Elections 2010 Mtei amwonya Kikwete


Moja ya mambo mtei aliyo mshauri Nyerere ni kuacha kusubsidize haya mashirika kama NMC. Kuyaacha haya mashirika yaendeshwe na watu binafsi.

Mifano ya leo ni kuwa baharesa na wauza chakula wengine wanafanya kazi vizuri tu..

Leo hii TZ breweries wamefungua kiwanda kingine mbeya, wakati wa enzi zile usambazaji wa bia tu ulikuwa unawashinda...

Kama hii sera ingetekelezwa kipindi kile viwanda vyetu vingi vingekuwa hai na vinauza mpaka nchi jirani, sasa hivi viwanda vyetu vingi vinapiagana market ya ndani.

Mabadiliko ni makubwa sana yaliyoletwa na hii sera ya ubinafsishaji sio kwa viwanda tu hata kwa bank zetu, productivity imeongezeka.
 
Hivi UDOM inajengwa kwa mapato ya ndani? Nilifikiri ni mkopo wa ndani kwa kupitia NSSF, PPF etc...But also haya mashirika si mashirika ya umma ambayo ni mabaki ya sera za ujamaa?
Hiyo UDOM ni govt bond ambayo NSSF imewekeza kwa serikali. hii inatisha NSSF kuinvest 48% kwenye govt bonds.

Haya mashirika yako katiaka hali mbaya sana kifedha yaani yana pension deficit kubwa sana sijui itakuwaje uko mbeleni. watu wanasumbuliwa sana kupata pension zao.

Haya mashirika yanatakiwa ya binafsishwe ili yaendeshwe kwa ufanisi zaidi. Hizo hela zilizopotea ingekuwa private company watu wangekuwa wananyea debe siku nyingi. Siku haya mashirika yatakapokuwa mahututi ndio tutatafuta wawekezaji
 

mifano yako ni mizuri, lakini unafikiri tatizo ilikuwa ni kusubsidize mashirika ya umma? mashirika yote yaliyobinafsishwa yanafanya vizuri? Kuna mfano wowote wa mashirika ambayo yalibinafsishwa na hayafanyi vizuri?
 

1. Kwa taarifa niliyonayo ni kuwa haya mashirika yana fedha nyingi mno hazina cha kufanyia na ndio maana sasa wanahimizwa sana katika kuinvest katika miradi mikubwa ya umma

2. Hi solution ya kukukimbilia kubinafsisha kila kitu inatisha. Hivi huko mnapocopy utume wa ubepari kama marekani nao wamethubutu kubinafsisha Social Funds?
 
haya mashirika yamewekeza katika miradi ya umma kwa ajili base rate kipindi cha balali ilikuwa juu sana, na kuinvest kwenye govt bonds ni safe kuliko kukopesha. sasa hivi ndulu amejitahidi mpaka base rate ikashuka kwa hiyo returns ni ndogo na hawa jamaa wamepunguza kuwekeza kwenye govt bonds.
kuhusu swala la fedha - kuna losses kubwa sana kwenye haya mashirika nyingine kutokana na bad investment decision na nyingine corruption. hizi losses haziwezi kuonekana sasa hivi kwa ajili private sector imekuwa na wastaafu ambao wanachukua pesa ni kidogo sana (hii ni kama deci wavunaji ni kidogo kuliko wapandaji). hawa pensioner kidogo walio nao wanasumbuliwa sana kulipwa. je ikifika wakati pensioner wengi itakuwaje
NSSF ina losses za more than tsh 60bn, je hizi hela zitarudi vp?? NSSF isipoangaliwa ita cause maafa makubwa sana kwa the so called middle class wa TZ

mareakani ni inchi ambayo ina pension deficit kubwa sana kuliko nchi zote duniani na haijui ifanyeje. state pension ya marekani na nchi za ulaya ziko hoi.
watu wanaoajiriwa upya ulaya na marekani wanapewa terms tofauti sana na wale walioajiriwa zamani.
moja ya shirika la posta royal mail (uk) mali ya serikali lina pension deficit ya £8bn halijui lifanyeje hii pension, sasa hivi linatafuta mwekezaji wa kulinusuru
 
Mnasahau Kwamba ni Mwalimu ndiye alimruhusu Mwinyi kukubaliana na IMF? There was no choice. Sasa kama mwishowe unakubali dawa, si ingekuwa bora kuikubali kabla ya kuingia ICU? Hali mbaya tuliyokuwa nayo miaka ya 78 - 85 ilitokana na kiburi kisichokuwa na msingi mzuri.

Kama wewe ni mzima unaweza kugombana na daktari. Lakini mgonjwa utagombana na daktari?

Nchi nyingi za Afrika zimeanza tena kuendelea baada ya kufuata masharti ya IMF. Tanzania ni mojawapo.

Mwishowe Mwalimu alikubaliana na IMF. That is a historical fact.
 
Hapana. Mwalimu amefariki bila kukubaliana na IMF. Kwenye kikao chake cha mwisho hapa Washington aliwasuta na kuwaambia "have some humility."
 
Hapana. Mwalimu amefariki bila kukubaliana na IMF. Kwenye kikao chake cha mwisho hapa Washington aliwasuta na kuwaambia "have some humility."

Mwinyi hakuruhusiwa na Mwalimu kuwekeana mkataba na IMF? Mwalimu hakukubali IMF inafanya vizuri. Ila alikubali Tanzania ifikie makubaliano na IMF. Angeruhusu hivyo mapema hatungeshuka kiasi kile.

Si lazima ukubali msimamo wa IMF ndio ukubaliane nao. Ukitaka kuwa jeuri basi uwe kweli mwenye uwezo wa kujitegemea. Kama lazima kusalimu amri, basi usichelewe mpaka ukazdiwa kabisa.

History has proven that Mtei was right.
 
I have no problem with history proving Mtei right. Katika hali yetu baada ya vita na Uganda na baada ya western countries to gang together under Reagan's pressure to force Tanzania to bend hatukuwa na choice. It was not a matter of Mwalimu kumruhusu Mwinyi kuwekeana mkataba na IMF. It was the prudent thing to do. But this did not change Mwalimu's belief that IMF' s prescription were not panacea.
 
Jasusi,

I am not saying that Mwalimu changed his views about the IMF. I am saying that he changed his opposition to Tanzania entering into agreement with the IMF. But he waited too long before allowing it.

Mwalimu didn't like the IMF. Neither did I. But that is neither here nor there. The thing is that we didn't have to do just that which Mwalimu liked. He was supposed to do what was best for the country. He should have listened to Mtei. That would have spared us all a lot of pain.
 
Augustine Moshi,
Mkuu wangu hapa utakuwa unakosea sana. na wale wote wanaotaka kumlaumu mwalimu ni lazima wajue pia kwamba IMF iliyokuwa miaka ya 70s sio hii ya leo wala hata ile ya miaka ya 80's.

Ikumbukwe tu kwamba wakati ule tulikuwa subjected to conditinalities ambazo zilihusu zaidi structural policies ili upwe mkopo.. Nchi zililazimishwa kubadilisha Structure Policies ili upate ku qualify kupewa mkopo tofauti na guideline conditionality za leo au hata wakati wa Mwinyi ambapo sharti moja kubwa lilikuwa kufuata Macroeconomic policies.

Sasa tunaporudi kwa Mzee Mtei ni muhimu tufahamu kwa nini Nyerere alikataa na hata kuwafukuza wale jamaa wa IMF kwani haikuwa sababu ya kutopenda mikopo isipokuwa masharti yake ndio yalikuwa magumu kwa Nyerere, ati abomoe kabisa kile alichokijenga na kuanza na mfumo mpya ambao utaruhusu vile asivyokubaliana navyo hata chembe (during coldwar).

Ni muhimu sana ktk majadiliano kama haya kuifahamu nafasi ya Nyerere kama ingekuwa sisi ktk nbafasi yake hata kama alifanya makosa...Ni sawa na leo hii mkuu wangu unataka kumwoza mwanao lakini washenga wanakwambia ili mwanao aolewe ni lazima abadilishe dini kuwa Muislaam wakati wewe mlokole wa Kikristu..(samahani kwa mfano huu)..Sasa aje mtu wako wa karibu akwambie mkuu wangu wale washenga wamekuja tena wanataka kusikia msimamo wako..Nina hakika utawafukuza napengine hata huyo rafiki yako ushikaji ukafa!..

Matokeo ya maisha ya mwanao baada ya wewe kukataa asiliolewe kwa kubadilisha dini yake isiwe sababu ya umaskini wake leo hii kwani binafsi nadhani hii ni dharau ya yaliyotangulia na madhara yake.. Nikirudi ktk mfano huo hapo juu, mimi sioni mantiki ya kukulaumu wewe mzazi kwa sababu tu ulimkataa mume tajiri wa kukutoa wewe na mwanao kwa sharti ambalo mimi kama Muislaam sioni ubaya wake..Na ndio wachangiaji wengi hapa wanamtazama Nyerere hivyo kwani wote hawa hapa hawakuupenda Ujamaa (imani ile) hivyo lolote ktk imani yao ndio lilikuwa bora zaidi pasipo kufanya utafiti wa imani yao kama iliweza kuzaa matunda kwa nchi maskini zilizoufuata masharti ya IMF wakati ule.

Hadi Usocialist unaanguka hakuna nchi yeyote maskini ilifanikiwa kwa mikopo ya IMF tena basi historia itatukumbusha kwamba miaka hiyo ya 70s fixed exchange rate system ilibomoka kila nchi zikawa zinatumia lots of different exchange rate systems. Mara mbili kulikuwa na oil shocks, ambapo bei ya mafuta ilipata vibaya kuliko hata hii ilopita majuzi tukapiga makelele dunia nzima kwani thamani ya Dollar wakati ule ilikuwa ndogo na tofauti na hii ya leo. Kulikuwa na instabilities kibao ktk uchumi wa dunia nzima..hivyo mikopo ya IMF isingeweza kabisa kufanya lolote kwa ushahidi kwamba hata nchi zile zilizochukua mikopo pia zilikwenda chini kiuchumi.

Sasa turudi wakati wa Mwinyi, moja muhimu la sisi kutambua ni kwamba masharti ktk guideline ya IMF ili watoa mikopo yao ilifanyiwa marekebisho makubwa baada ya kushindwa kufanya kazi miaka ya nyuma. Na hakuna mtu hapa anayeweza kunionyesha nchi maskini hata moja ilopata mkopo toka IMF wakati wa Nyerere ikafanikiwa kwani HAKUNA.... hata zile zilizokuwa Mapebari zilishindwa kuendelea zaidi ya kushuka kila mwaka ktk GDP zao..Kwa hiyo ni baada ya Ujamaa kufa na mwalimu kukubali Kung'atuka ndipo Ubepari ukapata mwanya wa kupenya ktk uchumi wetu na kwa sababu kilichotakiwa sasa kilikuwa performance criteria haikuwa kazi kubwa kwetu kukubali masharti ya IMF ambayo yaliijenga economic recovery plan hiyo mikakati ya SAP na kama sikosei wachumi wengi walipingana nayo..Nadhani hata Mtei (kama sikosei) pia hakukubaliana na yote yaliyoorodheshwa ndani ya mkakati huo. Kwa hiyo kuingia IMF haikuwa na maana ni neema tupu hata kidogo...

Wakuu zangu, Mtei alizungumzia hali iliyokuwepo wakati ule na nakuhakikishieni hakuna guarantee yoyote ya mafanikio kama tungechukua mikopo ile chini ya masharti yaliyokuwepo. Pengine Nyerere mwenyewe asingeweza kuongoza nchi ktk mfumo huo kwani kila kiongozi bora huwa na vision ya kile anachotaka kukijenga. Ni sawa na maneno ya Rev. Kishoka.. rais ni sawa na mtu aliyeko juu akiutazama msitu mzima na kutuelekeza sisi tulo chini tukiona mti baada ya mti na sii msitu mzima jinsi ya kwenda mbele tukifuata dira yake. Ukimweka chini naye akaongozwa na mtu mwingine kuna hatari ya sisi wote kupotea kwani dira haitakuwa yetu isipokuwa ya kupangiwa safari tusojua woote. Someni dossier hii

Na kwa kumalizia tu ni kwamba leo hii tunachukua mikopo pengine kuliko nchi nyingi za Kiafrika sasa iweje tunashindwa leo hali hatupo na Nyerere wala ktk Ujamaa!!!?.. Je ndio kusema Nyerere was right as well..
 
Baadaye Nyerere alionyesha, kwa matendo, kwamba ushauri wa Mtei ulikuwa sawa. Ndio kisa cha kumteua akafanye kazi IMF. Kwenye kitabu cha Mtei, ambacho naamini umekisoma, kuna maelezo mazuri kuhusu ni nini kiliwakosanisha. Mwishoni Mwalimu alikataa hata kujadiliana na IMF. "Hakutaka kuwa jiwe."

Ghana, na hata Tanzania, ni nchi zilizogeuka kutoka kudidimia na kuanza kukua tena kiuchumi, kutokana na kutimiza masharti ya IMF.

Mimi nakumbuka kuwatumia ndugu zangu Dar toothpaste, kutoka Ottawa, kwenye miaka ya 80. Nilikuwa nawapostia sabuni vile vile. Hii ilitokana na Mwalimu kutoambilika. Mwenyewe alikuwa anahubiri kwamba tunakosa sabuni na madawa kwa sababu ya kasi ya maendeleo!
 

Ili gazeti ni la mwaka huu au mwaka jana? Nimeishia kusoma para ya pili baada ya kukutana na hiyo red! Au ni makosa ya kiuchapaji?
 
Hawa ndiyo wazee tunaowataka wanaoweza kumwambia kijana wao ukweli sio wazee km akina makamba wanaomdanganya kiongozi wao huku wakijua kuwa hawamtendei haki na wanazidi kumwangusha................pamoja na hayo mzee wetuy mtei umechelewa kumpa kijana wako ushauri kwani watz tayari wameona kuwa ni kiongozi dhaifu na anawasaidizi dhaifu kwa hiyo kabla ya wewe hujamshauiri afanye kitu watz tayari tumeshamhukumu na tayari ccm imeanguka anguko kuu............
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…