classic! kuna watu wanataka tuamini tu bila hata kuhoji kuwa endapo tungefanya kila kitu ambacho IMF imetushauri kufanya tusingekuwa hapa tulipo. Well.. miaka 25 iliyopita tumefanya kila kitu ambacho WB, IMF, UNDP, UNICEF, ADB na wenzake wanayotaka tufanye je tunaweza kusema kweli hali yetu ni bora zaidi? Kufanya yote ambayo Mtei alishauri isingekuwa a panacea ya matatizo yetu kama taifa. Ingekuwa just that - tumefanya tuliyoambiwa na wakubwa kufanya hata kama hayakubaliani na misingi yetu kama taifa. Pamoja na heshima yangu yote niliyonayo kwa Mzee Mtei leo hii mapendekezo yake yamefanyiwa kazi kuanzia Mwinyi hadi Kikwete, ameridhika?
Mwanakijiji ukumbuke kuwa SAPs zilisaidia sana kufufua uchumi wa taifa. Ukumbuke Mwinyi alichukua nchi katika hali gani. tulikuwa hoi kwelikweli. Sasa hivi watu wengi wanasahau kuwa reforms and adjustments zilisaidia sana kutuodnia kufani. Tulikuwa na matatizo makubwa sana, sukari, sabuni, nguo, viatu, na mahitaji yote ya msingi yalikuwa adimu sana, kuna wakati mtu unakuwa na hela lakini duka la kaya lilikuwa halina kitu, ukinunua toka nje ya nchi kilitwa cha magendo na uliweza kupelekwa ndani, TV, radio gari ilikuwa ni kama kosa la jinai. Cellphone ilikuwa ndoto kabisa. RTC, NMC yalikuwa kama makaburi ya uchumi wetu.
Tulikuwa na serikali kubwa kupita kiasi, na kama utakumbuka hata akiba yetu ya fedha ilikuwa mbaya sana. Hali ilianza kubadilika baada ya kutekeleza SAPs. Ukiangalia kwa undani package ya SAP ilikuwa na lengo la kufufua uchumi ili upate nguvu ya kuweza kujiendeleza wenyewe, although in a process wengine tuliumia, na wengine kama kina JK na Kinana wakaamua kuacha jeshi na kuingia CCM. Sipigii debe IMF, WB na OECD kwa kuwa ushenzi wao unafahamika sana, lakini kwa kiasi fulani naweza kusema walitusaidia. Weakness bado iko kwetu, viongozi wetu hawaijali Tanzania hawana uzalendo, wanajali mifuko yao na akaunti zao, hata elimu waliyopata wanaitumia kujineemesha wao, sio kuiendeleza Tanzania. Kama kweli kungekuwa na lengo la kuiendeleza Tanzania, na elimu iliypo sasa miongoni mwa watanzania tungekuwa tumepiga hatua sana.
Ni vizuri sana tukiacha kulalamikia wengine wakati uozo mwingi uko ndani, Mwanakijiji sijui lini last time ulikuja Tanzania, unatakiwa uone uozo wa idara zetu za utendaji, uozo wa siasa zetu, na matatizo kwenye sturctures zetu. Ajabu ukiwaliza watu wanasema oh Tanzania today is not like that of 10 years ago, just a pack of crap, wanadanganyika kwa kuweza kuwa na simu za mkononi na laptop, lakini kila kitu kinaenda hovyo. Kitulacho ki nguoni mwetu, hakiko Washington wala London.
IMF, Donors na WB walituacha tujumanage baada ya kuona awamu ya tatu was doing "well" at least in term of implementing SAPs, waliona kama Tanzania ina mwelekeo mzuri and there was even a talk that TZ itakuwa bora zaidi, wakiamini kuwa tumeanza kutumia watanzania waliosoma kumanage uchumi wetu. Lakini awamu ya nne imevurunda kila kitu, tofauti sana na awamu ya tatu. Sasa hivi kuna sera nyingi sana za porojo, kama vile kilimo kwanza, maisha bora kwa kila mtanzania, lakini ukiangalia structures zote zilizopo ambazo zilitakiwa kufanikisha sera hizi ni kama zimekufa. Hakuna kitu kinachoitwa social welfare Tanzania at least in practical terms, angalia structures za wizara nyingi uone kama kweli zimetengenezwa ku deliver the goods. Nyingi unaona ni madawati tu ya kuchumia pesa ya maofisa wa wizara.
Hakuna political leadership inaweza ku-direct, kusupervise na kumanage mwelekeo wa nchi, hii sio siri. They talk about maisha bora lakini hakuna definition of it na targets za maisha bora, they talk about kilimo kwanza as new policy, wanasahau kuwa sera hiyo ni ya zamani sana. JKNyerere alituwekea mabwana shamba kutoka national level hadi village level, aliweza hata kuanzisha UFI (KIZAKU), TRAMA, TFA, kiwanda cha mbolea, tulikuwa na kitu kinaitwa Tanganyika packers, chakula barafu and things like that, serikali yake kweli ilikuwa inatekeleza sera hiyo...today they are fooling us na Kilimo kwanza as if tumesahau real kilimo kwanza. Tunafanywa watoto halafu na sisi tunapiga makofi.
Kwa hiyo Mwanakijiji, pamoja na ukweli kuwa IMF, WB can be questioned, bado Tanzania haijafikia hatua hiyo. We have to put our house in order first before we turn our guns to IMF and WB. Kuna mambo mengi sana tunayoweza kufanya as a country hatujafanya, hata kodi tu tunazotakiwa kukusanya hatukusanyi, hata wezi tunaowajua EPA, Kagoda, Radar tunawachekea, how can we be so brave to pint fingers at bretton wood institutions???
Kama awamu ya nne ingeendelea kujenga ilipofikia awamu ya tatu, ingesahihisha makosa ya awamu ya tatu, kweli tungekuwa tumepiga hatua zaidi. Tatizo ni kuwa wameleta matatizo zaidi na kutufanya tuone kuwa awamu ya tatu was better by far than ya nne. Lakini usishangae kusikia kuwa wameingia ena madarakani.