Mtazamo wangu: Sikukuu ya Krismass ni sikukuu ya kawaida ya kijadi ya wazungu kama zilivyo sikukuu zetu za mavuno vijijini

Mtazamo wangu: Sikukuu ya Krismass ni sikukuu ya kawaida ya kijadi ya wazungu kama zilivyo sikukuu zetu za mavuno vijijini

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Sikukuu hii imekuwepo kabla ya kuhusishwa na Ukristo. Inasemekana ili ukristo ujivunie waumini ilibidi waiingize kwenye dini na kuihusisha na Yesu. Matokeo yake wazungu wengi wasio na dini walivutwa.

Mimi ni mkristo, ila siichukulii siriasi licha ya huhusiswa na Yesu. Naichukulia kama Zile sikukiu za kijadi za mavuno ambazo watu vijijini hununua nguo mpya, kunywa soda nyingi, kula vitumbua na maandazi (hasa usukumani) na kula biskuti.

Kama tunakuwa na hamasa kubwa katika tamaduni na jadi za kizungu, basi tusisahau kuhudhuria na sikukuu zetu za kijadi vijijini kwetu. Tujifunze kupenda na vya kwetu kwa uzito uleule tunaopenda za kigeni.

Mfano. Denmark ni nchi inayoongoza kwa watu wengi ambao hawaamini uwepo wa Mungu na mambo ya dini, llakini ikifika sikukuu hii karibu wote wanasherekea maana historia inaonyesha kwenye utamaduni wao wa zamani kabla ya ukristo hizo sherehe zilikuwepo.

Kama waarabu walivyosambaza jadi na tamaduni zao kupitia dini, wazungu nao walipopokea ukristo kutoka kwa Wayahudi waliugeuza fursa ya kupenyezea jadi zao.

Ni hayo tu.
Ni vizuri ukifanya mambo ukiwa namaarifa mapana

Sikukuu njema
Mtumishi Matunduizi.
 
Sikukuu hii imekuwepo kabla ya kuhusishwa na Ukristo
Ilikuwa inaitwaje kabila ya kuhusishwa??

Na ilikuwa specific Kwa ajili ya nini hasa au ndio Hayo mavuno??


Inasemekana ili ukristo ujivunie waumini ilibidi waiingize kwenye dini na kuihusisha na Yesu. Matokeo yake wazungu wengi wasio na dini walivutwa.
Inasemekaña,.. inaonyesha huna uhakika. Na kitu kibaya Zaidi hujui history ya ukristo,,,na kwamba uliwafikiaje wazungu....Ulienezwa na kina Nani,,,, Please usiwaabishe wasukuma,,,Mimi ninamheshimu Sana the late John Magufuli.Aliwafanya wasukuma waonekane watu wenye kitu muhimu kichwani.


Mimi ni mkristo, ila siichukulii siriasi licha ya huhusiswa na Yesu. Naichukulia kama Zile sikukiu za kijadi za mavuno ambazo watu vijijini hununua nguo mpya, kunywa soda nyingi, kula vitumbua na maandazi (hasa usukumani) na kula biskuti
Unaweza kuwa sio mkristo au unaweza kuwa mkristo WA kina Joe davi tapeli ulieshindwa kuchagua Kati ya ukristo na usukuma...Hasa kutokana na kuwa na version fake na dhaifu ya ukristo...


Mfano. Denmark ni nchi inayoongoza kwa watu wengi ambao hawaamini uwepo wa Mungu na mambo ya dini, llakini ikifika sikukuu hii karibu wote wanasherekea maana historia inaonyesha kwenye utamaduni wao wa zamani kabla ya ukristo hizo sherehe zilikuwepo.
Hawa watu wasio na dini wanasheherekea Christmas ipi?? Kulingana na maana halisi ya Hii sikukuu..Au nao wanaomwamini YESU kisiri Siri??
 
Ilikuwa inaitwaje kabila ya kuhusishwa??

Na ilikuwa specific Kwa ajili ya nini hasa au ndio Hayo mavuno??



Inasemekaña,.. inaonyesha huna uhakika. Na kitu kibaya Zaidi hujui history ya ukristo,,,na kwamba uliwafikiaje wazungu....Ulienezwa na kina Nani,,,, Please usiwaabishe wasukuma,,,Mimi ninamheshimu Sana the late John Magufuli.Aliwafanya wasukuma waonekane watu wenye kitu muhimu kichwani.



Unaweza kuwa sio mkristo au unaweza kuwa mkristo WA kina Joe davi tapeli ulieshindwa kuchagua Kati ya ukristo na usukuma...Hasa kutokana na kuwa na version fake na dhaifu ya ukristo...



Hawa watu wasio na dini wanasheherekea Christmas ipi?? Kulingana na maana halisi ya Hii sikukuu..Au nao wanaomwamini YESU kisiri Siri??
Asante kwa mchango
 
Back
Top Bottom