatendea haki watu wa aina zote bila kujali vyama vyao na Utawala wa Sheria umerudi tena.

Kwa sisi makada imefikia point tunaona kama Mama anawapendelea sana Watoto wa kambo kuliko Watoto wake wa kuwazaa mwenyewe na hii ndio kariba ya Mwanadamu, sasa Wapinzani naamini wamekosa ajenda kilichobaki ni kungoja tu Mama kuwaruhusu kina Tundu Lissu warudi na atawaakikishia ulinzi wa kutosha maana ameshaanza kuwaandalia mazingira ya pakufikia bila shaka.

Sasa katika muktadha kama huu binafsi sioni kama Katiba Mpya ina umuhimu tena, tumuache Mama aendelee tu kutekeleza Ilani ya chama na kile ambacho anakiona sahihi. Wengine wanasema tumuache maama ajiandikie kitabu chake mwenyewe wala tusimshike mkono.

Kuhusu maswala ya tume huru, Uhuru wa vyombo vya habari, Utawala wa haki na Sheria na mengine mengi muachieni Mama najua kwa kipindi kichache wote tumenuelewa anapotupeleka sisi kama Taifa ni pazuri zaidi ya tulipotoka.

Post #6
 
Back
Top Bottom