Mtibwa Sugar wadai Miwa imeharibika sana haifai kwa uzalishaji

Mtibwa Sugar wadai Miwa imeharibika sana haifai kwa uzalishaji

Mjanja M1

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2018
Posts
4,058
Reaction score
14,382
Uongozi wa kiwanda cha Mtibwa Sugar umesema kuwa miwa mingi imeharibika na haifai tena kwa uzalishaji wa sukari hali inayopelekea bidhaa hiyo kuadimika.

Mvua juu ya wastani zinazoendelea kunyesha nchini zimesababisha sehemu kubwa ya mashamba ya miwa kujaa maji na kufanya kazi ya uvunaji wa miwa kushindwa kufanyika.

Kamati ya Bunge Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo ambayo jana ilitembelea kiwanda cha Mkulazi pamoja na Mtibwa Sugar na kuelezwa kuwa jambo hilo limechangia bei ya sukari kupanda.
 
Hiv hawa jamaa labda hawawez kwamba msimu unapokuwa mzuri wawe wanaproduce highest amount of sugar, then wanaipack store kisha kuitoa taratibu kadri muda unavyokwenda? Mana hii kero ya mvua ni toka nipo mdogo naisikia, haiwaletei hasara ? Si bora wawe wanaproduce miez 9 mitatu wanapumzika
 
Na mbaya zaidi wazalishaji wa sukari ndo wenye vibari vya kuagiza sukari inayo pelea kutokana na uzalishaji wa ndani kuto tosheleza Soko.

Hii ni hujuma ya wazi wazi kwa Watanganyika.
 
Back
Top Bottom