MTFE imeenda na kijiji

hermanthegreat

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2021
Posts
1,274
Reaction score
3,282
Wakuu.

Ni kilio Cha jamaa angu kilisikika huku akionekana kughadhabika Sana akidai kuwa.

Platform maarufu ya forex ijulikanayo kwa jina la MTFE imewaliza watu baada ya pesa kukataa kutoka.

Kila walijaribu Kutoa pesa wanaambiwa Kuna tatizo limejitokeza wajaribu tena baada ya siku saba, lakini siku saba zimeisha na hakuna matumaini yoyote bado tatizo ni lilelile.

Kama ilivyo kwa platform zingine ambazo hutoweka na pesa za watu, MTFE nayo imefanya hivo.

tuwaombe vijana wenzetu wa kitanzania waliokuwa wamewekeza dola nyingi kwa ndoto kubwa.
 
Kuna mjeda kastaafu akashawishiwa na mwanachuo.
Si akaweka pesheni yake yote MTFE.
YAAANI NI VILIO TUUU.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]dah,nacheka kama mazuri aisee

Pole yake,na awaseamehe tu
 
Omba isikukute.
Sema mimi jamaa zangu niliwatahadharisha kitambo wakawa wananilingishia kwenye ubao inasoma 1000$ nikasema we uliona wapi mtu unaweka hela tu af izae yenywe🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣.
Mnaotapeli endeleeni kutapeli maana wabongo ni vichwa ngumu
 
Mpya ni ipi,kwanini zikiwa mpya amshirilishi zikianza kuzama ndio mnashirikisha.Kwa hiyo ulikuwa unaweka ngapi unapata ngapi
 
Nimefurahishwa sana na hizi taarifa. MTFE wamesaidia kupunguza wajinga ndani ya nchi. Watu hawataki kazi acha wapigwe tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…